
Ikiwa zimebaki wiki mbili kabla ya kufanyika kwa mbio za Rock City Marathon jijini Mwanza, wadau mbalimbali wanaotarajia kushiriki katika mbiohizo wameonyesha kufurahishwa na zawadi zitakazo tolewa kwa washindi na washiriki ikiwemo medali na fedha taslimu zaidi ya Sh Mil 30.
Mbio hizo zilizojinyakulia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi zinatarajiwa kufanyika Octoba 20 mwaka huu kwenye Viunga vya Jengo la Biashara la Rock City Mall huku wadau mbalimbali wakiwemo viongozi waandamizi serikalini akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw John Mongella wakitarajia kushiriki katika mbiohizo.

Mratibu wambio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International (CPI), Bw. Kasara Naftal amesema pamoja na medali washindi wa kwanza wa
mbio za kilomita 42 kwa wanaume na wanawake watajinyakulia Tsh. Mil 4 kila mmoja Tsh. Mil2/- kwa washindi wa pili na Tsh. Mil1/-kwa washindi wa tatu, huku washindi wa nne hadi kumi na tano nao pia wakiibuka na zawadi za medali na pesa taslimu.
Kwa upande wa mbio za Kilomita 21, Bw. Kasara amesema pamoja na medali washindi wa kwanza kwa wanaume na wanawake watajinyakulia Tsh. Mil2/- kila mmoja, Tsh. Mil1/- kwa washindi wa pili na Tsh. Laki7/- kwa washindi wa tatu huku pia washindi wa nne hadi wa kumi na tano wakiibuka na zawadi za pesa taslimu na medali kila mmoja.
•
“Kuhusu mbio za kilomita tano ambazo zitahusisha washiriki kutoka mashirika na taasisi mbalimbali (corporates) tunatarajia zitaongozwa na Mkuuwa Wilaya ya Nyamagana Dk. Philis Nyimbi sambamba na washiriki wenye ulemavu wa ngozi yaani albino ambapo zawadi za fedha taslimu zitatolewa kwa washindi watatu wenye ualbino pekee.”
•
Bw. Kasara aliongeza kuwa kwa washindi wa mbio za kilomita mbili na nusu zitakazo husisha watoto wenye umri kati ya miaka 7 hadi 10 watapatiwa fedha taslimu.

Mbio hizo zilizoanzishwa miaka kumi iliyopita zinatarajiwa kupambwa na maonesho ya wadau umbalimbali wakiwemo wadhamini wa mbiohizo kampuni za TIPER, Pepsi, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA).
•
Wadhamini wengine ni pamoja na kampuni ya uwakili ya Lis Law Chambers & Consultants.