Ukata ndani ya GOR MAHIA. Yaomba msaada serikarini

Ukata mkubwa ndani ya GOR MAHIA

Katika hali inayoashiria ni kuyumba kiuchumi, klabu ya Gor mahia mabigwa Γ—18 wa Ligi kuu ya Kenya, imeandika barua kupitia shirikisho la soka Kenya kwenda kwenye Wizara ya michezo Kenya ikiomba msaada wa kifedha.

Wizara ya michezo Kenya imesema kwa sasa haina fedha wala bajeti ya kusafirisha timu ya Gor Mahia, hivyo safari ya mchezo wa kwanza Ligi ya Mabingwa wa Caf dhidi ya USM Algers Jumapili sasa iko kwenye hatihati ya kushindikana.

Gor Mahia imefanya harambee Jumanne ya ukusanyaji fedha katika ukumbi wa Nairobi Charter kwa ajili ya kupunguza gharama kwa timu na kulipa madeni ya wachezaji.

Kwa ujumla hali ya kiuchumi si njema ndani ya Gor Mahia tangu kuondoka kwa waliokuwa wadhamini wakuu SportPesa, kujiondoa kutokana na kutofikia makubaliano na Mamlaka ya mapato Kenya (KRA).

Samatta kukaa nje ya dimba kwa muda

#Repost from @samagoal77

Mazungumzo yangu na daktari baada ya vipimo
Daktari na karatasi ya kipimo mkononi.

Daktari: Ndugu Samatta

Mimi: Ndio Daktari

Daktari: Majibu yako yanaonesha…anachukua miwani anavaa anaguna mmmh… Mimi: Mapigo ya moyo yanaanza kupanda, tumbo linavurugika, haja kubwa inagonga nguo ya ndani.

Daktari: Una bahati sana eneo ambalo lilikuwa karibu kuumia lingekufanya ukae nje sio chini ya miez 6 lakini halijapata jeraha zaidi ya mtikisiko kwa hiyo siku chache za mapumziko zitakufanya uendelee kucheza.

Mimi: Huuuuuuu (nashusha pumzi) sikumbuki niliibana kwa sekunde ngapi.

Daktari: Kwa hiyo unaweza kuendelea na matibabu na mazoezi.

Mimi: Asante.

So majibu-maumivu sio mkubwa sana na baada ya siku kadhaa nitakuwa tena viwanjani kupambania kombeπŸ˜‚ asanteni wote mliojali na wote mlionitumia meseji za poleπŸ™

HAINA KUFELI.

MATOKEO YA SOKA JANA +RATIBA YA SOKA LEO. :

#EUROQualification
FT England 5 – 3 Kosovo
FT Montenegro 0 – 3 Czech Republic
FT Lithuania 1 – 5 Portugal
FT Luxembourg 1 – 3 Serbia
FT Albania 4 – 2 Iceland
FT France 3 – 0 Andorra
FT Moldova 0 – 4 Turkey
:
#WorldCupAFCQualification
FT Guam 1 – 4 Philippines
FT Maldives 0 – 5 China
FT Chinese Taipei 0 – 2 Nepal
FT Kuwait 0 – 3 Australia
FT Cambodia 0 – 1 Bahrain
FT Hong Kong 0 – 2 Iran
FT Singapore 2 – 1 Palestine
FT Yemen 2 – 2 Saudi Arabia
FT Afghanistan 1 – 0 Bangladesh
FT Qatar 0 – 0 India
FT Mongolia 0 – 1 Tajikistan
FT Myanmar 0 – 2 Japan
FT Indonesia 0 – 3 Thailand
FT Malaysia 1 – 2 UAE
FT Sri Lanka 0 – 1 North Korea
FT Turkmenistan 0 – 2 South Korea
:
#WorldCupCAFQualification
FT Malawi 1 – 0 Botswana
FT Eswatini 0 – 0 Djibouti
FT Zimbabwe 3 – 1 Somalia
FT Mozambique 2 – 0 Mauritius
FT Angola 2 – 1 Gambia
FT Rwanda 7 – 0 Seychelles
FT Togo 2 – 0 Comoros
FT Guinea-Bissau 2 – 1 Sao Tome and Principe
FT Namibia 2 – 0 Eritrea
FT Sudan 0 – 0 Chad
:
@sokaplace__
#InternationalFriendlies
FT Oman 1 – 0 Lebanon
FT Jordan 2 – 4 Paraguay
FT Tunisia 1 – 2 Ivory Coast
FT Ukraine 2 – 2 Nigeria
FT Ireland 3 – 1 Bulgaria
FT Morocco 1 – 0 Niger
FT Ecuador 3 – 0 Bolivia
FT USA 1 – 1 Uruguay
FT Colombia 0 – 0 Venezuela
FT Honduras 2 – 1 Chile
:
#TanzaniaFriendlyMatch
FT MbeyaCity 2-0 Njombe Mji
FT TotoAfrika 0-3 Yanga SC
:
RATIBA YA SOKA LEO.
:
#AlgeriaLigue1
16:00 AS Ain Mlila vs MC Oran

Prepared by @officialchristz
Powered by @bikotanzania

Kokosi cha zesco kinachokuja kuivaa yanga

Kikosi cha Zesco Utd kinacho tarajia kusafiari kuja TANZANIA kwaajili ya kuja kumenyana na Yanga Africans Sports Club katika hatua ya pili ya Klabu Bingwa Afrika.

JACOB gk
DIEUNDONE gk
SIMON
DAVID
MARCEL
CLEMENT
WINSTON
WAPE
ENOCK
MWILA
FACKSON
ANTONY
KONDWAN
JOHN
KOSUKE
JESSE
QUADRI
THABAN
UMARU.

@yangasc
@zesco_united_official

ZESCO United. Kuwasili kesho tanzania

✍🏻 Msafara wa Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Zambia πŸ‡ΏπŸ‡², Klabu ya ZESCO United unatarajia kuwasili Nchini Tanzania Siku ya Kesho Jumatano, September 11, 2019 ukitokea huko Kwao Zambia… Jumla ya Wachezaji 19, Kocha Mkuu George Lwandamina na Wasaidizi wake utapaa kesho Kutokea Uwanja wa Ndege Kimataifa wa Simon Mwansa Kapwepwe Mjini Ndola.
.
✍🏻 ZESCO United inakuja Nchini Tanzania kwa Ajili ya Mchezo wa Raundi ya Kwanza kabisa wa Klabu Bingwa Afrika (CAF Champions League) dhidi ya Wawakilishi wa Tanzania Katika Michuano hiyo, Young Africans SC πŸ‡ΉπŸ‡Ώ, Game itapigwa Siku ya Jumamosi September 14, ndani ya Uwanja wa Taifa.
.

✍🏻 Washambuliaji wao hatari, Jackson Werre Kutoka Nchini Kenya alipata majeraha lakini yupo Kikosini, Umaru Kasumba Kutoka nchini Uganda, John Ching’andu, Kiungo Mshambuliaji wao fundi, Enock Sabumukama Kutokea Nchini Burundi, Thaban Kamusoko Kutoka nchini Zimbabwe, Kosuke Nakamachi Kiungo wa Kimataifa wa Japan, Beki wao Mkongwe, Clement Mwape na Mlinda lango wao, Jacob Banda… Hao woote ni Sehemu ya Kikosi kinachosafiri kuelekea Tanzania.
#CAFCL #TotalCAFCL
⚑ @harunlugoyah ⚑

TFF YAWAPONGEZA WATANZANIA KWA KUJITOKEZA UWANJANI

Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limewapongeza Watanzania kwa kujitokeza kwa wingi katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia dhidi ya Burundi juzi Jumapili.

Katika mchezo huo ambao Stars ilishinda kwa mikwaju ya penati 3-0 baada ya sare 1-1 ambapo mashabiki walijitokeza kwa wingi na kuujaza uwanja wa Taifa.

Katibu mkuu wa TFF, Wilfred Kidao amesema anawapongeza Waandishi wa Habari za Michezo, Kamati ndogo ya hamasa ambapo ilisababisha mashabiki wengi kujitokeza na kupelekea timu kupata ushindi.

Kidao ameongeza kuwa hamasa hiyo inatakiwa kuendelea katika mechi zijazo ambapo sasa bado siku chache kabla ya kukutana na Sudan katika michuano ya CHAN ambapo Tanzania itaanzia nyumbani. “Waandishi mmefanya kazi kubwa sana katika mchezo wa kwanza kule Bujumbura mlihamasiha watu ambao walijitokeza kwa wingi sana na juzi uwanja pia mliujaza, kwahiyo tunataka kuendelea tulipoishia katika mchezo ulio mbele yetu dhidi ya Sudan,” alisema Kidao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taifa Stars Supporters, Kaligo Godson Kaligo amesema ushirikiano ukiopo baina ya TFF hii chini ya Rais, Wallace Karia ni mkubwa ndio maana mafanikio ni makubwa.

@tanfootball
#wapendasokaupdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started