Kiungo wa kenya kucheza ligi kuu iraq

DEAL DONE!. Kiungo wa Kimataifa wa Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬, Allan Kateregga amekamilisha Usajili wake wa kujiunga na Klabu ya Erbil Sport Club Kama mchezaji Huru, Klabu Yake hiyo mpya inashiriki Ligi Kuu Nchini Iraq.
.

– Msimu uliopita, nyota huyo wa @ugandacranes Alikuwa akiitumikia Klabu ya Maritzburg United kwa mkopo akiisaidia kutoshuka Daraja, Alitua hapo akitokea Cape Town City zote za Afrika Kusini… Amecheza Ligi Kuu nchini Kenya katika Klabu ya AFC Leopards iliyomuuza kwenda Klabu ya KCCA FC ya nyumbani kwao Uganda πŸ‡ΊπŸ‡¬ ambapo akiwa hapo hakudumu, Msimu Mmoja TU akatimkia Huko Bondeni ambako nako wamefikia Makubaliano ya kusitisha Mkataba baina yao… Fundi Sana huyu Jamaa “Dancing Rasta”.
#TransferNewsUpdate
@Harunlugoyah

MATOKEO YA MUDA WOTE

05 Dec 1971
Tanzania 4-1 Burundi – Kirafiki

31 Oct 1981
Burundi 1-2 Tanzania- Kirafiki

02 Nov 1981
Burundi 0-1 Tanzania – Kirafiki

02 Aug 1998
Burundi 1-0 Tanzania – Kufuzu AFCON
16 Aug 1998
Tanzania 0-1 Burundi – Kufuzu AFCON

31 Jul 1999
Tanzania 0-1 Burundi – CECAFA Cup

09 Dec 2001
Tanzania 2-1 Burundi – CECAFA Cup

05 Dec 2002
Burundi 0-2 Tanzania – CECAFA Cup

28 Nov 2005
Tanzania 2-1 Burundi – CECAFA Cup

15 Dec 2007
Tanzania 0-0 Burundi – CECAFA Cup

13 Jan 2009
Tanzania 3-2 Burundi – CECAFA Cup

04 Dec 2009
Tanzania 1-0 Burundi – CECAFA Cup

04 Dec 2010
Tanzania 2-0 Burundi – CECAFA Cup

08 Jan 2011
Tanzania 1-1 Burundi – Kirafiki

28 Nov 2012
Tanzania 0-1 Burundi – CECAFA Cup

04 Dec 2013
Tanzania 1-0 Burundi – CECAFA Cup

26 Apr 2014
Tanzania 0-3 Burundi – Kirafiki

07 Sep 2014
Burundi 2-0 Tanzania – Kirafiki

28 Mar 2017
Tanzania 2-1 Burundi – Kirafiki

04 Sep 2019
Burundi 1-1 Tanzania – Kufuzu Kombe la Dunia

Via @zakazakazi

Stars kuivaa burundi.Leo kisawa sawa

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ leo kitashuka dimba la Taifa kurudiana na Burundi katika mchezo wa hatua za awali kusaka tiketi ya michuano ya kombe la dunia

Timu hizo zilicheza siku tatu zilizopita nchini Burundi na kutoka sare ya bao 1-1

Ushindi au matokeo ya suluhu ya bila kufungana kwa Tanzania, yatatosha kuihakikishia kucheza hatua ya makundi

Mashabiki wameaswa wajitokeze kwa wingi uwanja wa Taifa ili kuwaunga mkono Stars katika mchezo huo

Viingilio vya mchezo, Mzunguuko ni Tsh 2000/- na VIP ni Tsh 5000/-, lengo ni kuhakikisha mashabiki wanajaza uwanja wa Taifa

Nahodha wa Stars Mbwana Samatta amesema wamejiandaa na wana matumaini ya kupata matokeo ya ushindi kwenye mchezo huo unaotarajiwa kuanza saa kumi jioni

TIMUA MAKOCHA YAANZA EPL

TIMUA TIMUA YA MAKOCHA YAANZA EPL,WATFORD YAMTIMUA KOCHA GARCIA
.

Klabu ya Watford inayoshiriki katika ligi kuu ya England imemtimua kazi kocha wake Jarvi Garcia na kumrejesha kocha waliyemtimua kabla yake Quique Sanchez Flores.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya matokeo mabovu katika msimu mpya Wa ligi wakipata pointi 1 katika michezo minne .
#wapendasokaupdates

Serena williams atwangwa na binti wa miaka 19

✍🏻 Tunaweza kusema, “Mende Kaangusha Kabati”, Mwanadada, Bianca Andreescu akiwa na umri wa miaka 19 TU, kamtwanga mkongwe, Serena Williams kwa seti ya moja kwa Moja 6-3, 7-5 na kuibuka Bingwa wa US Open kwa Michuano yake ya kwanza kabisa kushiriki, Andreescu pia amekuwa ni Mcheza Tennis wa kwanza kabisa kutoka nchini Canada kutwaa Grand Slam… Kamshangaza Bingwa Mara 23 wa Michuano hii 🏸 Serena Williams.
.
✍🏻 Ushindani wa Bianca Andreescu katika Dimba la Arthur Ashe Stadium, Ulimfanya Serena Williams Kushindwa kuifikia Rekodi ya Mwanadada, Margaret Court kutoka nchini Australia anaeshikilia Rekodi ya Muda wote kutwaa Mara nyingi Zaidi Ubingwa wa Grand Slam (24) – Uwanja Huu wa Arthur Ashe, ndio Serena Williams alitwaa Grand Slam kwa mara ya kwanza kabisa 1999.
.
✍🏻 Serena Williams Tangu ajifungue mtoto wake, amekuwa Akipoteza fainali ovyo, hii Ni Fainali yake ya Nne atapoteza Tangu ajifungue na kipigo chake kinamfanya mpinzani wake Sasa kukamata Nafasi ya tano Katika Orodha ya Wachezaji Tennis bora inayotolewa na Chama cha Tennis cha Wanawake (WTA).
#USOPEN #Updates
@Harunlugoyah

:RATIBA YA SOKA LEO.

#InternationalFriendlies
16:00 Kenya vs Uganda
:
#EUROQualification
19:00 Georgia vs Denmark
19:00 Switzerland vs Gibraltar
19:00 Romania vs Malta
21:45 Spain vs Faroe Islands
21:45 Sweden vs Norway
16:00 Armenia vs Bosnia and Herzegovina
21:45 Finland vs Italy
21:45 Greece vs Liechtenstein
:
#WorldCupCAFQualification
16:00 Lesotho vs Ethiopia
16:00 Tanzania vs Burundi
19:00 Equatorial Guinea vs South Sudan
19:30 Sierra Leone vs Liberia
:
#NetherlandsEersteDivisie
13:15 Helmond Sport vs FC Eindhoven
15:30 Roda JC Kerkrade vsTOP Oss
17:45 Almere City FC vs FC Volendam
:
#EgyptCup
21:00 Pyramids FC vs El Zamalek
:
Prepared by @officialchristz
Powered by @bikotanzania

MATOKEO YA SOKA JANA JUMAMOSI

#EUROQualification
FT Kosovo 2 – 1 Czech Republic
FT England 4 – 0 Bulgaria
FT Lithuania 0 – 3 Ukraine
FT Serbia 2 – 4 Portugal
FT Iceland 3 – 0 Moldova
FT Turkey 1 – 0 Andorra
FT France 4 – 1 Albania
:
#WorldCupCAF Qualification
FT Botswana 0 – 0 Malawi
:
#NetherlandsEersteDivisie
FT FC Dordrecht 1 – 1 MVV Maastricht
FT Telstar 0 – 2 Cambuur
FT Go Ahead Eagles 2 – 2 Excelsior
:
#TunisiaLigueI
FT CA Bizertin 1 – 1 CS Hammam-Lif
:
#MichezoYaKirafikiTanzania
FT Pamba SC 1-1Yanga SC
FT Azam FC 4-1 Pan Africa.

#Repost from @alliancefootballclub2011

Uongozi wa Alliance Fc leo hii umetangaza rasmi kuongeza nguvu katika idara ya habari kwa kuongeza waandishi wengine watatu.

Waandishi hao ni Fabian Fanuel wapili kutoka kushoto ambaye yeye atahusika katika maswala ya mitandao ya kijamii ,Winigester Macha watatu kutoka kushoto ambaye yeye rasmi atakuwa afisa habari wa Alliance Girls Fc inayoshiriki ligikuu ya wanawake Tanzania bara na wa mwisho ni Michael Jamsoni huyu atakuwa na jukumu zito la kupiga picha matukio ya timu zetu zote.

Makamu mwenyekiti wa timu wa kwanza kushoto Stephano Nyaitati amewakaribisha waandishi hao na kuwasihi wafanye kazi kwa bidii na kwa maarifa mapya ili kuongeza ufanisi katika timu.

Waandishi hao kwapamoja wameupongeza uongozi wa timu kwakuwaamini nakuwapa nafasi hiyo na kilammoja ameahidi kuifanya kazi yake kwa ubora mkubwa na kwakujituma ili kuonesha uwezo wake kwa sehemu aliyopewa.

Jackson Luka Mwafulango

Afisa habari Alliance Fc
Hongera @winniegmacha

Design a site like this with WordPress.com
Get started