Simba mliidharau UD songo- asema julio

Nyota wa zamani wa klabu ya Simba Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’ amesema moja ya sababu iliyopelekea Simba kuondoshwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa, ni kitendo cha kuidharau UD Songo

Julio ambaye pia amewahi kuwa kocha wa Simba, amesema baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana kwenye mchezo wa ugenini, pamoja na mafanikio iliyopata Simba kwenye michuano hiyo msimu uliopita, wachezaji waliona watakuwa na kazi rahisi

“Wachezaji walijisahau, baada ya kupata suluhu ugenini kwenye mchezo wa kwanza. Lakini pia wengine wakachukulia mambo yataenda tu kama walivyofanya msimu uliopita,” amesema

“Waliuanza mchezo taratibu wakati wenzao walianza kwa kasi wakihitaji kufunga bao la ugenini ambalo mwisho wa siku limewavusha”

Awaponda Wabrazil

Julio, kocha mwenye maneno mengi pia ameponda usajili wa wachezaji watatu kutoka Brazil akiwatuhumu waliofanikisha usajili huo kuwa wamehujumu fedha za Mo

“Hakuna mbrazili anayeweza kuja kucheza soka Tanzania”

“Watu wa huko wana malengo ya kucheza soka la mbele zaidi, hao wamekuja kutalii tu na si wachezaji mpira, subirini mtaona”

Awali ilielezwa kuwa wachezaji hao walisajiliwa kwa ajili ya michuano ya ligi ya mabingwa hata hivyo ni Fraga pekee aliyepata nafasi ya kucheza kwa dakika chache mchezo wa kwanza dhidi ya UD Songo

Mshambuliaji Wilker Da Silva bado ni majeruhi huku beki Tairone Santos yeye akishiriki mechi moja tu Simba Day

Hata hivyo kocha Patrick Aussems alieleza sababu ya kutowatumia wachezaji hao akisema bado wanahitaji kujifunza utamaduni wa soka la Afrika

Aidha amesema suala la lugha pia ni tatizo linalowafanya wachelewe kuzoea mazingira

Lakini alisema wameonyesha viwango vizuri, na watapewa nafasi kulingana na mahitaji ya mchezo

Real madrid ..majeruhi waongezeka

Real Madrid imekumbana na majeraha mengine kwa Mchezaji wao mwingine, Baada ya Kuthibitisha Kuwa Kiungo Mshambuliaji wao wa Kimataifa wa Colombia, James Rodriguez anasumbuliwa na Maumivu ya Misuli ya ndama.
.
– Kiungo huyo alianza XI kwenye game dhidi ya Real Vallodolid wakitoka Sare ya 1-1 siku ya Jumamosi, alitolewa Baada ya kupata Majeraha na Nafasi yake kuchukuliwa na kinda wa Kibrazil, Vinicius Junior.
.
– Rodriguez 28, anatarajia kufanyiwa uchunguzi wa kitibabu juu na majeraha hayo na Madrid Imethibitisha Kuwa haijulikani Ni Muda gani nyota huyo anarejea tena kuitumikia Klabu yake!.
#LaligaUpdates
@Sokawaytz

Neymar..Ronaldo..sio bora katika la liga…asema raisi wa la liga

Rais wa La Liga, Javier Tebas anasema wote Neymar na Cristiano Ronaldo sio muhimu kwa ligi hiyo kama Lionel Messi, ingawa ameongeza kwamba angependa kuona nyota wa Paris Saint-Germain, Neymar akirudi kucheza Uhispania.
:
– Neymar amehusishwa na kurudi ndani ya Ligi Kuu Uhispania msimu huu wa joto, na tayari akiwa amekosa michezo yote mitatu ya kwanza ya kampeni ya Ligue 1 ambayo Klabu ya imeshuka dimbani!.
.
– Kurudi Barcelona kunaonekana Kuwa na uwezekano mkubwa, hasa ni Baada ya Mabingwa hao kuanza kupunguza Nyota wao Kikosini kwa kumtoa kwa mkopo Philippe Coutinho Kwenda FC Bayern Munich, wakati Real Madrid pia wapo Katika mbio za kuwania saini ya Neymar!.
#TransferNewsUpdate
@Sokawaytz

Simba sc.kuhamishia nguvu ligi.kuu na FA

Baada ya kuondolewa.katika michuano ya klabu bingwa afrika ..mabingwa wa nchi simba sport club sasa ..nguvu yao yote wanaiamishia katika mashindano ya ligi kuu tanzania bara(Vodacom premia league ) pamoja na kombe la FA.

“Malengo yetu kwa sasa ni kufanya vizuri kwenye mashindano yote kuanzia Ligi Kuu, kombe la FA na mingine ambayo tutashiriki”Kocha Mkuu Patrick Aussems.

Simba kwa sasa.wanaingia kambini kujiandaa na mchezo wao wa ligi kuu tanzania bara unaotarajiwa kupigwa hapo kesho…hivyo simba wanatakiwa kufanyaaandalizi ya kutosha ili kuhakikisha wanauanza vyema msimu wa mwaka 2019/20..ili kurejesha furaha iliyopotea kwa mashabiki

#update habarizamichezo

Ivan Rakitic Kikosa namba barcelona sasa kuelekea juventus

– Ivan Rakitic ameambiwa kuwa atakuwa Mchezaji wa ziada kwa mahitaji huko FC Barcelona… Kiungo huyo wa Kimataifa wa Croatia yupo sokoni na Mazungumzo Kati ya Juventus ya Barça yanaendelea!.
:
– Kiungo huyo wa miaka 31 aliachwa kwenye benchi Kwenye game ya ushindi wa 5-2 dhidi ya Real Betis jana Jumapili na alicheza dakika 45 tu wiki iliyopita.
.

– Bado ana miaka miwili iliyobaki kwenye mkataba wake na mabingwa hao wa Uhispania, lakini Barça wameamua kuwa tayari kumruhusu aondoke msimu huu wa joto ikiwa ofa nono juu yake itawekwa mezani!.
#TransferNewsUpdate
@Sokawaytz

Mbappe..kapata majeraha…..atakaa nje muda usiojulikana

Paris Saint-Germain wamethibitisha Mshambuliaji wao wa Kimataifa wa Ufaransa, Kylian Mbappe atakuwa nje kwa karibu wiki nne baada ya kupata Majeraha Katika msuli wa mguu wake Siku ya Jumapili!.
.
– Mshambuliaji huyo wa miaka 20, Alikuwa akicheza game ya 100 katika Ligue 1, Lakini aliishia kutolewa mapema katika kipindi cha pili Klabu yake ikiibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Toulouse kwenye Dimba lao la Parc des Princes.
.
– Alikuwa mchezaji wa tatu wa PSG kulazimika kutolewa sababu ya kujeruhiwa kwenye mechi hiyo, Edinson Cavani aliondolewa katika Dakika za mwanzo za mchezo huo Nafasi yake ikichuliwa na Nahodha wa Cameroon 🇨🇲, Eric Choupo-Moting aliyekuja na kufunga Magoli Mawili Katika mechi hiyo, wakati Abdou Diallo nae alitolewa na Thiago Silva kuchukua Nafasi yake!.
#Ligue1Updates #psg
@Sokawaytz

Design a site like this with WordPress.com
Get started