Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Zimbabwe “The Warriors”, Sunday Chidzambwa Ametangaza kuachia Ngazi

OFFICIAL | Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Zimbabwe “The Warriors”, Sunday Chidzambwa Ametangaza kuachia Ngazi Mara moja Katika Nafasi yake hiyo ya ukocha Mkuu.
.
– Hakuna Sababu aliyotoa Katika barua yake ya kujiuzulu, Chidzambwa anatajwa kuwa ndiye Kocha Mwenye mafanikio makubwa Katika historia Makocha wa timu hiyo ya taifa… Akiinoa Zimbabwe.
✍🏻 Kaiwezesha Kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika “AFCON” Mara mbili 2004 na 2019.
✍🏻 Kaiwezesha kutwaa Ubingwa wa Michuano ya COSAFA Cup Mara Nne..
.
– Sunday Chidzambwa anabwaga Manyanga Siku chache kabla ya Zimbabwe kucheza Mchezo wao wa kuwania Kufuzu kwa CHAN dhidi ya Mauritius; Kocha huyo hii leo kawaongoza Wachezaji kufanya mazoezi kujiandaa na mchezo huo, haijulikani Nani atabeba Mikoba hiyo iliyoachwa wazi… Lakini Wasaidizi wake, Rahman Gumbo na Lloyd Mutasa wanaendelea kuinoa timu!.
#Updates
@Sokawaytz_

Mwinyi Zahera, Kocha Mkuu Yanga SC.. πŸ—£οΈ “Kuhusu Dante, Juma na Yondani…

Mwinyi Zahera, Kocha Mkuu Yanga SC..
πŸ—£οΈ “Kuhusu Dante, Juma na Yondani… nnachojua likizo ya Yondani iliisha siku anaitwa kambini timu ya Taifa pia Mimi siidai Yanga SC hata elfu Moja, siwadai pesa yoyote na sijawahi wakopesha hela kwa kusafirisha timu ama kutoa posho”
.
“nilipewa likizo ya siku 15 na ilianza tarehe 13 siku niliyoondoka Misri, kama mnajua mahesabu nadhani mtajua napaswa kurudi lini…siwezi kumtuma mtu akaniongelea jambo lolote linalonihusu ntaliongea mimi mwenyewe”.
#EPLUpdates

Real Madrid. Mfaransa, Paul Pogba, 26,

Uwezekano wa Real Madrid kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United Mfaransa, Paul Pogba, 26, utategemea kuondoka kwa Mshambuliaji wa Kimataifa wa Wales, Gareth Bale, 30 ndani ya klabu hiyo ya Uhispania.
.
– Bale, ambaye anapokea pauni 550,000 kwa wiki katika uga wa Bernabeu, ambako ana mkataba wa hadi mwaka 2022, anataka marupu rupu yake Katika Mkataba wake uliosalia ili kuondoka Real Madrid..
#TransferNewsUpdates

Klabu ya Yanga SC Imethibitisha kuwa itacheza mchezo wa Kirafiki dhidi ya Kariobangi Sharks

OFFICIAL | Klabu ya Yanga SC Imethibitisha kuwa itacheza mchezo wa Kirafiki dhidi ya Mabingwa wa SportPesa Super Cup na SportPesa Cup, Klabu ya Kariobangi Sharks kutoka Nchini Kenya πŸ‡°πŸ‡ͺ Siku ya kilele Cha Wiki ya Mwananchi, Agosti 04,2019.
.
– Klabu ya hiyo Pia Imethibitisha kuwepo kwa Burudani kutoka kwa Wasanii Mbalimbali Siku hiyo ambayo Watatambulisha Wachezaji wapya klabuni, Jezi Mpya za msimu na wimbo wa klabu… Mabadiliko ya Timu waliyopanga Kucheza nayo yametokea Baada ya AS Vita ya DR Congo πŸ‡¨πŸ‡© iliyopangwa awali, kuthibitisha kuwa haitacheza mechi hiyo ya kirafiki Baada ya Tarehe kuingiliana na Ratiba za Michuano ya Kimataifa ya CAF..
#Updates
@Sokawaytz_

Callum Hudson-Odoi asaini Mkataba Mpya wa Miaka Mitano Kuendelea kuitumikia Chelsea

✍🏻 Mshambuliaji Kinda wa Kimataifa wa Uingereza, Callum Hudson-Odoi amekubali Kusaini Mkataba Mpya wa Miaka Mitano Kuendelea kuitumikia Klabu yake ya Chelsea, Mkataba wake Mpya anatarajia kupokea Mshahara wa £100k kwa kila Wiki.
.
✍🏻 Hudson-Odoi 18, aliwasilisha ombi la kutaka kuuzwa na Klabu hiyo mwezi January na Chelsea ilikataa dau la Β£35m kutoka kwa Mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich… Lakini Sasa kwa mujibu wa @bbcsport, kinda huyo “Amesinyaa”.
.
✍🏻 Kwa Sasa Mchezaji huyo yupo Katika hatua za kupona Majeraha yake ya mguu aliyoumia mwezi wa April akiitumikia Klabu yake hiyo, na Sasa ataanza Mazoezi Mepesi mwezi September Mwaka huu..
#TransferNewsUpdates #transfers
@Sokawaytz_

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬ , Umar Kasumba amekamilisha Usajili wake wa kujiunga na Mabingwa wa Zambia, Klabu ya ZESCO United

– Mshambuliaji wa Kimataifa wa Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬ na Klabu ya Sofapaka FC ya Nchini Kenya, Umar Kasumba amekamilisha Usajili wake wa kujiunga na Mabingwa wa Zambia, Klabu ya ZESCO United… Msimu uliopita ndani ya ligi kuu Nchini Kenya aliweza kufunga Magoli 17 akiwa na Klabu ya Sofapaka FC..
.
– Kasumba 25; Amewasili Nchini Zambia tayari kuanza Majukumu ndani ya Klabu yake mpya. Ametua kuchukua nafasi ya, Lazarous Kambole aliyesajiliwa na Kazier Chiefs ya Afrika Kusini…
#TransferNewsUpdates
@Sokawaytz_

OFFICIAL: Real Madrid wamethibitisha kuwa winga wa Kimataifa Hispania na Klabu hiyo, Marco Asensio amepata Majeraha

OFFICIAL: Real Madrid wamethibitisha kuwa winga wa Kimataifa Hispania na Klabu hiyo, Marco Asensio amepata Majeraha Katika goti lake la mguu wa kushoto wakati wa mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Arsenal na atafanya upasuaji siku zijazo… Taarifa za Awali, atakosa msimu mzima 2019/20!.
#Updates

Bondia raia wa Urusi, Maxim Dadashev ameaga dunia baada ya pambano lake dhidi ya Mpinzani wake, Subriel Matias

Bondia raia wa Urusi, Maxim Dadashev ameaga dunia baada ya pambano lake dhidi ya Mpinzani wake, Subriel Matias kumsababishia majeraha makubwa ya ubongo… Dadashev mwenye umri wa miaka 28, alishindwa kutembea mwenyewe baada ya pambano hilo ambalo mkufunzi wake Buddy McGirt alilazimisha lisimamishwe katika raundi ya 11 baada ya bondia huyo kupokea kichapo kikali bila majibu.
.
– Pambano hilo lilipigwa Ijumaa wiki iliyopita. Na punde tu baada ya pambano Dadashev alikimbizwa hospitali…Madaktari waligundua kuwa damu ilikuwa ikimvuja kwenye ubongo na kufanyiwa upasuaji wa haraka, lakini akafikwa na umauti jana Jumanne.. #RIPDadashev
#Updates

Design a site like this with WordPress.com
Get started