NUSU FAINALI CANAF 2019 TANZANIA KUCHEZA NA NIGERIA LEO

NUSU FAINALI CANAF 2019
TANZANIA KUCHEZA NA NIGERIA LEO

Muda: 10h00( Angola ) Saa 6 mchana( Tanzania )

Ni katika Mashindano ya mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu Afrika ‘CANAF’ MSHINDI KUTINGA FAINALI. Tuiombee Tanzania, Tuwaombee Watanzania
πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Manara-hakuna anaeidai simba

Afisa Habari wa Simba Haji Manara amesema klabu hiyo haidaiwi na mchezaji yeyote, na kuwa kinachowakabili baadhi ya wachezaji ni masuala ya utovu wa nidhamu

Mapema jana uongozi wa Simba ulitoa tamko kuhusu sintofahamu inayowakabili wachezaji wake wanne Jonas Mkude, Clatous Chama, Gadiel Michael na Erasto Nyoni

Baadhi ya vyombo vya habari vilizusha kuwa wachezaji hao wamegoma lakini Simba imebainisha kuwa walisimamishwa kwa muda wakisubiri hatma yao baada ya kupelekwa kamati ya Nidhamu kufuatia kukabiliwa na matukio ya utovu wa nidhamu

“Simba haidaiwi hata senti na mchezaji yeyote, sisi tulishavuko huko kitambo,” amesema

Aidha Manara amewataka waandishi wa habari kupata taarifa sahihi kutoka kwa uongozi wa Simba badala ya kutunga habari zisizo na ukweli

Hatma ya nyota hao itafahamika baada ya kumaliza majukumu ya timu za Taifa

Jose Mourinho kumrithi Pochettino,

Aliyekuwa mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anapigiwa chapuo kurithi mikoba ya Mauricio Pochettino, kocha wa Tottenham Hotspurs

Pochettino amekalia kuti kavu baada ya timu hiyo kuanza msimu vibaya

Spurs ambayo ilitinga fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa msimu uliopita, wiki iliyopita ilikuwa mbaya kwao

Walifungwa mabao 7-1 na Bayer Munich kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa na baadae kufungwa mabao 3-0 na Southampton mchezo wa ligi kuu

Inaelezwa Spurs wako katika mchakato wa kusaka kocha mpya, Mourinho akitajwa kuongoza wanaowania nafasi hiyo

Ousmane Dembele kuikosa elclasico

Winga wa Barcelona Ousmane Dembele anatarajia kuukosa mchezo wa Clasico dhidi ya Real Madrid baada ya kusimamishwa kwa mechi mbili kutokana na kauli yake kwa mwamuzi Mathayo Lahoz katika mchezo dhidi ya Sevilla

Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alionyeshwa kadi nyekundu kwenye mechi ambayo Barca ilishinda 4-0, huku mwamuzi akiandika katika ripoti yake rasmi kwamba Dembele alimwambia: “Wewe ni mbaya sana”.

Lionel Messi na Kocha mkuu Ernesto Valverde walimtetea winga huyo wa zamani wa Dortmund, wakidai kuwa haongei Kihispania vizuri, na kupendekeza adhabu yake ipunguzwe kama ikiwezekana.

Lakini shirikisho la mpira wa miguu nchini Uhispania limemsimamisha michezo wa miwili ikimaanisha kwamba Dembele atakosa mechi za ligi dhidi ya Eibar na Real Madrid

Bocco aanza mazoezi kuweka mwili fiti

Nahodha wa Simba John Bocco ameanza mazoezi mepesi tayari kurejea kikosini baada ya kuwa nje kwa zaidi ya wiki saba

Meneja wa Simba Patrick Rweyemamu amesema mkongwe huyo amepona majeraha na ameanza mazoezi mepesi

“Bocco amerejea na ataonekana hivi karibuni akiwa na wenzake ikiwa ni baada ya kuwa nje kwa miezi kadhaa kutokana na kupata majeraha ambayo yamemfanya akose mechi zetu za ligi na michuano ya kimataifa,” amesema

Kurejea kwa Bocco ni habari njema kwa kikosi cha Patrick Aussems kuelekea mchezo dhidi ya Azam Fc Oktoba 23

Bocco aliumia kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Azam August 17, anaweza kuwa fit kuwavaa waajiri wake hao wa zamani

Yanga sc yatamba hatuiofii Pyramids

Uongozi wa klabu ya Yanga umesema umeipokea kwa furaha droo ya mtoano wa michuano ya kombe la Shirikisho wakiwa wamepangwa kucheza na Pyramids Fc ya Misri

Akizungumza baada ya droo hiyo iliyofanyika jana nchini Misri, Afisa Habari wa Yanga Hassan Bumbuli amesema wanazo taarifa za kutosha kuhusu mpinzani wao na wameanza rasmi maandalizi kuelekea mchezo huo

“Tunafahamu ni timu iliyoanzishwa mwaka 2008. Msimu uliopita ilimaliza nafasi ya tatu ligi kuu ya Misri na hivyo kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kombe la Shirikisho,” amesema

“Pia tunafahamu katika mechi zao nne za kombe la Shirikisho mpaka kufika hatua hii, wameshinda mechi mbili ugenini, sare na ushindi nyumbani”

“Ni timu yenye utajiri mkubwa, mapema mwaka huu tunafahamu ilinunuliwa na matajiri kutoka Arabuni”

“Lakini hilo halitutishi Yanga kwa sababu tunafahamu hii ni mara yao ya kwanza kushiriki michuano ya Kimataifa”

“Miaka ya hivi karibuni tumecheza Misri na vilabu vya Al Ahly na Zamalek na tulitoa ushindani mkali. Hivyo sisi hatuzihofii kabisa timu kutoka Misri”

“Kwa sababu tumeshamfahamu mpinzani wetu, tutaboresha ratiba yetu ya maandalizi ili kuhakikisha tunakuwa tayari kupata ushindi kwenye mchezo wa nyumba ambao utapigwa Oktoba 27”

Pyramids Fc inakadiriwa kuwa na kikosi chenye thamani ya zaidi ya Bil 60, ikinolewa na kocha wa zamani wa Uganda Cranes Sebastiane Desabre ambaye aliipeleka Uganda Misri kwenye michuano ya Afcon 2019

Pamoja na timu hiyo kuwa ngeni, uwekezaji mkubwa uliowekwa ni ishara kuwa wanataka mafanikio ya haraka kwenye soka la Afrika

Ukingalia klabu hiyo imeanzishwa mwaka 2008 na mwaka jana ilibadilishwa jina na kuitwa Pyramids Fc

Ndani ya msimu mmoja matajiri wametumia zaidi ya Tsh Bilioni 60 kuunda kikosi

Hapa Yanga lazima ifanye maandalizi ya kutosha na muhimu zaidi ni kuhakikisha wanapata ushindi kwenye mchezo wao wa nyumbani kwani ni kawaida timu za Misri zinapokuwa kwao ni ngumu kufungika

HISTORIA KIDOGO YA KOCHA MKUU WA PYRAMIDS

Anaitwa Sebastien Desabre, amezaliwa Aug 2, 1976, huko Valence, France. Kwa sasa ana miaka 43 na ni raia wa ufaransa.
:
πŸ‘‰ Amewahi kufundisha vilabu vifuatavyo, ESC Rocheville (France) kama kocha Msaidizi , ASEC Mimosas (Cote D’Ivoire), CS Garoua (Cameroon), Esperance deTunis (Tunisia), Clube Recreativo Desportivo Libolo (Angola), Dubai Club (United Arab Emirates), JS Saoura (Algeria), Wydad Athletic Club (Morocco) na Ismaily (Egypt)
:
πŸ‘‰ Pia aliongoza timu ya taifa ya Uganda (December 2017 – July 2019
:
πŸ‘‰ Tetesi kutoka Uganda zinaeleza kuwa, wakati anaondoka Uganda, baadhi ya vilabu vya Misri vilimnyemelea.
:
πŸ‘‰ Klabu ya Sahel ilipeleka ofa ya $16,000 kwa mwezi ambayo ni sawa na Tsh Mil 37 lakini akapiga chini ofa hiyo ya mboga.
:
πŸ‘‰ Al Ahly wakapanda dau mpaka kufikia $70,000 sawa na Tsh Milion 160 pia akapiga chini na kwenda kuchukua $90000 sawa na Tsh milion 203
:
πŸ‘‰ Hata hivyo wakala Wake Mr. Kanga pia ni wakala wa makocha wakubwa kama vile Herve Renard aliyetimuliwa Morocco, Alain Giresse (Tunisia), Hugo Broos, ambaye aliiongoza Cameroon kunyakua taji la AFCON 2017.
:
πŸ‘‰ Hapo awali akiwa na timu ya taifa ya Uganda Mwaka 2017 inasadikika kuwa alisaini mkataba wa malipo ya $25,000 kwa Mwezi sawa na Tsh Milion 58

Historia ya wapinzani wa yanga sc…Pyramids kutoka misri

Pyramids ni timu changa katika michuano ya kimataifa na pia katika anga la vigogo wa soka barani Afrika.
:
⚠️ Lakini rekodi yao ya mechi za mwisho ni lazima itazamwe kwa jicho la tofauti
:
πŸ‘‰ Katika mechi 12 za mwisho, PMD FC wamepoteza mchezo mmoja na kutoka sare michezo mitatu.
:
🚨 6/10/2019: Al Jaish 2-2 Pyramid FC
🚨 14/09/2019: Pyramids FC 1-1 CR Belouizdad 🚨 8/09/2019: Zamalek 3-0 Pyramid FC
🚨 30/05/2019: Al Hadoud 1-1 Pyramid FC
:
πŸ‘‰ Kwenye msimu uliopita Pyramids hawakupoteza mchezo wowote katika uwanja wao wa nyumbani.
:
πŸ‘‰ Walishinda mechi 11 na kutoka sare mechi 6.
:
πŸ›‘ Pyramids ndio timu pekee msimu uliopita ambao hawakufungwa kabisa katika uwanja wao wa nyumbani kwenye ligi yao.
:
πŸ‘‰ Mpaka sasa Pyramids wameshinda mechi zote (2) walizocheza ugenini katika michuano ya Shirikisho

Neymar kufikisha michezo 100 timu ya taifa leo dhidi ya senegal

#

FIFAFriendlyMatch
πŸ‡§πŸ‡· Brasil vs Senegal πŸ‡ΈπŸ‡³
🏟 Singapore National Stadium
⏰ 9:00 mchana

Nyota wa Brazil, Neymar leo atakuwa anafikisha mchezo wa 100 akiwa na timu ya taifa ya Brazil; Goli 6⃣1⃣

Leo kuna uwezekano wa Neymar kuifikia rekodi ya Ronaldo Nazario mwenye mabao 62 ⚽ timu ya Brazil.

Wafungaji bora wa mda wote Brazil: ⚽
Pele 77
Ronaldo 62
Neymar 61
Romalio 55

Pitia #NyumbaYaMabingwa @mbet.co.tz ujiwekee mkeka wako mapema ili badae ukiwa unashuhudia mpira nyavuni unaingiza mtonyo mfukoni.

Design a site like this with WordPress.com
Get started