Kakolanya ,ajibu hawakukosea njia

Mlinda lango namba mbili wa Simba Beno Kakolanya na kiungo Ibrahim Ajib jana walin’gara kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Bandari Fc, mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa

Wakati Kakolanya akiokoa michomo ya hatari, Ajib alifunga bao pekee ambalo liliihakikishia Simba ushindi muhimu wa bao 1-0

Mwanzoni wapo waliokosoa ujio wa wachezaji hao Msimbazi lakini sasa hakuna mwenye mashaka

Beno na Ajib walin’gara wakati wakiwa Yanga, hakuna shaka wataendeleza moto huo Msimbazi

Ajib ameanza kuonyesha makali yake baada ya kupona majeraha yaliyomuweka nje mwanzoni mwa msimu

Beno amekuwa bora kila anapopewa nafasi, ataendelea kumpa changamoto Aishi Manula ambaye bado ndiye kipa namba moja wa Simba

Belgium kuweka.historia mpya ulaya

#Euro2020Qualifiers live kupitia Startimes

Khazakstan 🇰🇿 vs 🇧🇪 Belgium
⏰ 10:00 jioni
🏟 Astana Arena
📺 ST World Football

Belgium tayari wameshafuzu Fainali za Euro 2020, wanatafuta rekodi ya kushinda mechi zote za kufuzu. Mpaka sasa Belgium wamecheza mechi saba wameshinda mechi zote 7, wakifunga goli 21 na kuruhusu goli 1 tu.

Belgium wameshinda mechi zote tatu zilizopita walipokutana na Khazakistan;

Belgium 3-0 ✅
Belgium 4-1 ✅
*Belgium 2-0 (ugenini) ✅

Mechi hii utaipata kupitia Startimes channeli ya World Football, pia waweza angalia kupitia App 📱 cheki link kwenye bio ya @startimestz

#MpangoniSoka
#StartimesPekee

Claudio Ranieri apata kandarasi.mpya

✍🏻 Kocha wa zamani wa Chelsea na Leicester City, Claudio Ranieri ameteuliwa kuwa kocha Mkuu Mpya wa klabu ya Sampdoria… Ranieri anachukua nafasi ya Eusebio di Francesco, ambaye alitimuliwa Jumatatu na kuiacha klabu hiyo ikiburuza mkia katika msimamo wa Serie A baada ya kufungwa mara sita kwenye mechi saba.

✍🏻 Ranieri mwenye miaka 67 pia alichukua mikoba ya Di Francesco huko Roma mnamo Machi kwa mkataba hadi mwisho wa msimu uliopita… Hivyo wanapokezana tu Vibarua 😄😄… Ranieri huu Ni Uteuzi wake wa 20 katika Vilabu tisa kama kocha Mkuu, Ikumbukwe AS Roma kaifundisha mara mbili tofauti.

✍🏻 Ranieri ambaye alianza kazi ya Ukocha Daraja la chiniii kabisa nchini Italia 🇮🇹 miaka ya 1980s, Anaifundisha Sampdoria ikiwa ni klabu yake ya Nane ya Ligi Kuu nchini kwao baada ya Kupita Vilabu Saba tofauti (Fiorentina, Juventus, AS Roma, Napoli, Cagliari, Inter Milan na Parma)…Mchezo wa kwanza wa Ranieri ambao Atawongoza washindi wa Serie A mwaka 1991, itakuwa ni nyumbani dhidi ya timu yake ya zamani, AS Roma siku ya Jumapili, 20 Oktoba.
#transfersUpdates #TransfersNews
@Harunlugoyah

Claudio Ranieri apata kandarasi.mpya

✍🏻 Kocha wa zamani wa Chelsea na Leicester City, Claudio Ranieri ameteuliwa kuwa kocha Mkuu Mpya wa klabu ya Sampdoria… Ranieri anachukua nafasi ya Eusebio di Francesco, ambaye alitimuliwa Jumatatu na kuiacha klabu hiyo ikiburuza mkia katika msimamo wa Serie A baada ya kufungwa mara sita kwenye mechi saba.

✍🏻 Ranieri mwenye miaka 67 pia alichukua mikoba ya Di Francesco huko Roma mnamo Machi kwa mkataba hadi mwisho wa msimu uliopita… Hivyo wanapokezana tu Vibarua 😄😄… Ranieri huu Ni Uteuzi wake wa 20 katika Vilabu tisa kama kocha Mkuu, Ikumbukwe AS Roma kaifundisha mara mbili tofauti.

✍🏻 Ranieri ambaye alianza kazi ya Ukocha Daraja la chiniii kabisa nchini Italia 🇮🇹 miaka ya 1980s, Anaifundisha Sampdoria ikiwa ni klabu yake ya Nane ya Ligi Kuu nchini kwao baada ya Kupita Vilabu Saba tofauti (Fiorentina, Juventus, AS Roma, Napoli, Cagliari, Inter Milan na Parma)…Mchezo wa kwanza wa Ranieri ambao Atawongoza washindi wa Serie A mwaka 1991, itakuwa ni nyumbani dhidi ya timu yake ya zamani, AS Roma siku ya Jumapili, 20 Oktoba.
#transfersUpdates #TransfersNews
@Harunlugoyah

Mtoto wa etoo aitwa kikosi cha taifa cameroon

– Mtoto wa mcheza soka wa zamani Samuel Eto’o, Etienne Eto’o Pineda ameitwa katika kikosi cha kwanza cha timu ya taifa ya Cameroon kwa vijana wa U17 kwa Ajili ya kushiriki Fainali za vijana za Kombe la Dunia la U17 huko Brazil mwishoni mwa Mwezi huu.

– Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 alistahili pia kuichezea Hispania, ambako alizaliwa, lakini sasa kakubali kujitolea kuichezea nchi ya baba yake ya Cameroon 🇨🇲… Mwanzo hakuwa sehemu ya kikosi kilichoshinda Kombe la Mataifa ya Afrika chini ya miaka 17 nchini Tanzania mapema mwaka, Ubingwa uliowafanya kufuzu Kombe la Dunia ambalo litaanza Oktoba 26.
..
– Mshambuliaji huyo kwa sasa ni nahodha wa Kikosi cha chini ya miaka 17 katika klabu cha Hispania, Mallorca, moja ya klabu ya zamani baba yake… Samuel Eto’o, ambaye alistaafu kucheza mpira wa miguu mapema mwezi huu, aliichezea Cameroon chini ya miaka 17 lakini pia alikuwa sehemu ya timu ya taifa ya Wakubwa kabla ya kitimiza miaka yake 17 tangu kuzaliwa.

– Kwenye Michuano yao ya Pili ya Dunia, Camaroon watacheza dhidi ya Argentina, Hispania na Tajikistan kwenye Kundi E huko Brazil… Mara yao ya mwisho kwenye Kombe la Dunia mnamo mwaka 2003 huko Finland, Cameroon iliishia hatua ya Makundi..
#U17FIFAWC #FIFAWC #FIFAU17WorldCup
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started