DAKIKA 90 ZA SIMBA KUNAKO DIMBA LA UHURU.

Na
@josejose189
:
Baada ya Yanga juzi kupotea kwa Ruvu Shooting hatimaye jana umepigwa mchezo mwingine wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (Vodacom Premier League) ambapo mnyama Simba ameanza Ligi vyema kwa kuwachapa maafande wa JKT Tanzania 3-1.
:
Dalili za Simba kushinda mchezo huo zilianza mapema mno mwanzoni wa dk ya kwanza tu ambapo mnyarwanda Meddie Kagere alifanikiwa kuzitikisa nyavu za maafande hao baada ya kazi nzuri ya Mzamiru Yassin iliyotokana na counter attacks iliyofanywa kupitia pembeni.
:
Erasto Nyoni akisimama vizuri kwenye safu ya ulinzi yeye na Tairone huku Tshabalala na Haruna Shamte wakikamilisha idadi ya walinzi ambalo walikuwa na jukumu la kumlinda Aishi.Bado hapajawa na combination kati ya Nyoni na Da Silva maana hawajawahi kucheza pamoja na kwa muda mrefu ila uimara wa Erasto as both senior and a key player ulimbeba na kumsaidia kutuliza timu na kui command ile defense line ya Simba,huku akisa hihisha baadhi ya makosa ya walinzi wa pembe(Tshabalala na Shamte) ambao walikuwa aggressive sana kutokana na mfumo.
:
Leo hii Aussems alianza na Mbrazil Fraga Gerson aliyekuwa akicheza chini kwenye nafasi ambayo mara nyingi amekuwa akicheza Mkude ambaye ni injured na hakuwa sehemu ya mchezo wa Leo.Uwepo wake ulimlazimu Mwalimu kumchezesha Mzamiru mbele yake kidogo huku Chama,Dilunga na Deo Kanda wakipewa jukumu la kui push timu na Kagere akisimama kama mshambuliaji wa kati.Hawa viungo ndio hazina kubwa ya Simba kwa sasa.Idadi ya viungo wengi inasaidia na kufanya timu ikabe ama ishambulie na kusaidia pia kuficha mapungufu kadhaa ya safu ya ushambuliaji.
:

Idadi hii iliwafanya JKT Tanzania kushindwa kuhimili pressure ya Simba kutokana na Simba kumiliki mpira kwa muda mrefu na kufika kwa urahisi kwenye eneo la adui.Hali hii iliwafanya JKT kujikiuta wakifanya makosa mengi kutoka kwenye safu ya kiungo hadi safu yao ya ulinzi na kuwafanya Simba kucheza kwa ari na confidence ya hali ya juu.Kazi ya Dilunga na Chama always ni kui drive timu.Wao huwa ni wepesi,wana kasi maamuzi na jicho la kuamua nini kifanyike,wapi na kwa muda gani.Kagere hakuwa na kazi ngumu zaidi ya kujiweka kwenye nafasi na kutafuta target maana walinzi wa JKT walikuwa wameshaingia kwenye mkasa wa woga uliosababisha wajiingize kwenye makosa na kuadhibiwa na wapinzani wao.

:
Kagere ni yule yule,tuliye muona msimu uliopita.Nadhani JKT walimchukulia poa.Ukabaji wake unaanzia kwa kina Dilunga na Chama.Pia inahitaji kuwepo kwa uwiano wa viungo kama waliokuwa nao Simba,kuzidiwa idadi ya viungo ni kukaribisha makosa kama yaliyo wakuta.Kazimoto na wenzake hawakuwa na kazi nyingine zaidi ya kuwa watumwa na kulazimika kutumia nguvu nyingi dhidi ya wapinzani wao.Ukiruhusu viungo was Simba wa dominate game,basi impact ya kupata matokeo lazima itakua kubwa pia kama kutakuwa na clinical finishing kwenye eneo la mwisho.
:
Game discipline pia ni moja ya jambo ambalo limewa gharimu JKT Tanzania,walitakiwa waingie kwa kuwaheshimu zaidi Simba kama timu kubwa na wao kukingia kama underdog.Kitendo cha wao kuingia uwanjani wakiwa wamekariri matokeo ya Simba dhidi ya Ud do Songo kilimfanya mwalimu wao aonekane kushiwa mbinu na wachezaji wake kushindwa kutumia uwezo wa ziada.Ujenzi wa Saikolojia ulikua wa muhimu mno kuelekea mechi hii.Nadhani mwalimu wao ameliona na atalifanyia kazi.Pia eneo lake la mwisho pia kuonekana kukosa utulivu chini ya Lyanga Danny ambaye alishindwa kutumia nafasi kadhaa za wazi.

Magoli mawili ya Kagere ni mwanzo mzuri japo ndio kwanza Ligi imeanza,lakini inamsaidia kuongeza ile ari ya kujituma na kujiamini mno hasa akijipigia hesabu za kuwania nafasi ya mfungaji bora.Pia ana play nafasi kubwa kama mchezaji muhimu anae tegemewa kwenye eneo la mwisho la timu ya Simba.Kuhusu magoli yake inabidi kabla hatuja laumu safu ya kiungo na ya ulinzi ya JKT ni vyema tukaanza kumsifia yeye kwanza,kwa kutumia akili kubwa wakati wa kufanya finishing. Ndivyo inavyotakiwa kwa mfungaji.
:
Kuhusu goli la Edward Songo wa JKT ni vyema na yeye tukampongeza,maana itakuwa sio jambo jema kuanza kumlaumu Aishi kama hatujasifia ile fantastic drive and shout out ambayo alifanya maamuzi akiwa mbali na semicircle .Mshambuliaji lazima uwe na akili ya ziada kama alivyofanya Songo Leo na yule Saadat Mohammed wa Ruvu Shooting jana aliye wafunga Yanga kwa kutumia akili binafsi.
:
Hadi mwisho wa game,Simba 3-1 JKT Tanzania.
:
Nadhani bado timu zinajipanga na ndio na Ligi ndio imeanza.Walimu watakuwa makini kifanyia kazi mapungufu yaliyo onekana ili kujenga vikosi bora na vyenye kutoa ushindani kwa mustakabali bora wa Ligi yetu.
:
Powered by @bikotanzania
Jose Jose @sokaplace_

Sasa Sanchez kuitumikia inter milan rasmi

DONE DEAL: Inter Milan Imethibitisha kukamilisha usajili wa Mshambuliaji wa Kimataifa wa Chile, Alexis Sanchez kutoka Manchester United kwa mkopo wa Msimu mmoja!.
.
– Alexis Sánchez buana ndio Mchezaji wa Soka Pekee kufunga hat-trick Katika LIGI KUU tatu tofauti barani Ulaya, tunazungumzia Serie A, LaLiga na pia Premier League..
.
– Lakini Alexis Sanchez mambo yamemuendea vibaya ndani ya @premierleague akiwa na Manchester United!.
✍️ 3⃣2⃣ Mechi.
✍️ Kaanza XI 3⃣8⃣% ya Mechi za Man Utd ndani ya Premier league tangu Asajiliwe!.
✍️ 3⃣ goals & 6⃣ assists
✍️ Wastani wa Goli Moja ndani ya Premier league Anafunga Baada ya kila Dakika 6⃣4⃣1⃣.
#TransfersNews #Inter #ManUtd
@Sokawaytz

Virgil van Dijk…atwaa tuzo ya mchezaji bora UEFA 2018/19

Virgil van Dijk amekuwa Mchezaji wa Kwanza wa Liverpool kutwaa tuzo ya UEFA Men’s Player of the Year, tangu Mara ya mwisho, Steven Gerrard Mwaka 2005.
#UefaChampionsLeague

Wala haihitaji kujadili wala marumbano kuhusu tuzo hii, well deserved.
.
Tukumbuke tu hii tuzo ni kwa mchezaji bora na mchezaji ni yeyote kuanzia nafasi ya kipa, beki, kiungo, na mshambuliaji
.
Ni ngumu kupata Washambuliaji wazuri wenye consistency kama ya Ronaldo na Messi ila amini kwamba ni ngumu pia kupata Beki mwenye kiwango cha Van Dijk japo kwa msimu mmoja tu, kwa upande wa beki amini kwamba uwa ngumu ata kwake kurudia kiwango kile kile ata kwa msimu mwingine tu
.
Van Dijk bana naeza mfananisha na makomando wa vita hatari sana kama “Alexander The Great” au “Cyrus the Great”, Ok next time nakuja kukwambia why namfananisha na hao makomando hatari kuwahi tokea Duniani. .
Hongera sana VIRGIL VAN DIJK

.
.
Written by : Daniel Mtani Thomson
IG: @danirito_thomson

RATIBA YA SOKA LEO +MATOKEO YA SOKA JANA

#EnglandChampionship
21:45 Cardiff City vs Fulham
:
#SpainLaLigaSantander
21:00 Sevilla vs Celta Vigo
23:00 Athletic Bilbao vs Real Sociedad
:
#ItalySerieA
21:45 Bologna vs SPAL
:
#GermanyBundesliga
21:30 Borussia Mönchengladb vs RasenBallsport Leipzig
:
#FranceLigue1
21:45 Metz vs Paris Saint-Germain
:
#AlgeriaLigue1
22:00 NC Magra vs USM Bel Abbes
22:00 US Biskra vs ASO Chlef
:
#EgyptCup
21:00 Pyramids FC vs El Hodood
:
#KenyaPremierLeague
15:00 Kariobangi Sharks vs Western Stima
15:00 Sofapaka vs Posta Rangers
:
MATOKEO YA SOKA JANA ALHAMISI.
:
#EuropaLeagueQualification
FT Qarabag FK 2 – 1 Linfield
FT Riga FC 1 – 0 FC Koebenhavn
FT AIK 1 – 4 Celtic
FT Apollon Limassol 0 – 4 PSV Eindhoven
FT BATE Borisov 2 – 0 FC Astana
FT Bnei Yehuda Tel Aviv 0 – 1 Malmoe FF
FT Molde 1 – 1 Partizan Beograd
FT PAOK Thessaloniki FC 3 – 2 Slovan Bratislava
FT Zorya Luhansk 2 – 2 RCD Espanyol
FT Spartak Moscow 1 – 2 SC Braga
FT Hapoel Beer Sheva 0 – 3 Feyenoord
FT Royal Antwerp 1 – 4 AZ Alkmaar
FT Trabzonspor 0 – 2 AEK Athens
FT F91 Dudelange 2 – 1 Ararat Armenia
FT Ferencvaros 4 – 2 Suduva
FT Rijeka 1 – 1 Gent
FT Maribor 2 – 2 Ludogorets Razgrad
FT Eintracht Frankfurt 3 – 0 Strasbourg
FT Rangers 1 – 0 Legia Warszawa
FT Wolverhampton Wande 2 – 1 Torino
FT Vitoria de Guimaraes 1 – 0 FC FCSB
:
#InternationalFriendlieswomen
FT Belgium 3 – 3 England
FT Chile 1 – 0 Costa Rica
FT USA 4 – 0 Portugal
FT Brazil 5 – 0 Argentina
:
#VodacomPrimierLeague
FT JKT 1-3 Simba SC
:
#TunisiaLigueI
FT Ben Guerdane 0 – 1 JS Kairouanaise
:
Prepared by @officialchristz
Powered by @bikoTanzania

Simba kuwakosa nyota watano leo dhidi ya jkt Tanzania

Wakati Simba ikitarajiwa kushuka uwanja wa Uhuru leo kuanza utetezi wa ubingwa wake kwa kuumana na JKT Tanzania, wachezaji watano wa timu hiyo wana hatihati ya kutocheza kutokana na sababu mbalimbali

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema nahodha John Bocco anaendelea na matibabu ya majeraha aliyopata kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam Fc

Kiungo Jonas Mkude bado anaumwa, anasumbuliwa na Malaria

Wengine ni Wilker Da Silva ambaye ni majeruhi wa muda mrefu, Shomari Kapombe na Paschal Wawa wao walipata majeraha kwenye mchezo dhidi ya UD Songo

Hata hivyo wachezaji hao jana walifika mazoezini, lakini walijifua chini ya uangalizi wa daktari wa timu

Aidha, Aussems amesema nafasi za wachezaji hao zitazibwa na wachezaji wengine walioandaliwa

Lazima timu iwe na kipa namba moja -asema aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems ametetea uamuzi wa kumuanzisha mlinda lango Aishi Manula kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya UD Songo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 na Simba kutolewa kwenye michuano hiyo

Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa Manula kukaa langoni baada ya kuwa nje kwa karibu wiki tatu akiuguza majeraha

Licha ya Beno Kakolanya kuonyesha uwezo mkubwa wakati Manula hayupo, hakupata nafasi ya kuanza mchezo huo

Aussems amesema timu lazima iwe na kipa namba moja, hivyo ulikuwa uamuzi sahihi kumuanzisha Manula kwa kuwa alikuwa amepona

“Lazima tuwe na kipa namba moja, mbili na tatu. Manula alikuwa amepona majeraha yaliyokuwa yakimsumbua hivyo alistahili kucheza,” amesema

Aussems amesisitiza kuwa walinda lango hao watacheza kulingana na utimamu wao kimwili na utayari wa mchezo

Design a site like this with WordPress.com
Get started