
– Arsenal wapata ahueni kwa kuongezeka kwa Walinzi wao Wawili, Kieran Tierney na Hector Bellerin kwenye kikosi chao kinachojiandaa Kuwa tayari kucheza tena Ligi Kuu ya Uingereza baada ya mapumziko ya kimataifa kumalizika.
.
– Wawili hao wameonyeshwa wakiwa katika mazoezi na kikosi cha timu ya kwanza kwenye uwanja wa mazoezi wa Arsenal huko Colney London, Nyota hao wameonekana wakiwa kwenye njia ya kurudi kutoka katika majeraha yao.
.
– Kurejea kwao inamaanisha kwamba wanatarajiwa kuwapa changamoto Ainsley Maitland-Niles na Sead Kolasinac katika ushindani kwenye kikosi cha timu ya kwanza.
.
– Tierney Mwenye umri wa miaka 22, alifika London akiwa na jeraha la goti na pia anapona kutokana na upasuaji mara mbili wa hernia aliyefanywa majira ya joto, Nyota huyo wa Kimataifa wa Scotland hajacheza tangu Mei… Wakati Bellerin Alikuwa Ni Majeruhi wa muda mrefu, Hajacheza Tena Tangu mwezi January alipopata Majeraha Katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Chelsea..
#Arsenal #PremierLeague #PLUpdates
⚽ @Harunlugoyah
















