Rayon Sports yatangaza kocha mpya

– Mabingwa wa Ligi Kuu Nchini Rwanda 🇷🇼, Klabu ya Rayon Sports Imethibitisha kumtamgaza, Javier Martinez Espinoza Raia wa Mexico Kuwa Kocha wao Mkuu Mpya akichukua Mikoba ya Roberto Oliviera Concalves Raia wa Brazil aliyeachana na Klabu hiyo kwa Makubaliano Binafsi Mwezi Uliopita.

– Espinoza Amesaini Mkataba wa Mwaka Mmoja kuiongoza Rayon Sports Jana Katika uwanja wa Ngoma ambako Klabu imepiga kambi kujiandaa na game ya Ngao ya Jamii dhidi ya Mabingwa wa Peace Cup, AS Kigali FC Siku ya Oktoba Mosi… Jukumu lake la kwanza kabisa Ni Kutetea Ubingwa wao wa Ligi Kuu ambapo wataanza kampeni yao Oktoba 05 dhidi ya Gasogi United.

– Roberto Oliviera Concalves ameondoka akiifanikisha Klabu hiyo Kuwa Mabingwa wa Ligi Kuu na Kufika hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika… Mbadala wake, Javier Martinez Espinoza yeye Katoka kutimuliwa Katika Klabu ya Vipers FC ya Uganda akidumu kwa Miezi Mitano TU Katika Mkataba wake wa Miaka Miwili!..
#TransfersNews #RayonSports
@Harunlugoyah

Inter Milan ndani ya Serie A Msimu Huu..rep9do mpya

✍️ Inter Milan ndani ta Serie A Msimu Huu: 🔵 4 Mechi.
⚫️ 4 Ushindi.
🔵 9 Magoli ya Kufunga.
⚫️ 1 Goli la Kufunga.

✍️ Inter chini ya Kocha wao Mkuu, Antonio Conte baada ya Ushindi Katika Derby ya Jana dhidi ya AC Milan Wameendelea kushika Usukani wa Ligi…
….
✍️ – Inter Milan Sasa hawajapoteza Mechi Saba za Milan Derby ndani ya Serie A (W4, D3), Kwa Mara ya Kwanza kabisa tangu March 1999..
#MilanDerby #acmilan #Inter #SerieA
@Harunlugoyah

FC Barcelona waanza Msimu ovyo.point 7 mpaka sasa

1st: Granada 10pts
2nd: Sevilla 10pts
3rd: Atlético Madrid 10pts
4th: Villarreal 8pts
5th: Real Madrid 8pts
6th: Athletic Bilbao 8pts
7th: Barcelona 7pts
:
7 – Kwa Pointi Saba Katika mechi Tano, FC Barcelona wameanza Msimu ovyo mno kwa kukusanya pointi chache Katika historia yao Katika LaLiga kwa Mara ya kwanza kabisa Tangu Msimu wa 1994/95 pia pointi Saba..
#Laliga #FCBarcelona
@Harunlugoyah

West ham…kuwakaribisha manchester united…nani.kuibuka bingwa

Leo majira ya saa 10:00 jioni kutakuwa na mchezo baina ya West Ham United na Manchester United, mchezo utakaopiogwa katika dimba la London.

Man United wamefunga jumla ya magoli 94 kwenye EPL dhidi ya West Ham, mabao mengi zaidi kuliko timu yoyote.

Kocha wa West Ham, Manuel Pellegrini ameshinda mechi za Ligi Kuu dhidi ya makocha watatu tofauti wa Manchester United (David Moyes, Louis van Gaal na Jose Mourinho).

Akishinda leo Anaweza kuwa kocha wa kwanza kuwahi kuwafunga makocha wanne tofauti wa Man United.

Mpaka sasa kwenye EPL
Man United Form: ✅⛔❌⛔✅=pointi 8
West Ham Form: ❌⛔✅✅⛔=pointi 8

Taifa stars kuivaa.sudan CHAN Leo

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ leo Jumapili saa moja jioni kitashuka dimba la Taifa kuikabili Sudan kwenye mchezo wa kwanza wa kusaka nafasi ya kucheza fainali za michuano ya CHAN inayohusishwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani

Fainali za michuano hiyo zitafanyika mwakani huko Cameroon

Kama Stars itavuka kizingiti cha Sudan basi itajihakikishia kushiriki fainali hizo kwa mara ya pili katika historia yake

Mara ya kwanza Stars kushiriki ilikuwa mwaka 2006 wakati huo ikinolewa na Maximo

Hivyo mchezo wa leo ni muhimu Tanzania kupata ushindi ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kukata tiketi

Mchezo wa marudiano utapigwa nchini Uganda Oktoba 18

Sudan ambayo itakuwa mwenyeji wa mchezo huo, imeuhamishia Uganda kutokana na kukosekana kwa usalama nchini mwao

Mashabiki wameaswa kujitokeza kwa wingi kuiunga mkono Stars ili iweze kupata matokeo

Viingilio vya mchezo huo, Mzunguuko ni Tsh 2,000/- na VIP ni Tsh 5,000/-

RATIBA YA SOKA LEO.

#AfricanNationsChampionshipQualification
19:00 Tanzania Vs Sudan
14:30 Madagascar vs Namibia
16:00 Ethiopia vs Rwanda
16:00 Zimbabwe vs Lesotho
16:30 Eswatini vs Zambia
18:00 Central African Republic vs DR Congo
18:00 Equatorial Guinea vs Congo
18:00 Ghana vs Burkina Faso
18:00 Niger vs Ivory Coast
19:00 Togo vs Nigeria
:
#EnglandPremierLeague
16:00 Crystal Palace vs Wolverhampton Wande
16:00 West Ham United vs Manchester United
18:30 Arsenal vs Aston Villa
18:30 Chelsea vs Liverpool
:
#SpainLaLigaSantander
13:00 Getafe vs Mallorca
15:00 RCD Espanyol vs Real Sociedad
17:00 Valencia vs Leganes
19:30 Athletic Bilbao vs Deportivo Alaves
22:00 Sevilla vs Real Madrid Madrid
:
#ItalySerieA
13:30 Sassuolo vs SPAL
16:00 Bologna vs Roma
16:00 Sampdoria vs Torino
16:00 Lecce vsNapoli
19:00 Atalanta vs Fiorentina
21:45 Lazio vs Parma
:
#GermanyBundesliga
16:30 Borussia Mönchengladb vs Fortuna Düsseldorf
21:00 Eintracht Frankfurt vs Borussia Dortmund
:
#FranceLigue 1
14:00 Rennes vs Lille
16:00 Angers vs Saint-Etienne
20:00 Lyon vs Paris Saint-Germain
:
#NetherlandsEredivisie
15:15 SC Heerenveen vs FC Utrecht
17:30 FC Emmen vs Feyenoord
19:45 ADO Den Haag vs AZ Alkmaar
19:45 PSV Eindhoven vs Ajax Amsterdam
:
#EgyptPremierLeague
14:00 Aswan FC vs Misr El-Maqasa
16:30 El Entag El Harby vs FC Masr
16:30 Wadi Degla FC vs Tanta
19:00 Al Masry vs El Hodood
:
#KenyaPremierLeague
14:00 Posta Rangers vs Western Stima
15:00 Kakamega vs Kariobangi Sharks
15:00 SoNy Sugar vs Bandari
15:00 Sofapaka vs Chemelil Sugar
15:00 Zoo FC vs Tusker FC
16:15 Gor Mahia vs KCB
:
#MoroccoBotolaPro
18:00 Raja Beni Mellal vs MAT Tetouan
20:00 OCK Khouribga vs Hassania Agadir
22:00 Ittihad Tanger vs Difaa El Jadida
:
#SouthAfricaPremierLeague
16:00 Baroka FC vs Highlands Park FC
16:00 Cape Town City FC vs Lamontville Golden Arr
:
#BelgiumFirstDivisionA
15:30 Standard Liege vs Eupen
19:00 Club Brugge vs Anderlecht
21:00 Zulte Waregem vs Gent
:
#TanzaniaFDL
16:00 Sahare All Star vs Green Worriors
:
Imeandaliwa na @officialchristz wa @sokaplace_

Design a site like this with WordPress.com
Get started