Kipchoge aweka hustoria katika vitabu

– Mkenya Eliud Kipchoge ameweka jina lake katika vitabu vya historia , akimaliza kilomita 42 za mbio za marathon kwa saa moja dakika 59 na sekunde 40 katika shindano la Ineos siku ya Jumamosi nchini Austria Vienna… Hatahivyo muda huo bora uliowekwa na bingwa huyo hautatambulika kama rekodi ya dunia.

– Kulingana Shirika la Riadha duniani IAAF , kwa mbio yoyote kufikia sheria zake na hivyobasi kutambulika kama rekodi ya dunia kuna masharti yanayopaswa kufuatwa kulingana na chombo cha habari cha AFP.
1️⃣ Kwanza mbio hizo lazima ziwe zimeandaliwa na shirika la riadha duniani IAAF ama shirikisho la raidha la nchini ambapo riadha hizo zinaandaliwa.
2️⃣ Wanariadha wanaodhibiti kasi hawawezi kuingia katika mbio hizo kwa zamu na kutoka.
3⃣ Lazima wanariadha wafanyiwe vipimo vya matumizi ya dawa za kusisimua mwili.
4⃣ Vinywaji vinapaswa kutoka kwa vituo rasmi na sio kupewa mwanariadha na wasimamizi wake.
5️⃣ Ni Sharti kuwepo zaidi ya washindani watatu katika mbio hizo.
6️⃣ Mwanariadha hafai kudhibitiwa kasi na gari lililopo mbele yake.
7️⃣ Njia itakayotumika ni sharti ifanyiwe ukaguzi na kupimwa na maafisa wa IAAF.

– Siku ya Jumamosi, Kipchoge alipewa vinywaji kila baada ya kilomita 5 na hivyobasi kukiuka sheria hizo za shirikisho la riadha duniani…. Kulingana na AFP , barabara hiyo ilikuwa imeandaliwa hali ya kwamba ingemchukua Kipchoge sekunde 4.5 zaidi kulingana na uchanganuzi wa wataalam wa michezo katika chuo kikuu cha Vienna.
Kwa jumla aliweza kushuka mita 26 na kupanda mita 12 , walisema wataalam hao.

Mbio hizo za Viena hazikuwa mashindano bali zililenga kuwapa motisha mamilioni ya watu duniani. Na Kipchoge amefanikiwa.
..
– Mkimbiaji huyo mwenye umri wa miaka 34 tayari anashikilia rekodi ya dunia miongoni mwa wanaume katika umbali huo akiwa na muda wa saa mbili dakika moja na sekunde 39, ambao aliweka katika mbio za Berlin tarehe 16 mwezi Septemba 2018.
#ELiud159 #NoHumanIsLimited #EliudKipchoge #IneosChallenge

YA SOKA JANA JUMAMOSI..

– EURO – Qualification:
FT Georgia 0 – 0 Ireland
FT Denmark 1 – 0 Switzerland
FT Faroe Islands 0 – 3 Romania
FT Malta 0 – 4 Sweden
FT Norway 1 – 1 Spain
FT Bosnia and Herzegovina 4 – 1 Finland
FT Italy 2 – 0 Greece
FT Liechtenstein 1 – 1 Armenia

– England – League 1
FT Blackpool 1 – 2 Rotherham United
FT Bristol Rovers 1 – 0 Milton Keynes Dons
FT Oxford United 3 – 0 Doncaster Rovers
FT Peterborough United 2 – 0 Lincoln City
FT Portsmouth 0 – 0 Gillingham
FT Rochdale 2 – 1 Accrington Stanley
FT Southend United 1 – 4 AFC Wimbledon

– Spain – LaLiga SmartBank
FT Girona 0 – 2 Elche
FT Sporting Gijon 1 – 3 Alcorcon
FT Almeria 0 – 0 Lugo
FT Malaga 1 – 2 Cadiz
FT Extremadura 1 – 1 Ponferradin

– International Friendly Match
FT Simba SC 1-0 Bandari FC
#results #SokaPlaceUpdates

Italia yafuzu EURO 2020

✅ 2-0 Finland
✅ 6-0 Liechtenstein
✅ 3-0 Greece
✅ 2-1 Bosnia and Herzegovina
✅ 3-1 Armenia
✅ 2-1 Finland
✅ 2-0 Greece

– Timu ya taifa ya Italia 🇮🇹 @Azzurri imefanikiwa kufuzu kucheza fainali za EURO 2020… Italia imeshinda michezo yao yote Saba ya kuwania kufuzu wakiwa Kundi J wanaliongoza kwa Point 21 na Magoli 20 ya Kufunga… Forza Azzurri 🇮🇹 👏👏.
🔥 Unstoppable.

Mambo yaliyojitokeza katika mechi ya simba vs badari fc

Mambo kadhaa niliyoyaona kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Simba dhidi ya Bandari Fc.
.
.
Nimeona utofauti mkubwa kati ya Wawa, na Santos, Wawa ni mzuri kwenye kupiga mpira mirefu kukaba ni tatizo kubwa kwake. Santos, anakaba kama ataendelea hivi hivi inaweza ikawa Chemistry bora ya msimu yeye na Nyoni 🙌.
.
.
Simba, walikuwa bora kwenye eneo la kiungo Shiboub, moja ya viungo bora waliyosajiliwa msimu huu miguu yake imejaa vitu vingi timu inapomuhitaji kushambulia unamkuta timu inapohitaji kukaba unamkuta what box to boxi midfielder 🙌.
.
.
Shamte Alli, leo alikuwa bora kufanya majukumu ya kushambulia leo mechi kwake ilikuwa bora. .
.
Beno Kakolonya, amefanya kazi nzuri sana eneo lake la goli kipa kuna save moja aliifanya nimekumbuka kama ya Juma Kaseja dhidi ya Sudan, pale Taifa.
.
.
Deo Kanda, anahitaji ajisamini kama anataka kuendana na kasi ya wachezaji wa Simba, amekosa maamuzi kwenye kutoa pasi za mwisho. Mabadiliko ya Rashid Juma, yalikuwa yana mafua sana .
.
.
Willson, wa Bandari, moja ya wachezaji wazuri watulivu mabeki wa Simba, walikuwa wana mchunga sana huenda ikawa sio mgeni kwao 🙌 .
.
.
Yule beki wa pembeni wa Bandari Fc, ni mzuri sana anajua majukumu yake uchezaji wake hauna utofauti na Shabalala, ila yeye anakupa vitu viwili kwa wakati moja kushambulia na kukaba. .
.
Kipindi cha Pili Simba, walivocheza bila ya Mshambuliaji, nimekupenda timu ya taifa ya Hispania, kwenye michuano ya Euro, walicheza bila ya mshambuliaji halisia wa kati.
.
.
Wilson Da Silva, tumpe mda anahitaji ajitume nje kuna Bocco,na Kagere.
.

@azizi_mtambo_15

Funnier fungia viwanja ligi kuu yaendelea

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi (Kamati ya saa 72) imezuia baadhi ya viwanja kutumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kutokana na kuwa na upungufu katika maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la kuchezea (pitch) na uzio wa ndani unaotenganisha wachezaji na washabiki (fence).

Viwanja hivyo ni Kinesi Bull (Dar es Salaam), Bandari (Dar es Salaam), Jamhuri (Morogoro), Namfua (Singida), na Mkwakwani (Tanga). .

Klabu ambazo timu zao zinatumia viwanja hivyo zimepewa nafasi ya kufanya marekebisho kipindi hiki ambacho Ligi zimepisha mechi za kirafiki za FIFA au kuchagua viwanja mbadala vyenye sifa.

Vilevile klabu zimekumbushwa kuwa kwa mujibu wa kanuni, zinapaswa kupeleka viwanjani gari ya wagonjwa badala ya gari yenye kitanda kwani kanuni ya 14(2) imetaja ambulance na si gari lolote.

“Wasimamizi wa mechi vituoni wanatakiwa kuhakikisha ambulance zinapokuwepo viwanjani kama ilivyoelekezwa kikanuni. Kama huduma ya ambulance haitokuwepo wanatakiwa kuzuia mechi kuchezwa”, imeeleza taarifa iliyotolewa na kamati hiyo

David liuz aitembelea Rwanda

Beki wa Arsenal, David Luiz, ametua Rwanda kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni sehemu ya ushirika uliopo kati ya Arsenal na nchi hiyo kupitia Shirika la Ndege la Rwanda.

Luiz ambaye alitua Arsenal akitokea Chelsea amesema anajivunia kufanya ziara hiyo nchini Rwanda.

“Nimewahi kusikia mambo mazuri kuhusu Rwanda, nina furaha kubwa pia kuiwakilisha klabu yangu (Arsenal), hakika nitajifunza mengi na kuisaidia jamii kwa ujumla,” amesema beki huyo.

Ziara kama hiyo ilishawahi kufanywa na mkongwe wa Chelsea, Didier Drogba.

Mo akumbuka tukio la.kutekwa

Juzi Ijumaa Oktoba 11 2019 umetimia mwaka mmoja tangu tukio la kutekwa Mwekezaji wa klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji ‘Mo’ liitikise nchi

Mo amesema tukio hilo hatalisahau kamwe kwani katika kipindi chote alichokuwa akishikiliwa, aliishi bila ya kuwa na uhakika wa kuiona kesho yake

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Mo ameandika ujumbe huu;

“Mwaka mmoja uliopita siku kama ya leo nilitekwa. Siku 9 nilizofungwa macho na mikono kilikuwa ni kitendo cha mateso zaidi kwenye maisha yangu yote”

“Kutokuwa na uhakika wa kuona dakika inayofata nikiwa hai ilikua ni hali ya kutisha, lakini nashukuru Mwenyezi Mungu, na sala za wengi, nilivuka shida zote”

“Kurudi kwangu salama ndio ushuhuda wa kweli wa nguvu ya maombi”

“Nilibarikiwa kwa kupewa nafasi ya pili ya maisha. Asanteni Watanzania wenzangu wote na kila mtu duniani kote kwa maombi yenu na msaada usio na shaka”

“Mwenyezi Mtukufu awasimamie katika mambo yenu kwa upendeleo mkubwa! Ameen”

Timu ya walemavu tanzania yafuzu kombe la dunia

Licha ya kupoteza mchezo wa kutafuta nafasi ya mshindi wa tatu ikifungwa magoli 2-1 na Liberia katika mashindano ya Afrika, bado Timu ya taifa ya Tanzania ya mpira wa miguu kwa wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’, imefanikiwa kufuzu kuliwakilisha bara la Afrika katika michuano ya kombe la Dunia litakalofanyika kati ya Uingereza au Costa Rica mwaka 2022.

Tembo Warriors imefanikiwa kupata nafasi hiyo ikiwa ni kati ya timu 4, nyingine zikiwa ni Liberia (washindi wa tatu), Nigeria (washindi wa pili) na Angola ambao wamekuwa mabingwa wa Afrika wa mashindano hayo.

Ikumbukwe kwamba hii ilikua ni mara ya kwanza kwa Tanzania kushiriki mashindano makubwa ya kimataifa kama haya ikiwa inatimiza pia mwaka mmoja pekee tangu kuundwa kwa shirikisho linalosimamia mchezo huo hapa nchini.

Bado nchi rasmi itakayokuwa mwenyeji wa mashindao hayo haijatajwa huku Uingereza na Costa Rica zikipewa nafasi kubwa.

Yanga yataja sababu za kuipeleka pyramids mwanza

Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amesema wameuchagua uwanja wa CCM Kirumba kuutumia mechi dhidi ya Pyramids Fc baada ya kujiridhisha unakidhi vigezo

Aidha Mwakalebela amesema Yanga inakabiliwa na mchezo wa ligi kuu mkoani Mwanza dhidi ya Mbao Fc hivyo wanaamini watakuwa na muda wa kujiandaa mkoani pamoja na kuzoea uwanja

“Tutakuwa Mwanza kwa ajili ya mchezo wa ligi, hivyo Kamati ya Utendaji ikaona ni vyema mchezo dhidi ya Pyramids Fc tuupeleke huko kwani itaturahisishia maandalizi yetu,” amesema

“Lakini tutakuwa na muda wa kutosha kuutumia na kuuzoea uwanja wa CCM Kirumba kabla ya kuwakabili Pyramids Oktoba 27”

“Muhimu zaidi tunawapa nafasi wakazi wa jiji la Mwanza na mikoa ya jirani kushuhudia mchezo wa Kimataifa baada ya kukosa burudani hiyo kwa miaka kadhaa”

Yanga inatarajiwa kuweka kambi ya wiki moja jijini Mwanza kabla ya mchezo huo

Aidha, mabingwa hao wa kihistoria watautumia mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbao Fc ambao utapigwa Oktoba 24 kama sehemu ya maandalizi yao

Design a site like this with WordPress.com
Get started