Wachezaji waliotangaza kustaafu soka kwa mwaka huu :

Wachezaji waliotangaza kustaafu soka kwa mwaka huu
:
๐Ÿ‘‰-Robin van Persie
๐Ÿ‘‰-Xavi
๐Ÿ‘‰-Fernando Torres
๐Ÿ‘‰-Claudio Marchisio
๐Ÿ‘‰-Ashley Cole
๐Ÿ‘‰-Wesley Sneijder
๐Ÿ‘‰-Bastian Schweinsteiger
๐Ÿ‘‰-Arjen Robben
๐Ÿ‘‰-Samuel Eto’o
๐Ÿ‘‰-Patrice Evra
๐Ÿ‘‰-Peter Crouch
๐Ÿ‘‰-Darren Bent
๐Ÿ‘‰-Tim Howard
๐Ÿ‘‰-Chad Marshall
:
Mchezaji gani utamkumbuka zaidi kati ya hawa?

Cannavaro kutafuta mkataba mwingine taifa stars

“Cannavaro baada ya kupata mkataba na timu ya taifa tukamtakia kila la heri kwa sababu alikuwa mchezaji wetu tena nahodha na badaye akawa meneja lakini mkataba wake umekwisha na timu ya taifa imemuhitaji. Hiyo ndiyo taarifa rasmi”-Hassan Bumbuli, afisa Habari wa Yanga amenukuliwa na kituo cha radio akifafanua kuhusu nafasi ya Cannavaro kama meneja wa Yanga.
โ€ข
“Alivyokuwa Yanga TFF walitueleza kuwa wanamuhitaji Cannavaro, wakaambiwa mkatabawake umekwisha wanaweza kumtumia. Hata kama bado angekuwa na mkataba tungemruhusu aende kujiunga na benchi la ufundi la timu ya taifa huku atoe nafasi kwa watu wngine.”

Ndairagije aongeza beki mwingine kikosini taifa stars

– Beki wa kati wa klabu ya Azam FC, Oscar Masai, ameongezwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kilichoingia kambini jana.

– Stars imeingia kambini kujiandaa na mechi mbili, ya kwanza ikiwa ni ya kirafiki dhidi ya Rwanda ‘Amavubi’, itakayopigwa jijini Kigali Oktoba 14 mwaka huu, pamoja na ile ya marudiano ya kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Sudan Oktoba 18 mwaka huu.

– Masai, ambaye ni mmoja wa mabeki chipukizi wanaochipukia kwa kasi nchini, alikuwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana ‘Ngorongoro Heroes’ kilichotwaa ubingwa wa vijana wa CECAFA wikiendi iliyopita..
#TaifaStars #CHAN2020Qualifiers

Mchanganuo wa vyungu vya makundi klabu bingwa afrika

Timu zilizopo kwenye Chungu A zimewekwa humo kwa sababu ndizo zina Points kutokana na ushiriki wao mzuri kwenye mashindano ya klabu Afrika na pia zimetoka kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

– Haziwezi kukutana timu za kutoka Chungu Kimoja wala Chungu A v B haziwezi Kukutana, sababu timu za Chungu B nazo zina points lakini zimetokea kwenye hatua ya kwanza ya Kombe la Shirikisho..

– Timu zilizo kwenye Chungu A zitakutana na timu kutoka Chungu D, lakini timu mbili za Chungu D zitabaki….Timu zilizo kwenye Chungu B zitapangwa na timu kutoka Chungu C, lakini pia timu mbili za Chungu C zitabaki.

– Timu mbili zitakazobaki kwenye Chungu C zitakutanishwa na timu mbili zitakazobaki kwenye Chungu D na hivyo kukamilisha jumla ya mechi 16 za mtoano, ambapo Washindi wa Jumla 16 watafuzu kucheza hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu 2019/20…
#CAFCCUpdates #CAFCC #TotalCAFCC
@Harunlugoyah

Simba sc yatoa Taarifa Rasmi kuhusu wachezaji wake

Taarifa Rasmi iliyotolewa na Klabu ya Simba SC, ikitoa ufafanuzi kamili juu la Sakata la Wachezaji wake, Jonas Mkude, Clatous Chama, Gardiel Michael na Erasto Nyoni..

– Pia Klabu hiyo Imethibitisha kuwa Kiungo wao wa Kimataifa wa Kenya, Francis Kahata alipewa ruhusa ya kwenda kwao kwa Matatizo Binafsi, na Sasa amerejea na yupo na timu… Taarifa ya klabu hiyo imesema kuwa Taarifa zoote tofauti zinazotolewa nje ya klabu ni za UONGO..
#VPLUpdates #SimbaSC

Simba sc yatoa Taarifa Rasmi kuhusu wachezaji wake

Taarifa Rasmi iliyotolewa na Klabu ya Simba SC, ikitoa ufafanuzi kamili juu la Sakata la Wachezaji wake, Jonas Mkude, Clatous Chama, Gardiel Michael na Erasto Nyoni..

– Pia Klabu hiyo Imethibitisha kuwa Kiungo wao wa Kimataifa wa Kenya, Francis Kahata alipewa ruhusa ya kwenda kwao kwa Matatizo Binafsi, na Sasa amerejea na yupo na timu… Taarifa ya klabu hiyo imesema kuwa Taarifa zoote tofauti zinazotolewa nje ya klabu ni za UONGO..
#VPLUpdates #SimbaSC

Klabu ya AC Milanyatangaza kocha mpya

Klabu ya AC Milan imemteua kocha mkuu wa zamani wa Inter Milan, Fiorentina na Lazio, Stefano Pioli kama meneja wao mpya, kufuatia kumtimua aliyekuwa kocha wao, Marco Giampaolo jana Jumanne baada ya kudumu miezi mitatu tu…Pioli Raia wa Italia ๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡น, 53, anakuwa kocha wa kudumu wa tisa wa Rossoneri tangu waliposhinda taji la Serie A mara ya mwisho mnamo 2011..

– Hashtag ya #PioliOut ili- trend kiasi kikubwa kwenye Mtandao wa Twitter nchini Italia Jana Jumanne, mashabiki wasio na furaha wakipinga kuteuliwa kwa kocha huyu, lakini haijazuia kupewa Kandarasi ya Miaka Miwili hii hii leo

– Milan ni ya 13 katika Msimamo ws Serie A, alama tatu juu ya eneo la kushuka Daraja.. AC Milan, mabingwa mara saba wa Ulaya, hawajacheza kwenye Ligi ya Mabingwa tangu 2013-14…lakini Klabu hiyo ingeweza kushiriki Europa League mwaka huu, lakini kwa sasa inatumikia adhabu ya kufungiwa mwaka mmoja kutoshiriki Michuano ya Ulaya kufuatia uvunjaji wa Sheria za Financial Fair Play.
#ACMilan #SerieA #TransfersNews
@Harunlugoyah

Ligi ya Ufaransa (Ligue 1) ndio ligi ambayo imechezwa michezo mingi kwa kila timu hadi sasa

Ligi ya Ufaransa (Ligue 1) ndio ligi ambayo imechezwa michezo mingi kwa kila timu hadi sasa, PSG wanaongoza ligi hiyo katika hali ambayo haimshangazi yeyote ambaye amekuwa akiifatilia ligi hii tangu ambapo Olympique Lyon ilitwaa mataji 7 mfululizo.

PSG wanaongoza ligi kwa tofauti ya pointi 2 wakiwa wamewazidi Nantes wanaofuatia kwenye nafasi ya pili huku Angers wakiwa kwenye nafasi ya 3 katika mfululizo wa yale ambayo hatukuyatarajia kuyaona mpaka wakati huu.

Ambacho hakikutarajiwa ni kuona PSG wakiwa wamefungwa mechi mbili hati kufikia wakati huu hali inayoashiria kuongezeka kwa ushindani kwenye ligi hii ambayo ilikuwa ikidharauliwa kwa jinsi ambavyo ilionekana kutawaliwa na klabu moja kwa muda mrefu.

Katika orodha ya mambo ambayo huwezi kuacha kujadili ni nafasi ya Olympique Lyon ambayo tayari wametangaza kuachana na kocha wao Sylvinho baada ya mlolongo wa matokeo mabaya ambayo yamewaacha wanaingia kwenye wiki ya kimataifa wakiwa nafasi ya 14 kwenye ligi baada ya kushinda mechi mbili pekee.

Msimu uliopita Lille wakichagizwa na nyota wao Nicolas Pepe ambaye walimuuza kwenda Arsenal, hakuna mengi yakiyobadilika hadi sasa kwa timu hiyo ambayo imetoa mtu aliyeongoza kwa ufungaji na kwa mara nyingine akiwa mwafrika anayetokea Nigeria Victor Osimhen ambaye hadi sasa amefunga mabao 7 akifuatiwa na Wissam Ben Yedder aliyehamia Monaco akitokea Sevilla, Habib Diallo (FC Metz) na Moussa Dembele (Lyon) wote wakiwa wamefunga mabao 6.

Burudani hii huwezi kupata sehemu yoyote isipokuwa kupitia kingโ€™amuzi cha @StarTimesTz pekee. Ukiwa na kingโ€™amuzi cha Antenna utalipia kifurushi cha UHURU Tsh. 18,000 tu na kingโ€™amuzi cha Dish utalipia kifurushi cha SMART Tsh. 21,000 tu.

#StartimesPekee #MpiraPasiMpiraGoli

VAR yasitishwa katika mechi ya Ligi ya Saudia Arabia

VAR yasitishwa katika mechi ya Ligi ya Saudia Arabia baada ya mmoja wa wafanyikazi kwenye uwanja huo kuchomoa kifaa cha VAR ili kuchaji๐Ÿ”Œ simu yake๐Ÿ˜

Hii ilikuwa mechi kati ya Al-Nassr na Al-Fateh utata ulipojitokeza baada ya mwamuzi kutaka kutumia VAR katika tukio la faulo lililojitokeza uwanjani.

Mechi ilimalizika kwa Al Nassr kushinda bao 1-0.

Design a site like this with WordPress.com
Get started