
SHIKAMOO KIFO,TANGULIA JEBA… Na Octa ayubu Jr…. Ibrahim rajabu “Jeba” Huenda wengi wamelisikia hili jina baada ya mishipa ya damu ya Jeba ilipokata ushirikiano na moyo wake na umauti ukatengeneza urafiki na mwili wake.
Nilitamani nikutane na Jeba nipige nae story kwa kifupi afurahi labda ningepata hata bahati ya kushuhudia tabasamu lake,anyway nahisi bado isingewezekana kutokana na userious aliokuwa nao.
Nenda Jeba,Wachache tutakukumbuka ila kariakoo utasahaurika baada ya masaa 72 tu.Utazungumziwa sana kwa kipi ulichokifanya? Ungepita kariakoo hata kusalimia miezi mitatu tungekukumbuka sana.
Nenda Jeba,mwambie Mh Joel bendera Tanzania imeshiriki Afcon ila imeambulia magoli mawili tu bila point yoyote.Mwambie kocha aliyeipeleka Misri alivorudi tu alikutana na mabegi mlangoni kwa amri ya waziri.
Mwambie Patrick mafisango,Jezi yake imemaliza mafao ya kustafishwa na sasa inatumika tu.Mwambie Simba imecheza robo fainali na msimu huu imesajili wabrazil kwa ajili ya ligi kuu maana klabu bingwa hawapo tena.
Usiishie hapo kama mtakutana na Ismail mrisho mwambie Tff yetu ilishaisahau mpaka familia yake.Mwambie Abdul suleiman anaelekea kupotea na mbao ishamsahau,hii ndio bongo.
Mwambie Godfrey Boni (Ndanje )Yanga yake ipo klabu bingwa japo hawana ubingwa wowote.mwambie viongozi wake wameshasahau hadi tarehe aliyoondoka katika hii sayari wako bize na michango ya klabu.
Nakumbuka kuna kipande cha wimbo nilimsika Ngwea akisema akifa pengo lake halina spea.Basi mwambie kweli tumekosa spea na tumeshindwa kumtengeneza ngwea mwingine.
Tangulia Jeba,Zanzibar watakukumbuka mno,Nani ataandika lile bango la “Nani kama Jeba?” Kwenye michuano ya mapinduzi? Daah ! Nimeamini chanda chema hakidumu.
Nitajitahidi nikutane na Thobias kifaru aniambie wana mpango gani kama klabu juu ya kuifariji familia ya jeba na jamii ya wazanzibar.Maana mtibwa ndio iliyomtambulisha jeba kwenye macho ya watanzania.
Mungu amlaze mahala pema fundi halisi wa soka Ibrahim Rajabu “JEBA”Niliwahi kuandika na naludia “Kariakoo ilitufanya tukamsahau Jeba”
#SokaPlaceTanzania