Ubaguzi uwanjani ..mechi yasimamishwa Mara mbili

✍🏻 Mchezo wa kuwania kufuzu kucheza Michuano ya EURO 2020, kati ya England dhdiya Bulgaria ulisimamishwa mara kadhaa kwani mashabiki walionywa juu ya tabia ya ubaguzi wa rangi kwa Wachezaji weusi, hasa wakielekezewa Raheem Sterling na Troy Mings wote wa England, Ubaguzi huo pia ulionesha pamoja na Saluti za Nazi na kuimbwa kwa milio ya tumbili… Game ililazimika kusimama mara ya kwanza dakika ya 28 huku England ikiongoza 2-0.
..
✍🏻 Tangazo la ndani ya uwanja lililaani Vitendo hivyo hiyo kabla ya kusema mechi ingehairishwa kucheza ikiwa tabia hiyo itaendelea… Mchezo huo ulisitishwa tena dakika ya 43 kabla ya kuanza tena baada ya majadiliano kati ya mwamuzi na meneja wa England, Gareth Southgate… England ilimaliza mchezo kwa kushinda 6-0 Na Kuendelea kuwa kinara wa Kundi A…. (Nazi Salutes – Maana yake nitakupa baadaye kidogo 🙌)..
#England #EURO2020Qualifiers
@Harunlugoyah

Neymar kukaa nje ya ndimba kwa wiki Nne

✍🏻 Neymar anatarajiwa kuwa nje kwa wiki Nne baada ya nyota huyo wa Paris Saint-Germain kupata jeraha akiitumikia timu yake ya taifa ya Brazil 🇧🇷… Klabu ya Ligue 1 ilithibitisha katika taarifa yao kuwa Mbrazil huyo atafanyiwa vipimo na mashine ya Uchunguzi “MRI Scan”.

✍🏻 Tathmini itafanywa katika muda wa siku nane, lakini anatarajiwa kukosa kucheza mwezi mzima… Neymar alilazimika kutolewa baada ya dakika 12 tu ya sare ya 1-1 akiwa na Brazil wakicheza na Nigeria 🇳🇬 huko Singapore 🇸🇬, na nafasi yake ikachukuliwa na Phillipe Coutinho wa Bayern Munich… Kati ya Mechi anazotarajia kukosa Neymar ni dhidi ya Nice, Club Brugge (×2 H & A), Marseille, Dijon na dhidi ya Brest..
#neymar #Brazil #PSG
@Harunlugoyah

Alexis Sanchez kuka nje ya dimba miezi mitatu

✍🏻 Alexis Sanchez anatarajia kuwa nje ya uwanja hadi miezi mitatu kutokana na kupata jeraha la kifundo cha Mguu, kwa Mujibu wa Kocha wa Chile 🇨🇱, Reinaldo Rueda… Mshambuliaji huyo wa klabu ya Inter Milan, akiwa hapo kwa Mkopo akitokea Manchester United, aliumia katika kipindi cha pili cha mchezo Akilitumikia taifa lake la Chile 🇨🇱 dhidi ya Colombia 🇨🇴 siku ya Jumamosi, game iliyoisha kwa Suluhu..
..
✍🏻 Sanchez alijiunga na kikosi hicho cha kocha Antonio Conte kwa mkopo wa msimu mmoja tangu Mwezi Agosti na amefunga bao lale moja tu kwa Inter katika mechi nne, akipokea kadi nyekundu katika mchezo huo huo aliofunga dhidi ya Sampdoria mwezi uliopita..
#Sanchez #AlexisSanchez #Chile
@Harunlugoyah

@Cristiano Alifunga goli lake la kwanza miaka 1⃣7⃣ iliyopita

👑 @Cristiano Alifunga goli lake la kwanza miaka 1⃣7⃣ iliyopita akiwa Sporting CP ya kwao Ureno katika mechi dhidi ya Moreirense, mpaka sasa kafunga Magoli dhidi ya Wapinzani 153 tofauti, Magoli mengi zaidi dhidi ya Mpinzani mmoja ni dhidi ya Sevilla (27).

✍🏻 Cr7 ana hat-trick 54… Hatimae Usiku wa Jana wakipoteza mechi yao akiwa na Ureno anafunga goli linomfanya kufikisha idadi ya Magoli 7️⃣0️⃣0️⃣ katika Historia yake ya kucheza Soka kwenye mechi yake ya 9️⃣7️⃣4⃣.
….
✍🏻 Katika, Cristiano Ronaldo anakuwa Mchezaji wa Sita kufikisha idadi hiyo ya Magoli 700+ baada ya..
🇦🇹 Josef Bican – 805
🇧🇷 Pele – 779
🇧🇷 Romario – 748
🇭🇺 Puskas – 709
🇩🇪 Gerd Muller – 701
🆕 🇵🇹 Cristiano Ronaldo – 700
…..
✍🏻 🐐 @Cristiano Ronaldo:
🌍 @SelecaoPortugal
⚽ 95 Goals

🇮🇹 @JuventusFC
⚽ 32 Goals

🇪🇸 @RealMadrid
⚽ 450 Goals

🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 @ManUtd
⚽ 118 Goals

🇵🇹 @Sporting_CP ⚽ 5 Goals
🎉 700 Career Goals 🎉
#CristianoRonaldo
@Harunlugoyah

@England yatoa kipigo kikubwa kwa mara ya kwanza ugenuni

🔥 @England imefunga mabao 6⃣+ katika mchezo wa ugenini kwa mara ya kwanza tangu Nov 1984 (ushindi wa 8-0 dhidi ya Uturuki)… England wamefunga mabao 5+ katika michezo yao minne kati ya nane ya mwaka huu 2019 – Walifunga mabao 5+ katika mechi nne katika mechi zao 76 kwenye miaka sita iliyopita iliyojumuishwa (2013-2018)… Ushindi wao wa 6-0 vs Bulgaria 🇧🇬 jana, unawafanya kuwa na Aggregate ya magoli 17-0 katika mechi Nne tu dhidi yao..
….
✍🏻 Harry Kane amefunga mabao 9⃣ katika mechi zake tisa za mwisho kwa England… 🔥 Raheem Sterling ana magoli 7⃣ na Assist 5⃣ katika game zote za kuwania kufuzu kwa EURO 2020 🔥🔥… Magoli 9⃣ kati ya 1⃣1⃣ ya @England kafunga mwaka huu 💪…. Mwaka huu, Ross Barkley kafunga Magoli Manne katika game Sita kwa England, magoli yake yotee Matano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za EURO kwa taifa lake kafunga Ugenini tu..
⚽️ v San Marino (Sept 2015)
⚽️ v Lithuania (Oct 2015)
⚽️⚽️ v Montenegro (March 2019)
⚽️ v Bulgaria (Oct 2019)
…..
✍🏻 Baada ya ukame kwa taifa na Klabu, Marcus Rashford, Hatimae kafunga baada ya mechi 12 bila goli lolote kwa @ManUtd au @England, Goli lake la kwanza kwa England tangu afunge mara ya mwisho Oktoba 15,2018… England @UEFAEURO here we go!..👏👏.
#England #UEFAEURO #EURO2020Qualifiers
@Harunlugoyah

Yanga yapewa.mbinu kufuzu hatua ya makundi

Nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Amri Kiemba amesema njia pekee ya Yanga kutinga hatua ya makundi michuano ya kombe la Shirikisho, ni kuhakikisha wanapata ushindi mnono nyumbani

Oktoba 27 Yanga itashuka dimba la CCM Kirumba kumenyana na Pyramids Fc kutoka Misri ukiwa ni mchezo wa raundi ya kwanza kusaka nafasi ya kutinga hatua ya makundi

Kiemba amesema mara nyingi timu za Tanzania huwa zinapata matokeo dhidi ya timu za Kaskazini katika michezo inayopigwa nyumbani lakini matokeo hayo mebamba huwa hayazisaidii kwenye michezo ya ugenin

Aidha Kiemba amesema licha ya Pyramids Fc kuwa timu isikuwa na uzoefu wa michuano ya CAF hii ikiwa mara yao yakwanza kushiriki, bado itakuwa timu hatari kwa Yanga kutokana na uwekezaji mkubwa wa timu hiyo na ubora wa ligi yao

“Naiangalia mechi hiyo kwa namna nyingine. Kwa tofauti ya ligi ya Tanzania na Misri naona bado ni timu ngumu haijalishi tunacheza na timu gani. Tusiangalie historia ya timu tu, tuangalie pia historia ya ligi wanayocheza. Mechi haitakuwa rahisi,” amesema

“Mara nyingi timu za Tanzania zimekuwa na uwezo wa kupata matokeo hata kwa timu za Afrika ya Kaskazini (kwenye mechi za nyumbani) shida imekuwa mechi inapokuwa ugenini.”

“Tumeshindwa pia kupata magoli ya kutosha hapa nyumbani ili yazisaidie timu zetu ugenini. Ukishinda goli 1-0 nyumbani kwa timu za Kaskazini mwa Afrika unakuwa kama tayari umeshatoka.”

Historia fupi ya Rwanda🇷🇼 Vs Tanzania🇹🇿

Rwanda🇷🇼 Vs Tanzania🇹🇿
.
🏟stade Nyamirambo!.
⏰saa 1:00 usiku.
.
✍Tanzania🇹🇿 na Rwanda “Amavubi”🇷🇼 wamekutana mara 18 katika historia tangu mwaka 1998!.
.
✍Tanzania akishinda 6 Rwanda ameshinda michezo 7 na sare 5!..
.
✍Mechi ya kwanza kukutana ilikuwa mwaka 1998 wakatoka sare ya 2-2 katika mechi ya kirafiki ya kimataifa.
.
✍kuanzia mwaka 2010 wamekutana mara 9 huku kila upande wakishinda 3 na sare 3!”wanawezana sana hawa!.
.
✍mara ya mwisho kukutana Tanzania alikufa 2-1 michuano ya Cecafa pale kenya!.
.
✍Mechi ya leo inaweza kuwa ya kisasi kwa Tanzania!ni vita kati ya wachezaji katika nafasi mbalimbali kwani wachezaji wengi wanajuana wamekuwa wakikutana katika michuano mbalimbali mfano Niyonzima,Kagere,Mkude,Nyoni,Domayo!.Hawa wamewahi kucheza klabu moja katika nyakati tofauti!.
.
🗣mechi za mwisho za Rwanda hivi karibuni.🇷🇼
🏟Mechi 5.
✔kushinda 2.
🤝sare 0.
❌kufungwa 3.
🥅magoli ya kufungwa 6.
⚽magoli ya kufunga 11(Hatari zaidi katika kushambulia).
.
TANZANIA🇹🇿
🏟mechi 5
✔kushinda 0.
🤝Sare 1.
❌kupoteza 4.
🥅magoli ya kufungwa 10.
⚽magoli ya kufunga 3.
.
✍Tanzania ina wastani mbaya katika ulinzi na ushambuliaji pia ukilinganisha na Rwanda!.Lolote linawezekana kutokea mpira wa Afrika ni uleule!.
.
.
Prepared by @anode360 Powered by @mcheza_tz @bussi_ntua @tshombee1 #sokaonlineupdates

Mwalim.jk nyerere ni shabiki wa yanga sc

KUMBE…!! Enzi za uhai wake, Rais wa Kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere alikuwa ni shabiki kipenzi wa Yanga SC.

Hii ni kwa mujibu wa Mwanasiasa mkongwe nchini Stephen Wasira wilayani Butiama katika kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Mwalimu Nyerere.

Wasira amefichua hilo baada ya kuulizwa swali na Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa mpenzi wa timu gani.

Powered by @upholstery_designsco ….. @yangasc @antonionugaz @dismasten @hbumbuli #TimuYaWananchi #NyerereDay #NyerereDay2019

Mwalim.jk nyerere ni shabiki wa yanga sc

KUMBE…!! Enzi za uhai wake, Rais wa Kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere alikuwa ni shabiki kipenzi wa Yanga SC.

Hii ni kwa mujibu wa Mwanasiasa mkongwe nchini Stephen Wasira wilayani Butiama katika kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Mwalimu Nyerere.

Wasira amefichua hilo baada ya kuulizwa swali na Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa mpenzi wa timu gani.

Powered by @upholstery_designsco ….. @yangasc @antonionugaz @dismasten @hbumbuli #TimuYaWananchi #NyerereDay #NyerereDay2019

Design a site like this with WordPress.com
Get started