Simba mwendo mdundo mpaka ubingwa

Wakati wengine wakiutafuta ushindi kwa tochi, Simba ndo vinara wa ligi kuu wakishinda mechi zote nne walizocheza mpaka sasa

Katika mechi hizo Simba imefunga mabao 10 na kuruhsu mabao mawili tu

Watani zao Yanga hali yao ni tete baada ya hapo jana kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Polisi Tanzania inayonolewa na kiungo wa zamani wa Simba Selemani Matola

Matola amejitengenezea ufalme dhidi ya Zahera, mkufunzi wa Yanga

Kwani tangu alipokuwa na Lipuli Fc, Matola ni kawaida yake kuifunga Yanga

Yanga inashika nafasi ya pili kutoka chini kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama moja!

Mpaka sasa tayari Simba ina faida ya alama tano dhidi ya watani zao hao

Wachezaji wanaowania tuzo mchezaji bora EPL mwezi wa tisa

✍🏻 Wachezaji Nane wanaowania tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi wa Tisa (Septemba) ndani ya ligi Kuu Nchini Uingereza (Premier league).

1️⃣. Trent Alexander-Arnold (Liverpool)
🏟 Mechi 3⃣
✅ Ushindi 3⃣
️⚽ Goli 1️⃣.

2️⃣. Pierre-Emerick Aubameyang (Arsenal).
🏟 Mechi 4⃣
✅ Ushindi 1️⃣
🤝🏻 Sare 3⃣
️⚽ Magoli 5️⃣.
….
3⃣. Kevin De Bruyne (Manchester City).
🏟 Mechi 3⃣
✅ Ushindi 2️⃣
❌ Kipigo 1️⃣
️⚽ Goli 1️⃣
🎯 Assist 3⃣
….
4⃣. Riyad Mahrez (Manchester City).
🏟 Mechi 3⃣
✅ Ushindi 2️⃣
❌ Kipigo 1️⃣
️⚽ Goli 2️⃣
🎯 Assist 1️⃣
….
5️⃣. John McGinn (Aston Villa).
🏟 Mechi 3⃣
🤝🏻 Sare 2️⃣
❌ Kipigo 1️⃣
️⚽ Goli 2️⃣.
….
6️⃣. Ricardo Pereira (Leicester City).
🏟 Mechi 3⃣
✅ Ushindi 2️⃣
❌ Kipigo 1️⃣
️⚽ Goli 2️⃣
….
7️⃣. Son Heung-min (Tottenham).
🏟 Mechi 4⃣
✅ Ushindi 2️⃣
🤝🏻 Sare 1️⃣
❌ Kipigo 1️⃣
️⚽ Goli 2️⃣
🎯 Assist 2️⃣
….
8⃣. Callum Wilson (Bournemouth)
🏟 Mechi 3⃣
✅ Ushindi 2️⃣
🤝🏻 Sare 1️⃣
️⚽ Goli 4⃣
#PremieqrLeague #POTM
@Harunlugoyah

Michael Owen asema Manchester United kuwa ni “timu mbaya zaidi kwa miongo kadhaa”.

Mshambuliaji wa zamani wa England, Michael Owen amekitaja kikosi cha Manchester United kuwa ni “timu mbaya zaidi kwa miongo kadhaa”.

– The Red Devils wameanza ovyo msimu huu wa Ligi, Raundi ya Saba Wanajikuta wakiwa nafasi ya 10 kwenye jedwali la Ligi Kuu, alama Tisa tu sawa pointi 12 nyuma ya vinara wa ligi, Liverpool… Na Owen anaamini kikosi hicho ni timu mbovu kabisa ambayo hajaiona kwa muda mrefu licha ya juhudi za Solskjaer kujenga timu..
….
🗣 “Manchester United sasa ni timu ambayo ipo katikati mwa Msimamo wa ligi, Sidhani kama watakuwa ndani sita bora msimu huu, kibinafsi, Katikati ya Msimamo nadhani inawezekana.

🗣 “Hii ni Manchester United mbaya zaidi kuwahi kutokea, Tangu Sir Alex Ferguson kuondoka katika nafasi yake.

🗣 “Jambo ambalo ningependa kusema ni kwamba, Ole Gunnar Solskjaer ameidhoofisha timu yake bila kujua… Kuwaondoa watu kama Lukaku, Herrera, Matteo Darmian, Sanchez, Smalling. Anajua kabisa angeweza kuboresha timu yake na wachezaji hao, lakini Amefanya hivyo kwa kusudi bila kufikiria.
#PremierLeague #ManchesterUnited
@Harunlugoyah

SIWAFUNDISHI KAZI,ILA NAWAKUMBUSHA…STARS

SIWAFUNDISHI KAZI,ILA NAWAKUMBUSHA.

Na Octa Ayubu Jr

Nimejaribu kufuatilia kwa ukaribu uteuzi wa kikosi Cha timu ya taifa kwa makocha wote waliopita ndani ya miaka 10,Ni nadra Sana kuyakosa majina mawili Kelvin Patrick Yondan na Erasto Edward Nyoni.Hawa ni miongoni mwa wachezaji wakongwe ndani ya timu ya taifa.

Sahau kuhusu Juma kaseja aliyepumzishwa kwa kipindi kirefu kabla hajapitiwa na neema ya Ettiene Ndayragije na kurejeshwa.wahenga walishasema “Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha” lakini wakaongeza “Usipoziba ufa utajenga ukuta”. Erasto nyoni,Naweza kuthubutu kutamka sioni mchezaji anayekuja kuziba pengo lake kwa urahisi,kwasababu huyu ni mchezaji pekee anayeweza kumpa mwalimu option ya matumizi yake katika namba 5 tofauti.Ni mchezaji gani atakuja kukifanya anachokifanya nyoni? Makocha wanaliona hili? ile ngongoro iliyopo fainali ya Cecafa ina mbadala wa nyoni?

Yondan sio mchezaji wa nafasi nyingi Kama ilivyo kwa nyoni.Lakini tuliza akili,fikiri Ni nani wa kurithi mikoba yake? Tena sio kwa kucheza vizuri mechi moja tu,bali mchezaji atakayedumu kwenye kiwango Bora kwa muda mrefu Kama alivyofanya nyondani.

Sidhani kama Tff na makocha wanaoiongoza Tanzania walijaribu kuomba kadi zao wakaangalia umri wao,badala yake wanachoangalia ni mwendelezo wa ubora wao bila kufikilia Mwisho wao na Tutaziba vipi mapengo yao.

Nilianza kuiona sura ya kelvin Yondan kwenye miguu ya Yusuph mlipili bahati mbaya kwake Ni kuingia jeshini kipindi Cha Vita,huku mshare wa Saa ukifuta ndugu na kadi yake ya kliniki.Ndio ameingia Simba kipindi ambacho Simba inahitaji mafanikio hivyo kulazimika kuwa fiti muda wote na kama unapata majeraha urudi kwenye ubora mapema Jambo ambalo limekuwa gumu kwake huku umri wake ukiwa sio rafiki.

Kuna mechi nyingi za kirafiki tunacheza,lakini kwa bahati mbaya zaidi nazo Yondani na Nyoni wanacheza.hizi ndizo zilikuwa mechi za kutengeneza mbadala wao kama alivyoaminiwa Kelvin John.Lakini kitendo cha kuendelea kuwatumia Nyoni na Yondani Kuna Wakati tutawakumbuka,lakini tutakuwa tumekwishaumia

Hawajachelewa,Nyoni na Yondan bado wanacheza katika ubora lakini umri wao hauna tofauti na Gari la mkaa mda wowote litaingia gereji.Hawa mda wowote wanaweza kutangaza kustaafu tukabaki kutazamana Nani alaumiwe.

Tff kwa kushirikiana na Benchi la ufundi wanatakiwa kushauriana ni jinsi gani Tanzania itapata mbadala wa Hawa malegend wawili.Kuna mahali nilisema tusahau kuhusu kaseja kwa sababu katika nafasi yake kuna mwanga unaonekana kupitia kwenye mikono ya Aishi manula,mwanga wa nyoni ukizimwa na pumzi ya zahera Alipoamua kumpoteza Pato ngonyani na huku miguu ya Yondani ikimezwa na majeruhi ya Salim mbonde. ©Sokaplace Tanzania
Tags @tanfootball @taifastars_

Makocha wanaowania tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi wa Tisa (Septemba) EPL

Makocha wanne wameteuliwa kuwania tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi wa Tisa (Septemba) ndani ya Ligi Kuu Nchini Uingereza “Premier League”… Kura ya Mashabiki itajumuishwa na ile ya jopo la Wachambuzi wa mpira wa miguu kuamua mshindi atakayetangazwa wiki ijayo.

1️⃣. Eddie Howe (Bournemouth).
W2 D1 L0 GF8 GA4
– Howe aliongoza AFC Bournemouth katika ushindi wao wa kwanza vs Southampton, kaiongoza timu bila kufungwa na mabao nane wakifunga na kumaliza Mwezi Septemba nafasi ya nane.
….
2️⃣. Jurgen Klopp (Liverpool).
W3 D0 L0 GF6 GA2
– Mshindi wa tuzo ya mwezi Agosti, kaiongoza Liverpool kushinda game tatu Mfululizo, huko Stamford Bridge, Ushindi vs Sheffield United uliowafanya kushinda mechi 16 mfululizo ikiwa ni rekodi.

3⃣. Frank Lampard (Chelsea).
W2 D0 L1 GF8 GA4
– Chelsea chini ya Lampard ilifunga mabao nane mwezi huo. Matano walipata katika ushindi vs Wolverhampton Wanderers kabla ya kupata ushindi wa kwanza nyumbani, dhidi ya Brighton.
….
4⃣. Brendan Rodgers (Leicester City).
W2 D0 L1 GF7 GA2
– Baada ya kupata kipigo chembamba cha kwanza vs Manchester United, Rodgers akiiongoza Leicester City walipata ushindi dhidi ya Tottenham Hotspur na ushindi wa 5-0 dhidi ya Newcastle United ambao ulikuwa ushindi wao mkubwa katika Historia yao ndani Ligi Kuu na kuwafanya kumaliza nafasi ya tatu..
#PremierLeague #MOTM
@Harunlugoyah

Miraji na aussems..wataa tuzo za mwezi wa 9 VPL

Kocha Mkuu wa klabu ya Simba SC, Patrick Aussems amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Septemba wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2019/20..
..
– Wakati huo huo. MSHAMBULIAJI wa Mabingwa hao Watetezi, Miraji Athumani amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Septemba wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu wa 2019/20.
#VPLUpdates🇹🇿

Mario Mandzukic na Callum Wilson watakiwa kutua od traford

Mario Mandzukic na Callum Wilson ndio Washambuliaji wanao takiwa na klabu ya Manchester United kabla ya dirisha la uhamisho la Januari kufungwa.

– Meneja wa United, Ole Gunnar Solskjaer hivi karibuni alikiri klabu hiyo itaangalia kutafuta mfungaji mpya wa mabao katika mwaka mpya, na kwa mujibu wa vyanzo ni kwamba Mabosi wa United wanaendelea kuwafuatilia, Mshambuliaji huyo wa Juventus, Mandzukic na Wilson wa Bournemouth… Mfungaji bora wa Ligue 1 Mpaka Sasa, Moussa Dembele wa Lyon nae ni mchezaji mwingine kwenye orodha ya Wachezaji wanaotakiwa na United ambayo inasaka mbadala wa Romelu Lukaku, ambaye walimuuza kwenda Inter Milan.

– Mandzukic, 33, amebakiza miaka miwili tu kwenye mkataba wake na hakujumuishwa katika kikosi cha Ligi ya Mabingwa cha Juventus na hajacheza chini ya bosi mpya Maurizio Sarri, atapatikana tena wakati dirisha litakapo funguliwa tena baada ya kukataa kuhamia United, Paris Saint-Germain na klabu ya huko Qatar msimu wa joto…Callum Wilson amefunga mabao matano katika michezo saba ya Ligi Kuu hadi sasa, Wilson, 27, ana zaidi ya miaka mitatu kwenye mkataba wake na Bournemouth.
#TransfersNews #ManchesterUnited
@Harunlugoyah

Ditram Nchimbi aongezwa kikosi cha taifa

Kaimu kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania 🇹🇿, Etienne Ndayiragije amemuongeza Mshambuliaji hatari wa klabu ya Polisi Tanzania, Ditram Nchimbi katika Kikosi cha timu hiyo ya taifa kinachojiandaa na mechi ya Kirafiki dhidi ya Timu ya Taifa ya Rwanda 🇷🇼 … Ditram atakuwa Mchezaji wa 29 baada Wachezaji 28 kutangazwa na Kocha huyo siku ya Jana..
#TaifaStars

YANGA HAIJARIDHIKA NA SARE DHIDI YA POLISI JANA

Nahodha msaidizi wa timu ya Yanga, Juma Abdul amesema wachezaji hawaja ridhishwa na matokeo ya sare ya mabao 3-3 waliyopata jana dhidi ya Polisi Tanzania uliofanyika uwanja wa Uhuru.

Juma ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na majeruhi pamoja na maslahi yake binafsi amesema matokeo hayo hawaku yatarajia na yamewaumiza isipokuwa wanajipanga kwa michezo mingine.

Mlinzi huyo wa kulia amesema changamoto kubwa waliyonayo kwa sasa ni muunganiko wa wachezaji kwakua asilimia kubwa ni wageni. “Hatukuipenda sare dhidi Polisi, tulitarajia kupata ushindi lakini ndio sehemu ya mchezo tunajipanga kwa mchezo unaofuata dhidi ya Coastal Union. “Walimu wameona mapungufu yaliyojitokeza ninaamini watayafanyia kazi kabla ya mchezo wetu unaofuata siku ya Jumapili,” alisema nahodha huyo.

#wapendasokaupdates
#VodacomPremierLeague

Design a site like this with WordPress.com
Get started