
Kikosi cha Simba kesho kitarejea mazoezini kujiwinda na mchezo wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom dhidi ya JKT Tanzania, mchezo ambao utapigwa Alhamisi kwenye uwanja wa Uhuru
Benchi la ufundi liliwapa wachezaji hao mapumziko ya siku moja baada ya mchezo wa jana wa ligi ya mabingwa ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1
Mabingwa hao wa Tanzania bara wanahitaji kusahau machungu ya mchezo huo na kuhakikisha wanaanza vyema kampeni ya kutetea ubingwa wao kwa msimu wa tatu mfululizo



















