

– Rais wa Klabu ya Zamalek, Mortada Mansour amemwachisha kazi Kocha Mkuu wa Klabu hiyo, Khaled Galal mda mchache Baada ya kupokea kipigo Katika Mechi ya Derby ya Cairo Jana Jumapili… Pia ametangazwa Klabu inayomtaka Nahodha wa timu hiyo, Mohamed Ibrahim waende mezani kuzungumza… Sababu kaonesha kiwango kibovu 🙄😄🙌..
.
– Al Ahly iliyokwisha twaa Ubingwa iliikaribisha Zamalek huko Borg El-Arab katika Mechi ya mwisho kabisa ya Ligi Kuu Nchini Misri, Ahly walishinda Mechi yao kwa Goli Moja Pekee la Dakika ya 58 kutoka kwa shujaa wa Al Ahly, Ali Maaloul.
.
– Dakika chache baada ya mchezo, Mortada Mansour alitangaza kutimuliwa kwa Khaled Galal na wafanyikazi wake wote wa Benchi la Ufundi…Galal alirudi kwa Mara ya Pili kuchukua jukumu la kuinoa Zamalek baada ya kuondoka kwa Aliyekuwa Kocha Mkuu Raia wa Uswizi, Christian Gross mnamo Mei 31…Tangu wakati huo, Galal aliifundisha Zamalek katika michezo minne ya ligi, na timu hiyo ikikusanya pointi tano tu kati ya 12 baada ya kutoa sare na Haras El-Hodood na El-Gouna, ushindi dhidi ya Ismaily, na kupoteza game ya Cairo derby dhidi ya Al Ahly ambayo ilikuwa ndio ya mwisho kwake ndani ya Zamalek..
#TransferNews #Alahly
@Sokawaytz_














