Kocha Mkuu wa klabu ya Mbeya City FC, Juma Mwambusi amefunguka

✍ Kocha Mkuu wa klabu ya Mbeya City FC, Juma Mwambusi amefunguka na kuweka wazi Kuwa timu yake Bado haipo vizurii Kipindi hiki, Mwambusi analaumu Zaidi Mabeki wake Kuwa Wazembe kwa Kushindwa kujilinda vizuri na kusababisha Wapinzani wao kupata Magoli Kirahisi
:
✍ Akiongea na @sokaplace__ Baada ya game ya Jana wakitoka Sare ya 2-2 dhidi ya Lipuli FC Uwanja wa Samora mkoani Iringa, Kocha huyo amesema wameona makosa yanayojirudia, wao Kama Makocha wanatakiwa kuyafanyia kazi makosa hayo kutojirudia Tena Katika Safari yao inayokuja
:
✍ Katika mechi ya Jana vs Lipuli, Mbeya City ilikuwa inafungwa na kuanza kazi ya kusawazisha Goli na Hilo kwao lilifanikiwa na kuweka kupata pointi Moja ambayo Kocha wao amesema sio mbaya kwa Ugenini kupata Matokeo hayo… Kwa ujumla Msimu Huu, Wababe hao wa Jiji la Mbeya hawajaanza vema Msimu, Mechi tatu wamekusanya pointi tatu, yaani Game zoote wametoka Sare
:
Katika Matokeo hayo, Mwambusi amesema aliichukua Mbeya City ili kuitengeneza na kuifanya timu iwe ya Ushindani, na Mpaka Sasa mwanga umeanza kuonekana na yeye Hana wasiwasi na kuja kwa Mafanikio klabuni.
:
✍🏻 @harunlugoyah #TPLUpdates #sokaplaceupdates

RONALDO akwama.kufunga frekic

RONALDOπŸ™†β€β™‚πŸ™†β€β™‚ Cristiano Ronaldo tangu ajiunge na vibibi kizee vya Turin hajafanikiwa kufunga faulo(freekick) yoyote katika faulo 24 alizopiga akiwa na Juventus.

Idadi hiyo ikiwa ni katika mashindano yote ya Seria A na ligi ya mabingwa Ulaya(UCL). Upande mwingine Paulo Dyabala tangu msimu wa 2015/16 Serie A amefanikiwa kushinda faulo 8 tu hadi sasa!.Pjanic amefanikiwa kufunga faulo 6 na Bernadeschi akishinda faulo moja tu!. Je Ronaldo awapishe wengine wajaribu au aendelee kupiga tuu hadi afanikiwe??😁

Tanzania U20 kukutana na Uganda U20 robo fainal CECAFA

CONFIRMED!. Timu ya taifa ya vijana ya Tanzania Chini ya Umri wa Miaka 20, itavaana na Wenyeji, Uganda U20 Katika hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya CECAFA U20 inayoendelea Nchini huko Uganda.
….
– Tanzania imefanikiwa kumaliza kinara wa Kundi B wakifungana kila kitu na Kenya….kilichowatofautisha Ni Kadi za Njano, vijana wa Tanzania wakionekana kuwa na Nidhamu Zaidi kuliko Kenya walio na Kadi Zaidi… Hivyo Sasa Jumpili jioni ndio Mtanange huu mkali kabisa utapigwa… Zanzibar waliokamata nafasi ya tatu katika Kundi B wao watakuwa na kibarua Cha kuwakabili Vijana wa Eritrea Siku hiyo hiyo!..

– Nusu fainali nyingine, Kenya uso kwa uso dhidi ya Burundi na Sudan wao ni Vita na ndugu zao Sudan Kusini… Game hizi Mbili kupigwa Mapemaa Mchana wa Jumapili..
#CECAFAU20ChallengeCupUganda2019
@Harunlugoyah

Barcelona wapigwa faini ya €300 usajili wa antonie Grezmman

– Barcelona wamepigwa faini ya €300 tu na Shirikisho la Soka la Uhispania (RFEF) kwa hatua zao katika kukamilisha Uhamisho wa Antoine Griezman kutoka Atletico Madrid…Atletico wanadai kwamba Barcelona ilifikia makubaliano ya kusajili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa wakati kifungu chake cha Uhamisho kilipokuwa ni €200 milioni (Β£178m / $221m) Katika Mwezi wa Machi.

– Griezmann Alikamilisha Uhamisho wake wa €120m (Β£107m / $134m) kwenda Camp Nou mnamo Julai 12, na kifungu chake cha ununuzi kilipungua mwanzoni mwa mwezi huo huo… Atletico wakidai Ni janja janja ilitumika kwa BarΓ§a na Griezmann walikubaliana wangoje Muda uende ili dau lipungue.

– Lakini shirikisho hilo limesema kuwa Barca imevunja tu sheria zake kwa kufanya Mazungumzo na Griezmann bila idhini ya Atletico… Wakati Atletico ikiamini kifungu cha mchezaji huyo cha kununuliwa kilipaswa kuwa euro 200m, Shirikisho limejibu sababu hiyo haina mashiko, Na Sasa BarΓ§a imepigwa faini na RFEF leo Alhamisi ya kuzungumza na mchezaji Bila idhini ya Klabu yake, hivyo klabu sasa inatakiwa kulipa faini ya €300 kwa kukiuka sheria… Hiyo Ni Pesa ya Chai hata Shabiki anaweza kujitolea na kulipa, takribani Laki Saba na Elfu 50 za Kibongo bongo 😱..
#fcbarcelona #LaligaUpdates #Laliga
@Harunlugoyah

KAMATA RATIBA YA SOKA LEO.

#SpainLaLigaSantander
22:00 Villarreal vs Real Betis
:
#GermanyBundesliga
21:30 FC Union Berlin vs Eintracht Frankfurt
:
#AfricaChampionsLeague
16:00 Kampala CCA vs Petro de Luanda 20:00 Mamelodi Sundowns FC vs Cote d’Or
21:00 Esperance vs Elect-Sport
:
#AfricaConfederationsCup
17:30 Motema Pembe vs Al Khartoum Club
20:00 Bidvest Wits vs Young Buffaloes FC
:
#EgyptPremierLeague
18:30 FC Masr vs Aswan FC
:
#MoroccoBotolaPro
20:00 Difaa El Jadida vs MCO Oujda
:
#SouthAfricaPremierLeague
21:00 Maritzburg United vs Chippa United FC
:
#TanzaniaFDLFixture
16:00 Stand United Vs Green Worriors
16:00 Iringa United vs Maji Maji
:
Imeandaliwa na @officialchristz wa @sokaplace__

MATOKEO YA SOKA JANA

#VodacomPrimierLeague
FT Lipuli Fc 2-2 Mbeya City
FT Kagera Sugar 0-3 Simba Sc
:
#SpainLaLigaSantander
FT Eibar 3 – 2 Sevilla
FT Celta Vigo 1 – 1 RCD Espanyol
FT Real Sociedad 3 – 0 Deportivo Alaves
:
#ItalySerieA
FT Torino 2 – 1 Milan
:
#NetherlandsEredivisie
FT Feyenoord 0 – 3 AZ Alkmaar
:
#BelgiumBekerVanBelgie
FT Royal Antwerp 4 – 2 Lokeren
FT Standard Liege 2 – 1 Lommel
:
#EgyptPremierLeague
FT El Hodood 2 – 2 Wadi Degla FC
FT ENPPI 1 – 1 El Geish
:

Miamba ya Soka nchini Argentina. Kutafuta saint ua Zlatan Ibrahimovic

Miamba ya Soka nchini Argentina, Klabu ya Boca Juniors wametoa ofa yao ya kutaka kumsajili Mshambuliaji hatari wa Kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic, kutoka Klabu ya LA Galaxy ya Ligi Kuu Nchini Marekani!.

– Zlatan mwenye umri wa miaka 37, ametoka kuweka Rekodi ya Kuwa mchezaji Pekee Katika historia ya Klabu ya LA Galaxy kufunga Magoli 25+ kwa Msimu mmoja.. Mpaka Sasa Zlatan tayari kafunga Magoli 28 ya ligi kwa timu yake ambayo inashika nafasi ya tatu katika Msimamo, nyuma ya vinara Los Angeles na Minnesota Walio Nafasi ya Pili.
#TransfersNews
@Harunlugoyah

Messi. Kukaa nje ya dimba …baada ya kupata majetaha

FC Barcelona Imethibitisha Nahodha wao, Lionel Messi atakuwa nje kwa muda Baada ya kupata majeraha mengine Katika game dhidi ya Villarreal Juzi Jumanne… Messi alitolewa baada ya dakika 45 za Kipindi Cha kwanza ikiwa ndio mechi yake ya kwanza tu msimu Huu Kuanza Kikosi Cha kwanza.

– Nyota huyo wa Kimataifa wa Argentina, alikosa Mechi Nne za mwanzo wa Msimu Huu, alirejea Kucheza Dakika 30 dhidi ya Borussia Dortmund Katika Champions League, pia alitokea Benchi Barcelona ikipigwa 2-0 Katika Laliga vs Granada na Alianza XI Jumanne na kuumia vs Villarreal ambapo alitoa Assist ya Goli Kabla ya kuumia Tena.

– Bila ya Kuwa na Messi, BarΓ§a imekuwa ikipata taabu sanaa kupata Matokeo, Kwa Ujumla Msimu huu imeshinda Mechi tatu, vipigo viwili na Sare Moja Katika Ligi na Suluhu dhidi Borussia Dortmund Katika Champions League… Kwa Matokeo hayo Katika Ligi yanawafanya kukaa nafasi ya tano Katika Msimamo na alama zao 10… pointi tatu nyuma ya Atletico Madrid na pointi Nne nyuma ya vinara Real Madrid..
#fcbarcelona #LaligaUpdates
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started