
Safari ya kuelekea Qatar 2022 ndio inaanza sasa, timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars inatarajiwa kuingia kambini leo kwa ajili ya maandalizi ya maandalizi ya mchezo wa kufuzu kombe la dunia dhidi ya Burundi.
Katibu Mkuu wa TFF Wilfred Kidao amesema wameshakamilisha taratibu zote za maandalizi kuelekea mchezo huo.
:
“Burundi wote tunaifahamu ni miongoni mwa timu bora kwenye ukanda wetu na tumeona inavyocheza lakini sisi tunaamini tuna timu bora vilevile tunawachezaji bora.”
:
“Kikubwa tunahitaji support, TFF pekeyake haiwezi, waandishi wa habari pekeyao hawawezi, serikali pekeyake haiwezi. Tunahitaji nguvu za pamoja.”
:
“Sisi TFF tumeshaanza maandalizi ya mechi hii kwa muda tunashirikiana na serikali na ubalozi wetu ulioko nchini Burundi kuhakikisha mambo yote ya kiutawala na kufanya vijana wawe kwenye mazingira mazuri kwa ajili ya kucheza mpira tumeanza kuyafanya.”
:
“Wachezaji wote wanaocheza nje walioitwa tayari tumewatumia tiketi na wengine wameshaanza safari ya kuja. Wachezaji wataingia kambini August 28 (leo) lakini wachezaji wa Simba baada ya mchezo wao wa August 29 moja kwa moja wataingia kambini.”


Leo agosti 28 mabingwa wa kihistoria klabu ya yang african wanashuka dimbani kuwakabili ruvu shooting katika mchezo wao wa kwanza wa ligi kuu soka tanzania …..mchezo unaotarajiwa kupigwa majira ya saa 1:00 jioni katika uwanja wa uhuru jijini dar es salaamKuelekea mchezo wa leo dhidi ya Ruvu shooting kocha mkuu wa wanajangwani Mwinyi zahera amesema amewambia wachezaji wake kuwa mchezo wa leo utakua mgumu mno kwao huku akiwambia kazi iliyowaleta itaanza leo hivyo wataingia kwa tahadhari kubwa Sana ili kuanza vyema kuwania taji la ligi kuu Tanzania bara…….kila raheli wananchi mnapokua mnajiandaa na mchezo wenu
“Nimewaambia wachezaji wote wapya kwamba hakuna hata siku moja Yanga inacheza mechi nyepesi, mechi zote ni ngumu”-Zahera Mwinyi, kocha Yanga.

#AlexisSanchez #Inter #manchesterunited















