
Kiungo wa klabu ya Liverpool na James Milner mwenye umri wa miaka 33 amesema mpaka sasa hajui hatma yake ndani ya klabu hiyo licha ya kwamba anataka kusalia. (Liverpool Echo)

Kiungo wa klabu ya Liverpool na James Milner mwenye umri wa miaka 33 amesema mpaka sasa hajui hatma yake ndani ya klabu hiyo licha ya kwamba anataka kusalia. (Liverpool Echo)


Siku kama ya leo miaka 17 iliyopita Manchester Utd walimsajili Rio Ferdinand


#DealDone Aliyekuwa Golikipa wa Simba Sc na Mbao Fc Emmanuel Mseja ametua Dodoma Jiji Fc kwa mkataba wa mwaka mmoja.

U


Uzi mpya wa nyumbani wa Orlando Pirates ya Afrika Kusini utakaotumika msimu ujao wa 2019/20

Klabu ya Beijing Guoan ya China imetoa ofa ya mshahara wa £1m kwa mwezi ili kupata saini ya mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale ambaye hayupo kwenye mipango ya Zidane msimu huu. (Mirror)


Azam FC imevuliwa ubingwa wa Kagame Cup baada ya kufungwa 1-0 na KCCA ya Uganda kwenye mchezo wa fainali uliomalizika hivi punde.


OFFICIAL | Aliyekuwa Beki wa Klabu ya Simba SC ya Tanzania 🇹🇿, Zana Coulibally Amewasili Jijini Kinshasa Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa N’djili ( N’djili International Airport) kukamilisha Usajili wake wa kujiunga na Klabu ya AS Vita Club 🇨🇩… Simba SC imeachana na Beki huyo wa Kimataifa wa Ivory Coast..
#TransferNewsUpdates

Kitendo cha Shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) kuipanga Simba hatua ya awali ya michuano ya ligi ya mabingwa, kimevuruga ratiba ya timu hiyo kuelekea Tamasha la SIMBA DAY linalofanyika kila mwaka
Simba inapaswa kusafiri kwenda nchini Msumbiji kuumana na USD Songo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya awali ambao utapigwa kati ya tarehe 09, 10 au 11 mwezi wa nane
Hivyo hakuna uwezekano SIMBA DAY kufanyika August 08 kama lilivyofanyika miaka yote
Hata hivyo msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara amesema Tamasha hilo litafanyika, lakini huenda kutakuwa na mabadiliko ya tarehe


Mabingwa wa soka Tanzania Bara Simba wataanza kampeni ya kutinga hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa kumenyana na US Songo ya Msumbiji katika mchezo wa hatua ya awali
Simba itaanzia ugenini katika mchezo wa kwanza utakaopigwa kati ya August 09-11 na itamalizia mchezo wa pili uwanja wa Taifa kati ya August 23-25
Kama Simba itafanikiwa kuvuka raundi ya awali, katika raundi ya kwanza itamenyana na mshindi wa mchezo kati ya Platinuma Fc ya Zimbabwe dhidi ya Nyasa Bullets ya Malawi
Ushindi katika hatua hiyo utaipeleka Simba hatua ya makundi
Mwanzo kulikuwa na taarifa kuwa Simba ingeanzia raundi ya kwanza.
Hata hivyo kulingana na droo iliyofanywa na CAF, itacheza kuanzia hatua ya awali

Achana na kiwanja cha nyasi bandia ambacho kinasubiri kutandikwa nyasi hizo baada ya zoezi la kuweka miundombinu kukamilika
Mabingwa wa nchi Simba, huko Bunju watakuwa na viwanja viwili ambapo wakati huu tayari ujenzi wa kiwanja kingine kitakacho-pandwa nyasi asili unaendelea
Kisima cha maji yatakayotumika kumwagilia kiwanja hicho kimechimbwa na sasa zoezi la kutandaza mbolea linaendelea kabla ya nyasi hizo kupandwa
Uongozi wa Simba umedhamiria kumaliza ujenzi wa viwanja hivyo haraka kwani mradi huo ulipaswa kuwa umekamilika tangu mwezi wa pili
Mtendaji Mkuu wa Simba Crescentius Magori amesema hadi kufikia mwezi Oktoba mwaka huu, uwanja huo utakuwa tayari kwa matumizi
