Ujue uwanja wa FNB Stadium ambao ni uwanja wa mpira mkubwa zaidi barani Afrika


Jina kamili la uwanja huu ni First National Bank Stadium, au Soccer City pia hufahamika kwa jina la “The Calabash” uwanja huu upo kwenye mji mdogo wa Nascer uliopo Kwenye Manispaa ya Johannesburg Afrika Kusini

Uwanja huu hutumiwa na klabu ya Kaizer Chiefs kama uwanja wao wa nyumbani kwenye michezo ya ligi kuu ya Afrika Kusini PSL pia hutumika kwenye mechi za kimataifa wa timu ya taifa ya Afrika Kusini Bafana Bafana pia hutumika kwenye michezo mbali mbali ya klabu bingwa barani Afrika

Uwanja huu unaongoza kwa ukubwa barani Afrika ukiwa na uwezo wa kuchukua jumla ya watazamaji Elfu tisini na nne mia saba thelathini na sita [94,736] , pia uliwahi kuweka rekodi ya kujaa zaidi ya idadi inayotakiwa, ilikuwa August 1 mwaka 2015 kwenye mchezo wa Soweto derby ambapo Kaizer Chiefs “Amakhosi” waliwakaribisha Orlando Pirates uwanja huu uliingiza jumla ya watazamaji 94,807

Uwanja huu ulifunguliwa rasmi mwaka 1989 na mwaka 2009 ulifanyiwa maboresho kwa kupanuliwa na kuongezwa ukubwa eneo la majukwaa ya watazamaji

Mwaka 1996 uwanja huu ulipewa heshima ya kuchezwa fainali ya Afcon ambapo Afrika Kusini walitwaa ubingwa baada ya kushinda 2-0 dhidi ya Tunisia, pia mwaka 2013 ambapo fainali ilichezwa hapo FNB na Nigeria walipata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Burkinafaso


Uwanja huu pia ulitumika kwenye michuano ya kombe la dunia mwaka 2010 na fainali ya michuano hiyo ilipigwa kwenye uwanja huo

Uwanja huu pia utatumika February 29 mwaka huu kwenye mchezo wa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Afrika Kusini PSL ambapo Orlando Pirates watakuwa wenyeji wa mchezo dhidi ya Kaizer Chiefs

Kihistoria uwanja huu ulikuwa sehemu ya kwanza kabisa ya Hayati Nelson Mandela kufanya mkutano wake baada ya kutoka kifungini gerezani mwaka 1990

Powered by @sports_lady_tz
#dailysporttz

Brescia wamtimua kocha wao mkuu

Brescia wamethibitisha kumuondoa katika nafasi yake aliyekuwa Kocha wao mkuu Eugenio Corini ….

mwendelezo mbovu ndani ya Serie A imekuwa kigezo namba moja, lakini namba mbili ni baada ya kushindwa kupata matokeo katika michezo saba ya ligi kuu ya Italy na kishindwa kujinusuru kuepuka mstari wa timu zinazoshuka daraja wakisalia nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi ya Seria A

NAMUNGO FC MAJALIWA WABISHI KINOMANOMA

HITIMANA Thiery, Kocha Mkuu wa Namungo FC amesema kuwa ni kwenye Uwanja wao wa Majaliwa hakuna kilichofukiwa zaidi ya jitihada za wachezaji kutafuta matokeo.
Kwenye mechi tisa ilizocheza Uwanja wa Majaliwa msimu huu, imeshinda mechi saba na kutoa sare moja na imefungwa mechi moja na mbishi wake akiwa ni Coastal Union kutoka Tanga.
Thiery amesema kuwa hakuna walichofukia kwenye uwanja wao wa nyumbani zaidi ya wachezaji wake kujituma na kutumia vema Uwanja wa nyumbani.
“Ligi ni ngumu na tunatambua kwamba tukiwa ugenini tunapata tabu kupata matokeo kwa kuwa wenyeji wanakuwa na mashabiki wao ila sisi hatuna hivyo tukiwa nyumbani tunapambana kupata ushindi,” amesema.
Mechi ilizocheza Uwanja wa Majaliwa imefunga jumla ya mabao 13 na kufungwa mabao matano, leo ina kazi mbele ya Alliance FC mchezo utakaochezwa uwanjani hapo.
Matokeo ya Uwanja wa Majaliwa yapo namna hii:- Namungo 2-1 Ndanda, Namungo 2-0 Singida United, Namungo 0-0 Mwadui, Namungo 1-0 Lipuli, Namungo 1-0 Mtibwa Sugar, Namungo 2-1 Ruvu Shooting, Namungo 1-3 Coastal Union, Namungo 1-0 Polisi Tanzania, Namungo 3-0 Mbao.

Visit website

Liverpool yaponea chupuchup kuondoshwa FA


Chipukizi wa Liverpool, Neco Williams na Adam Lewis wakishangilia baada ya timu yao kupata bao pekee dakika ya 75, Ro-Shaun Williams akijifunga katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Shrewsbury Town jana Uwanja wa Anfield kwenye mchezo wa marudio Raundi ya Nne Kombe la FA, England kufuatia mchezo wa kwanza kumalizika kwa sare ya 2-2 Januari 26 Uwanja wa Montgomery Waters Meadow

Leicester na Newcastle wapo vitani kumwania nyota wa Brentford, Said Benrahma

Leicester na Newcastle wapo vitani kumwania nyota wa Brentford, Said Benrahma anayefikia thamani ya Pauni 15m

..
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Algeria, ambaye amesaidia Brentford kukwea hadi nafasi ya tano katika michuano ya Championship mpaka sasa huenda akasajiliwa na vilabu vya ligi kuu ya uingereza

Arsenal yaingia sokoni tena

Kiungo wa kati wa Feyenoord Orkun Kokcu ndiye mlengwa anaetazamwa na Arsenal katika dirisha la uhamisho majira ya joto (Daily mail)


Feyenoord ipo tayari kumwachia kijana huyo mwenye umri wa miaka 19 majira ya joto, lakini itahitaji ada ya zaidi ya pauni milioni 15 ili kimwachia kijana huyo.


Arsenal wametuma mascouts kumtazama kijana huyo wa Feyenoord

Manchester United matatani Sergio Romero akiondoka

Manchester United hawajapata mbadala endapo kipa wao Sergio Romero atajaribu kulazimisha kuondoka majira ya joto – (The Sun)


Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake wa sasa, …

kwa upande wa kipa chaguo la tatu Lee Grant anaonekana kufuata nyayo za Romero kwani anata kuondoka majira ya joto pindi mkataba wake utakapo malizika

Design a site like this with WordPress.com
Get started