Tazama.kikosi.kibovu cha FIFA mwaka.2019

Baada ya FIFA kutaja timu ya Wachezaji Bora wa mwaka ‘FIFA The Best’ wiki kadhaa zilizopita.

Gazeti maarufu la Uhispania Marca kama kawaida yake liliamua kuandaa toleo la 3 la kikosi cha wachezaji wabovu zaidi ‘The Worst X1’ ambapo wasomaji wake walipiga kura kuchagua kikosi hicho.

Ila malalamiko yameanza kujitokeza baada ya beki wa Arsenal, Mustafi kunukuliwa akisema 🗣”Mimi sio beki wa pili mbaya zaidi ulimwenguni. Ninaweza pia kukabiliana na ukosoaji mgumu. Lakini ukosoaji umezidi na hauna maana. Nimekuwa mlengwa katika hili. Wakati fulani, watu hata walinilaumu tukifugwa na wakati huo nilikuwa sijacheza hata.”😀

Katika kikosi icho wachezaji watatu wa Manchester United wapo kwenye Kikosi Kibovu cha mwaka.

Nani kaonewa? Nani kakosekana?

Thomas Muller. Kuondoka Bayern Munich

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na BILD, Mshambuliaji wa Fc Bayern Munich Thomas Muller anataka kuondoka klabuni hapo mapema mwezi Januari kwenye usajili wa dirisha dogo 😱. . .
Mabosi wa klabu hiyo wanatarajia kuanza mazungumzo na nyota huyo Mjerumani siku za hivi karibuni ili kuhakikisha anabadilisha maamuzi yake. . .
Inasemekana moja ya sababu inayomfanya Muller afikirie kuondoka ni kutopata muda mwingi wa kucheza ndani ya kikosi hicho chini ya kocha Mcroatia Niko Kovac 😔
.
.
Written by @officialfelixtz
.
.
Powered by @mcheza_tz @bussi_ntua @tshombee1 #sokaonlineupdates

Allasane Plèa kuziba pengo la Mbappe!.

Allasane Plèa kuziba pengo la Mbappe!.
.
Allasane Plea🇫🇷 mchezaji wa klabu ya Borussia Mönchengladbach ya nchini Ujerumani ameoitwa katika timu ya taifa ya Ufaransa kwa ili kuziba nafasi ya Kylian Mbappe ambaye ni majeruhi.
.
Plea mwenye umri wa miaka 26 amefanikiwa kuitumikia timu ya wakubwa ya ufaransa mechi moja tu katika maisha yake ya soka!.Huenda ikawa nafasi yake ya pili kulitumikia taifa lake la Ufaransa!.
.
Kuelekea mechi za kufuzu EURO2020 Ufaransa imekumbwa na majeruhi kadhaa kwa wachezaji wake muhimu jambo linalomfanya Deschamps kufanya mabadiliko na kuingiza sura mpya katika timu hiyo ya taifa🇫🇷.
.
Plea mchezaji wa zamani wa Nice,Auxerre na Lyon anaemudu nafasi ya winga na mshambuliaji wa kati tangu ajiunge na Borussia Mönchengladbach mwaka 208 amecheza mechi 41na kufunga magoli 16.
. .Anakwenda kuchukua nafasi ya Mbappe Lottin.Ataweza kuziba pengo la Mbappe ?
.
.
Written by @anode360

Zlatan Ibrahimovic atengenezewa sanamu nchini kwao

✍🏻 Zlatan Ibrahimovic Amezindua Sanamu lake Binafsi nchini kwao Sweden 🇸🇪.. Hii ni Heshima nyumbani kwao akitambulika kama Legend 👏🏻👏🏻.
… “Unapokuja New York utaona Sanamu ya Uhuru, unapokuja Sweden, unataona Sanamu ya Zlatan.” @iamzlatanibrahimovic 🇸🇪 Akithibitisha Ufalme wake nchini kwao 🤴
#ZlatanIbrahimovic #Sweden
@Harunlugoyah

TANZANIA YAFUZU NUSU FAINALI

Timu ya taifa ya Tanzania ya mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’, imefuzu kucheza nusu fainali ya michuano ya Afrika ijulikanayo kama CANAF inayoendelea katika jiji la Benguela, nchini Angola.

Tembo warriors imefika hatua hiyo baada ya kuifunga Timu ya taifa ya Cameroon kwa magoli saba kwa sifuri (7-0) na sasa itakutana na Nigeria katika hatua hiyo ya nusu fainali, siku ya Alhamisi ya tarehe 10 Oktoba, 2019 baada ya kupisha mapumziko ya siku ya kesho, Jumatano.

Katika mchezo huo pia mtanzania Khalfani Majani ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga hattrick katika michuano ya mwaka huu baada ya kupachika magoli manne wavuni.

Khalfani Majani ndiye aliyekua mfungaji bora wa ligi ya ndani kwa ngazi ya vilabu na pia mfungaji bora wa michuano ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na huku magoli hayo pia yakimuweka katika nafasi nzuri ya kuwania ufungaji bora kwa bara la Afrika.

Tuendelee kuunga mkono na kuiombea Tembo Warriors. Viva Tanzania 💪🇹🇿

Mlinda lango, Dean Henderson ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England

✍🏻 Mlinda lango, Dean Henderson ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England kufuatia kuondoshwa katika kikosi mlinda lango, Tom Heaton kufuatia kupata jeraha… Henderson, ambaye anacheza kwa mkopo Sheffield United kutoka Manchester United, atajiunga na kikosi hicho cha kocha Gareth Southgate kwenye dimba la St. George leo Jumatano, kuelekea game zao mbili dhidi ya Jamhuri ya Czech na Bulgaria.

✍🏻 Henderson 22; ameitwa kwa mara ya kwanza kabisa baada ya Heaton kurudi Aston Villa kwa ajili ya kufanyiwa tathmini zaidi juu ya jeraha alilopata wakati wa ushindi wao wa 5-1 dhidi ya Norwich City mwishoni mwa wiki iliyopita…. Henderson, ambaye hapo awali alikuwa akiiwakilisha England katika ngazi za U16 hadi kiwango cha U21, atakuwa sehemu ya kikosi cha watu 24 kwa safari ya kwenda Jamhuri ya Czech Ijumaa na kwa mechi yao nyingine huko Bulgaria Jumatatu ijayo.

✍🏻 Dean Henderson ana Clean Sheets 24 tangu kuanza kwa msimu Uliopita; ni idadi kubwa zaidi ya Makipa wote katika Madaraja yote Manne ya Ligi za Uingereza… Kwenu Manchester United, De Gea au Henderson?! 😄😄.
#England #EURO2020Q #UEFAEURO
@Harunlugoyah

Rais wa Liberia 🇱🇷, Mh. George Weah..afanya mazoezi na timu ya taifa

– Rais wa Awamu ya 25 wa Liberia 🇱🇷, Mh. George Weah jana alifanya mazoezi ya mwisho yeye pamoja na Wachezaji wa timu yao ya taifa kuelekea game yao ya hii leo ya kuwania kufuzu kucheza hatua ya Makundi ya Kuwania kucheza fainali za Mataifa ya Afrika AFCON 2021..

– Rais Weah Ni Mshindi mara tatu wa tuzo ya Mchezaji Bora Afrika, Mshindi mara moja wa tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia wa FIFA na Mchezaji wa kwanza na wa Pekee kutoka Afrika kushinda tuzo ya Ballon d’Or, Alifanya Mazoezi hayo na Lone Star akiwa na Jezi ya klabu ya Lille ambayo anavaa Mtoto wake, Timothy Weah… Lakini Mtoto wake huyo Anaitumikia timu ya taifa ya Marekani 🇺🇸!.. #TotalAFCON2021 #AFCON2021Q
@Harunlugoyah

Makundi klabu bingwa CAF kujulikana.leo

👉 Majira ya Saa Mbili za Usiku hii leo, Makundi ya Klabu Bingwa Afrika Msimu huu 2019/20 yatajulikana baada ya Droo kukamilika huko Cairo, Nchini Misri… Vilabu vilivyofuzu Vikiwa katika Vyungu Vinne tayari kwa Makundi Kupangwa..

POT A
Espérance Tunis 🇹🇳
TP Mazembe 🇨🇩
Wydad AC 🇲🇦
Al Ahly SC 🇪🇬

POT B
Etoile Sahel 🇹🇳
Mamelodi Sundowns 🇿🇦
Zamalek SC 🇪🇬/Generation Foot 🇸🇳
Raja CA 🇲🇦

POT C
USM Alger 🇩🇿
ZESCO United 🇿🇲
AS Vita Club 🇨🇩
Al Hilal Club 🇸🇩

POT D
Primeiro de Agosto 🇦🇴
Petro Atletico 🇦🇴
JS Kabylie 🇩🇿
FC Platinum 🇿🇼
#TotalCAFCL #CAFCL

Kocha wa zamani.wa cameroon. Adai malipo yake

✍🏻 Kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Cameroon 🇨🇲, Clarence Seedorf na msaidizi wake Patrick Kluivert wanalidai Shirikisho la soka nchini Cameroon fedha, $8M kufuatia kufukuzwa kwenye kazi zao ya Ukocha wakiwa bado wana Mkataba nao..
..
✍🏻 Makocha hao wawili walidumu chini ya mwaka mmoja katika majukumu yao na walitimuliwa baada ya Cameroon kufungwa hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ya mwaka wa 2019 na timu ya taifa ya Nigeria… Kwa ujumla Seedorf kaiongoza Cameroon katika mechi 10 games, Ushindi mechi Tatu, Droo Nne, na Vipigo Vitatu..

✍🏻 Kulingana na Chombo cha habari cha Cameroon, Seedorf na Kluivert wamewasilisha malalamiko yao Shirikisho la Soka Duniani “FIFA” wakitaka pesa zao Takribani Tshs 18.4 Trillion 😆 kama fidia ya kutimuliwa na Cameroon kabla ya kandarasi yao ya miaka nne haijamalizika tangu kuteuliwa kwao Agosti 2018..
#Updates
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started