
1: Mechi ya Mbinu🙌 4-2-3-1 ya Luc Aymael dhidi ya 4-1-4-1 ya Katwila. Tofauti ya hii mechi ilikua nguvu, kasi na pasi sukari ya Ditram Nchimbi
.
.
2: Mtibwa walikua bora walipokua na mpira, wakawa dhaifu mno bila mpira. Kama si uwezo wa Humud, kwenye kuwapress viungo wa Yanga, Mtibwa ingekuwa kwenye madhara makubwa mno
.
.
3: Yanga wamebadilika sana kimuundo. Build up wanafanya watu watatu mpaka wanne. Top level kabisa hii🙌 Changamoto kubwa waliobaki nayo ni kwenye ‘penetration phase’. Bado movement za mastraika hazijakua bora kupokea pasi bora za viungo .
.
4: Shomari Kibwana🙌 Dakika 90 bora sana kutoka kwake👏 Alimuweka Morrison kwenye mfuko wa kushoto, mfuko wa kulia, akatoa silaha zake kuishambulia ngome ya Jafari Mohamed
4: Ubora wa Jafari kimbinu kwenye nidhamu ya kukaba ulimpa wakati mgumu Kihimbwa kukimbia kwenye nafasi, lakini Jafari aliwanyima Yanga faida ya Morisson kukabwa na watu wawili
5: Humud🙌 Mechi bora sana kwake. One of the best Holding Midfielder wa kisasa kwenye Ligi yetu kwa sasa. Anakuwepo kuanzisha build up, anakuwepo kupress timu inapokosa mpira. Amenikosha sana👏
6: Makapu🙌 Aisee. Inavutia kumtazama Makapu huyu. Amebadilika mno. Timing zake kuwania mpira zimeimarika mno. Utulivu umerejea. Bila shaka Lamine Moro ana mchango kwenye mabadiliko haya kama beki kiongozi wa Yanga
7: Kama Katwila angekua na uthubutu mapema wa kuanza na ‘double striker’, pengine angeikamata Yanga mahala pabaya. Ali Makarani hakumpa msaaa mzuri Riphat Msuya, kipindi cha kwanza
8: Leo Nimeona talent mpya🙌 ni yule dogo namba 21 wa Mtibwa.. Somebody Omari Hassan. That Kid is fantastic aisee🙌 Mguu wake wa kushoto una mengi ambayo bado hajatuonyesha, acha niendelee kumsubiri
9: Molinga Falcao👏 Tofauti yake na Yikpe ni kunusa hatari kwenye eneo la mwisho. Nje ya hapo, Tariq Seif anaweza kuja kuwaweka wote benchi siku akirejea uwanjani
10: Niyonzima Haruna, Papy Tshishimbi ndio roho ya plan ya Luc Aymael. Kuimaliza Yanga ni kuimaliza ile nafasi anayoachwa Niyonzima akiwa na mpira
Nb: Alichofanikiwa kupanda leo ni basi la timu tu😀