KUISHANGILIA YANGA JUMAMOSI “BUKU 3 TU”

Kiasi cha shilingi za Kitanzania elfu tatu tu kinatosha kushuhudia mpambano Wa kusaka kucheza katika ligi ya mabingwa Afrika hatua ya Makundi.

Yanga imeweka wazi Leo viingilio katika michezo huo utakaochezwa katika uwanja Wa Taifa siku ya Jumamosi huku Kiingilio cha juu likiwa ni laki moja kwa Tiketi za daraja la Royal.

#wapendasokaupdates

CEO mpya simba aongea mzuka

Siku chache tangu uongozi wa klabu ya Simba kumtambulisha bosi mpya, kitendo hicho kimelipandisha mzuka benchi la ufundi ambalo limeapa kukisuka zaidi kikosi ili kiwe na makali ya kufanya mauaji katika mechi zao zijazo za Ligi Kuu Tanzania Bara.

Wikiendi iliyopita, Simba walimtambulisha rasmi Senzo Mazingisa, raia wa Afrika Kusini, kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu (C.E.O) baada ya Crescentius Magori, kumaliza muda wake.

Moja ya vitu ambavyo Mazingisa, alivyovingumza katika utambulisho wake, ni kuifanya Simba kuwa klabu bora Afrika kulingana na makubaliano ya mkataba wao.

Kauli hiyo ya Mazingisa inaonekana kuanza kufanyiwa kazi na benchi la ufundi ambalo linataka kusuka kikosi cha maangamizi kuelekea mechi zao za Ligi Kuu Bara na michuano yoyote itakayopita mbele yao.

Katika mazoezi yaliyofanyika jana kwenye viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Salaam, inadhihirisha hilo kwa sababu ya aina ya tizi walilokuwa wanapewa wachezaji wa timu hiyo.

Licha ya uwepo wa wachezaji wachache mazoezini kutokana na wengine kuwa na majukumu ya timu zao za Taifa, Kocha Mkuu Patrick Aussems, alikuwa makini kuhakikisha kila mmoja anafanya kile anachotaka.

Wekundu wa Msimbazi hao, walikuwa wakifanya mazoezi ya aina tofauti, zaidi ikiwa yale ya kuongeza pumzi na kasi ya kukimbia wanapokuwa uwanjani.

Wacheza walikuwa wanakimbia kwa zamu huku wamefunga vifaa vya kuwafanya kuwa na kazi pamoja na pumzi, kocha akiwa amewasimamia, wakipokezana.

Kocha Patrick Aussems, aliweka bayana kuwa lengo kwa sasa baada ya kupitia kipindi kigumu cha kuondolewa katika michuano ya kimataifa, anataka kuwadhihirishia wapenzi wa soka kuwa kikosi chao ni bora.

Aussems alisema kutokana na maandalizi wanayofanya, ubora wao utaanza kuonekana katika mechi dhidi ya Mtibwa Sugar inayotarajia kuchezwa Ijumaa hii kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Alisema mechi yao imerudishwa nyuma, tofauti na simu waliyotakiwa kucheza, lakini hilo halimpi presha kwani msimu huu wamejipanga na kitendo cha ratiba hiyo kubadilika hakijaathiri chochote.

“Tumeendelea na mazoezi kwa wachezaji ambao hawapo katika timu za Taifa, nafurahi kikosi kipo vizuri tumejipanga kukabiliana na Mtibwa Sugar, tena imerudishwa tunacheza Ijumaa, hiyo haina tatizo.

“Haya mazoezi ya mbio tuliyoyafanya leo(jana), ni kuwaweka wachezaji vizuri, mengine yamepita na sasa tunaangalia mbele kuonyesha kila mtu kwamba sisi ni timu bora na hilo litaanzia siku ya mechi dhidi ya Mtibwa Sugar,” alisema Aussems.

BINGWA

TAARIFA RASMI KUTOKA FAMILIA YA MZEE RUPIA.

:

Ni kweli ndugu yetu Christopher Rupia amefariki dunia siku ya jumapili. Marehemu alianguka uwanjani wakati anaangalia mechi kati ya Taifa Stars na Burundi.
Marehemu Rupia alikua mfanyakazi mstaafu wa NSSF alikuwa anaishi Mongolandege Shule kinyerezi.

Mipango ya mazishi inafanyika hapo nyumbani kwake na anatarajiwa kuzikwa kesho Jumatano hapa hapa DSM.
:
Kwa wale wapenda soka watakao weza kwenda kumpumzisha mzalendo mwezetu wa @taifastars_ wanaweza kupiga Simu katika No hii ya mtoto wake
Kwa Namba hizi +255715121316 Mika Rupia kijana wa kiume wa Marehemu

@sokaplace__ tunatoa pole kwa wafiwa wote waliopatwa na Msiba huu.

@tanfootball @sokaonline_ @matchday_tz @giftmacha_official

Hazard Kaitumikia Madrid kwa Mara ya Kwanza Laliga!. :

Eden Hazard amekuwa kwenye mazoezi ya Klabu yake wiki hii na anatarajia kucheza mechi yake ya kwanza kwa Real Madrid dhidi ya Levante Katika Muendelezo wa Laliga wikendi ijayo kwa mujibu wa ripoti ya Jarida la AS huko Hispania.
:
– Mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Ubelgiji, bado hajafanikiwa kucheza mechi ya Kimashindano ndani ya kikosi chake cha Madrid tangu kuhamia klabuni hapo kwa euro milioni 100 (pauni milioni 88) Akitokea Chelsea baada ya kupata jeraha la paja.
:

– Madrid watakutana na Levante kwenye game ya La Liga Jumamosi, kabla ya kuikabili Paris Saint-Germain kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wiki ijayo huko Paris, Ufaransa… Madrid ipo nafasi ya tano na point Tano Baada ya Kucheza tatu za Ligi, Point Nne nyuma ya Wapinzani wao wa Jiji, Atletico Madrid walio Vinara, Huku Point Moja Mbele ya Mahasimu wao wa Ligi, FC Barcelona..
#LaLiga #LaligaUpdates #RealMadrid
@Harunlugoyah

Sancho kuanza mbele ya Rashford

– Jadon Sancho ataanza badala ya Marcus Rashford Katika Kikosi cha England kitacho cheza dhidi ya Kosovo leo Jumanne usiku, inaripoti Daily Mail… England iliyo na pointi Tisa Katika Kundi A itavaana na Kosovo walio Nafasi ya Pili kwa Pointi Nane Katika harakati zao za kuwania Kufuzu kwa fainali za EURO.
.
– Kocha Mkuu wa The Three Lions, Gareth Southgate atamchagua nyota wa Borussia Dortmund mbele ya Rashford wa Manchester United, ambaye alifanikiwa kusababisha Penati katika ushindi wa Jumamosi dhidi ya Bulgaria… Penati ambayo ilipigwa na Harry Kane aliyefunga hat trick game hiyo.
.
– Southgate atataja lineups yake isiyobadilika kwa kiasi kikubwa, lakini anafikiria kumuanzisha Trent Alexander-Arnold wa Liverpool na Ben Chilwell wa Leicester City badala ya Kieran Trippier wa Atletico Madrid na Danny Rose wa Tottenham..
#England #EURO2020 #Kosovo
@Harunlugoyah

ZAHERA: BADO KILO NNE FALCAO AANZE MAVITU

Kocha mkuu wa timu ya Yanga, Mwinyi Zahera amesema mshambuliaji wake David Molinga ‘Falcao’ bado kupungua kilo nne ili kurejesha makali yake ya kufumania nyavu.

Zahera amesema Falcao alikuwa na kilo 92 alipojiunga na Yanga lakini kwa sasa ana kilo 78 huku akibakisha nne ili kuwa bora na kurejesha furaha kwa Wana Yanga.

Mshambuliaji huyo amesajiliwa kuchukua nafasi Mkongomani mwenzie Heritier Makambo ambaye amejiunga na Horoya ya Guinea kabla ya kuanza msimu huu.

Zahera amesema ana matumaini makubwa na Falcao ya kufanya vizuri na kama atapungua kilo nne ataongeza kasi na kufunga mabao mengi. “Falcao alikuwa na kilo 92, tunafanya jitihada za kuhakikisha anapungua na zimebaki kilo nne zikipungua hizo atakuwa bora na atafunga kila siku,” alisema Zahera.

Falcao jana alifunga bao lake la kwanza katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Pamba FC kwenye uwanja wa CCM Kirumba ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.

#wapendasokaupdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started