
Golikipa namba moja wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara chini ya umri wa miaka 20 ‘Ngorongoro Heroes’ Ally Salim amerejea kikosini baada ya kukaa nje ya uwanja kwa siku tatu kufuatia kuumia bega kwenye mechi dhidi ya Kenya.
Golikipa huyo wa Simba leo Jumamosi amefanya mazoezi na wenzake kujiweka fiti kwaajili ya mechi ya robo fainali ya michuano ya CECAFA Chalenji dhidi ya wenyeji Uganda utakaopigwa kesho Jumapili.
Daktari wa timu hiyo, Shecky Mngazija, amesema, “Tulimpa Ally mapumziko ya siku tatu baada ya kuumia lakini sasa yuko fiti na amefanya mazoezi yote. Kuhusu kuwa atacheza ama la, ni maamuzi ya kocha Mkuu.” Akizungumzia maandalizi ya mechi ya kesho, Kocha Mkuu, Zuberi Katwila amesema anafahamu kuwa kucheza na wenyeji ni kazi, lakini atatumia dakika 10 za mwanzo kuwasoma ili aweze kujua mbinu zaidi za kuwamaliza. “Tumesafiri jana, haikuwa safari nyepesi lakini leo tumefanya mazoezi mepesi kuwaweka wachezaji sawa kwaajili ya mechi. Utakuwa mchezo mgumu maana tunacheza na mwenyeji na hatujabahatika kumuona akicheza,” amesema Katwila. “Siwezi kubadili mbinu ambazo zimetufikisha hapa. Tunajipanga kushinda na vijana wako kwenye hali nzuri kushindana,” Mechi nyingine za robo fainali hapo kesho ni Burundi dhidi ya Kenya, Zanzibar na Eritrea zitakazochezwa Jinja wakati mechi nyingine hapa mjini Gulu ni Sudan dhidi ya Sudan Kusini.
#wapendasokaupdates
CAF Champions League :











