
Mwambie acha, acha kabisa. Haikuwa kazi rahisi kuuwasha, acha uendelee kuteketeza vilivyosalia tuzoe majivu. Nakukumbusha tu, Afrika nzima inautamani moto wetu.
Hakuna anayetamani kukanyaga nchi hii akiwa na lengo la kupata ushindi. Wanaujua moto wetu Watanzania linapokuja suala la HAMASA waulize Waburundi watakuambia walichoshuhudia kwenye majukwaa ya uwanja wa Taifa, ulikuwa moto mkubwa. Wale ndio sisi Watanzania sasa.
Sasa tunarejea CHAN mnakumbuka tuliishia wapi?, ni pale tulipowawashia moto Wakenya kwenye majukwaa ya uwanja wa Taifa kisha tukaenda kuwawashia tena Moi Kasarani. Tunauzimaje dhidi ya Sudan?, hapana, hawa pia wanastahili moto ndani na nje.
Tunaanza nao hapa Jumapili hii Septemba 22, mshtue Mzalendo mwenzako, mwambie leo tunaanza kukusanya ‘kuni’ kwa ajili ya kuwawashia moto Sudan. Tukaujaze uwanja, tushangilie.
Moto ni ule ule….. @tanfootball @taifastars_
#wapendasokaupdates
#TunakanyagaMpakaCHAN🇹🇿


















