Kambi ya taifa stars kuanza leo

Wachezaji 26 wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ walioteuliwa na kocha Etienne Ndayiragije wameanza kuripoti kambini leo tayari kuanza maandalizi ya mchezo dhidi ya Kenya wa kusaka nafasi ya kucheza fainali za CHAN utakaopigwa Julai 28, uwanja wa Taifa

Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF mapema leo, Stars inatarajiwa kuweka kambi kwenye Hotel ya APC, Mbweni kujiandaa na mchezo huo

Wachezaji saba wa Simba ambao wako Afrika Kusini kwenye kambi ya mabingwa hao wa Tanzania Bara, watalazimika kurejea nchini kuungana na wenzao

Nyota wa Simba walioitwa kwenye kikosi cha Stars ni Aishi Manula, Gadiel Michael, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Hassani Dilunga, Ibrahim Ajib na John Bocco

Hatua ya Awali ya Klabu Bingwa Barani Afrika…

πŸ‘‰ Hatua ya Awali ya Klabu Bingwa Barani Afrika…
Yanga SC v Township Rollers (Botswana).
Simba SC v UD Do Songo (Msumbiji).
KMKM v Desportivo De 1 Agosto (Angola).
:
πŸ‘‰ Hatua ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika…
Azam FC v Ethiopia 1 (Ethiopia)
KMC FC v AS Kigali (Rwanda)
Malindi SC v Mogadishu City FC (Somalia).
#CAFCC #CAFCL #TotalCAFCC #TotalCAFCL

ZESCO United ambao ndio Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Zambia πŸ‡ΏπŸ‡², Wametangaza Washindi Mbalimbali wa tuzo za msimu ndani Klabu yao

– ZESCO United ambao ndio Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Zambia πŸ‡ΏπŸ‡², Wametangaza Washindi Mbalimbali wa tuzo za msimu ndani Klabu yao; Katika tuzo hizo Mshambuliaji, Lazarous Kambole kajibebea tuzo Tatu licha ya kuuzwa Mapemaa mwezi Uliopita kwenda Klabu ya @kcfcofficial ya Afrika Kusini..
:
– Tuzo Alizobeba Kambole Ni…
πŸ‘‰ Mchezaji Bora wa msimu wa ZESCO United.
πŸ‘‰ Mchezaji Bora wa Wachezaji wa Mwaka.
πŸ‘‰ Mchezaji Mwenye Nidhamu wa Mwaka..
:
– Kambole mwenye umri wa Miaka 25 Amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu kuwatumikia Miamba hao wa Soweto, Nyota huyo wa Chipopolo anatarajia kucheza Mchezo wake wa kwanza akiwa na jezi ya Amakhosi wikendi ijayo Kwenye game ya CBL Cup dhidi ya Mahasimu wao, Orlando Pirates.
#Updates #ZescoUnited
@Sokawaytz_

Design a site like this with WordPress.com
Get started