Herve Renard amejiuzulu kama kocha mkuu wa Morocco

– Herve Renard amejiuzulu kama kocha mkuu wa Morocco baada ya timu hiyo kutolewa mapema katika Michuano ya kombe la mataifa ya Afrika…Morocco ni mojawapo wa timu zilizopigiwa upatu kabla ya kuanza kwa mahsindano hayo Misri 2019 lakini ilishindwa kufanya vema baada ya kutolewa kwa mikwaju ya penalti dhidi ya Benin katika hatua ya 16 Bora.
.
– Renard, raia wa Ufaransa amewahi kushinda mataji mawili ya AFCON akizifundisha timu za taifa za Zambia Mwaka 2012 na Ivory Coast mnamo mwaka 2015, Kocha huyo alikiongoza kikosi cha Morocco tangu Februari 2016, na Pia Renard aliitoa Morocco kutoka nafasi ya 81 katika orodha ya Viwango vya Ubora wa soka vya FIFA Duniani hadi katika nafasi ya 47.
.
– Aliyewahi kuwa kocha Mkuu wa Klabu ya PSG, Laurent Blanc ameripotiwa kuwepo Katika Mazungumzo na Shirikisho la Soka Nchini Morocco 🇲🇦 kwa ajili ya kuchukua Mikoba hiyo iliyo wazi kwasasa..
#Updates #transfersUpdates

Mshambuliaji wa Klabu ya, Al Merrikh ya Sudan, Saif Eldin Malik amekamatwa na Polisi

🏻 Mshambuliaji wa Klabu ya, Al Merrikh ya Sudan, Saif Eldin Malik amekamatwa na Polisi na kwasasa yupo Chini ya Uangalizi wa Polisi wa Nchini humo kwa wiki ya Pili Hivi Sasa, Nyota huyo anatuhumiwa kwa vitendo vya uporaji wa mali za umma wakati wa mapinduzi ya Sudan, licha ya mchezaji huyo kukataa mashtaka yote dhidi yake..
:
✍🏻 Kwa Mujibu wa Taarifa kutoka Nchini Sudan Ni kwamba, moja ya Jengo la huduma za Kiserikali lilivunjwa na baadhi ya vitu kupotea… Miongoni mwa watu wanao tuhumiwa kufanya uharibifu Huo huyu Mchezaji, lakini kwa Upande wake anasema hakufanya hivyo… Kwa Upande wake Klabu yake ipo kimya na Wala haijatoa Taarifa yoyote na Wala kumtetea Mchezaji wao!..
#Updates
@Sokawaytz_

Ratiba ya #Taifastars kufuzu Afcon Mwaka 2021.

Ratiba ya #Taifastars kufuzu Afcon Mwaka 2021.

Kiuhalisia Taifa stars inahitaji kujiandaa mapema sana katika harakati hizi za kufuzu Afcon Mwaka 2021 kwani Kundi letu sio Jepesi ni Kundi Gumu sana.
:
Tusitegemee mteremko katika kundi hili
Ambalo wapo wababe kama
Equatoriol Guinea
Libya
Tunisia :

Kilala Kheri Taifa stars katika Maandalizi ya Mchezo dhidi ya Kenya kufuzu Chan Nchini Cameroon
@sokaonline_
@sokawaytz_
@full_sokatzz

Tottenham wanajiandaa kumsajili kiungo wa kati wa Real Betis na Argentina, Giovani lo Celso, 23 Ambaye aliifungia Real Betis mabao 16

Tottenham wanajiandaa kutumia tena kitita kikubwa cha fedha wiki hii kukamilisha usajili wa kiungo wa kati wa Real Betis na Argentina, Giovani lo Celso, 23 Ambaye aliifungia Real Betis mabao 16 msimu uliopita….pamoja na winga mwenye umri wa miaka 19 wa Fulham na England, Ryan Sessegnon Ambaye Fulham wanataka pauni milioni 40 kumuachilia Sessegnon.
#TransferNewsUpdates

Aston Villa Imethibitisha kumsajili Mshambuliaji wa Kimataifa wa Misri, Mahmoud Hassan

– Aston Villa Imethibitisha kumsajili Mshambuliaji wa Kimataifa wa Misri, Mahmoud Hassan anaejulikana kwa jina Maarufu, Trezeguet amabaye kajiunga na Villa akitokea Klabu ya Kasimpasa ya Uturuki.
.
– Trezeguet 24; Imeripotiwa kuwa kasajiliwa kwa dau la £8.5m, ambalo litaongezeka kulingana na Ubora wa Mchezaji akiwa na Villa, anatua Uingereza Baada ya kutoka kuitumikia timu yake ya taifa ya Misti Katika fainali za mataifa ya Afrika “AFCON” wao wakiwa wenyeji lakini hawakufanya vema!.
.
– Trezeguet Ni Usajili wa Tisa kwa @AVFCOfficial Baada ya kuwasajili, Wesley, Tyrone Mings, Matt Targett, Ezri Konsa, Anwar El Ghazi, Bjorn Engels, Jota na Kortney Hause ambao wote watahudumu Villa Park Baada ya Klabu hiyo kurejea Premier League..
#EPLTransfersUpdates #EPLUpdates

Kikosi cha Zesco United kwa ajili ya Mshindano ya Klabu Bingwa yatakayoanza Mwezi Ujao

Kikosi cha Zesco United kwa ajili ya Mshindano ya Klabu Bingwa yatakayoanza Mwezi Ujao.
:
Goalkeepers
Jacob Banda
Samson Banda
Dieudonné Ntibahezwa
:
Defender
Marcel Kalonda
Fackson Kapumbu
Shemmy Mayembe
Clement Mwape
David Owino
Solomon Sakala
Simon Silwimba
:
Midfielder
Anthony Akumu
Misheck Chaila
John Ching’andu
Logic Ching’andu
Kondwani Mtonga
Mwape Mwelwa
Kosuke Nakamachi
Mwila Phiri
Edward Tembo
Quadri Kola
Thabani Kamusoko
Sabumukama Enock
:
Strikers
Jesse Jackson Were
Kalengo Winston
Savior Nkonkola
Kasumba Umaru

#SokaPlaceUpdates #cafchampionsleague

📆 Siku kama ya leo mwaka 2013, klabu ya Arsenal iliweka dau la £40,000,001 ili kumsajili nyota wa Liverpool Luis Suarez (kwa wakati huo) 💰

📆 Siku kama ya leo mwaka 2013, klabu ya Arsenal iliweka dau la £40,000,001 ili kumsajili nyota wa Liverpool Luis Suarez (kwa wakati huo) 💰

Design a site like this with WordPress.com
Get started