
#Part1 – Miaka 4 ya Klopp: Safari ya Kuirudishia Liverpool Hadhi Yake.
.
.
Jumapili hii, Klopp na vijana wake wanaelekea Old Trafford kuumana na Manchester United, mtanange kileleni mwa msimu na uongozi wa points 8 mbele ya Manchester City wanaoshika nafasi ya pili.
Mechi hii ya Jumapili inaangukia katika wiki ambayo Klopp anatimiza miaka 4 na Liverpool, katika kipindi hicho amefanya mabadiliko makubwa katika klabu hii.
Klopp alimrithi Brendan Rodgers na kuanza kazi rasmi mnamo 17 October 2015, mchezo wake wa kwanza uliisha kwa sare ya 0-0 dhidi ya Tottenham- kwenye kikosi ambacho kilijaa vijana wengi wasiokuwa na uzoefu wa kutosha.
Katika wachezaji 18 walioitwa kwenye mchezo huo – ni wanne tu ambao wamebaki katika klabu – Adam Lallana, Divock Origi, James Milner na Nathaniel Clyne. Tangu wakati huo, Klopp ameibadilisha Liverpool, kuiongoza kutwaa Champions League na kuifanya kuwa timu inayopewa nafasi kubwa ya kutwaa uchampions wa nyumbani.
Kuelekea mchezo wa Jumapili, Klopp anaonyesha namna amefanya kazi kubwa kuifanya Liverpool kuwa klabu ya kuogopwa barani ulaya – hasa ukizingatia kikosi alichorithi kutoka kwa Brendan Rogers kilikuwa dhaifu kuliko kikosi alichorithi mpinzani wake wa Jumapili Ole Gunnar Solskjaer. Lakini alifanikiwa kuwapeleka fainali mbili katika msimu wa kwanza, na kuwawezesha kucheza Champions League katika kila msimu tangu wakati huo.
Klopp amefanikiwa kufanya usajili mzuri wa wachezaji wanaofit katika filosofia yake ya soka, wenye haiba nzuri yenye kutengeneza ushirikiano mzuri kwenye timu.
Kuna sababu nyingi Kwanini Liverpool wanafanikiwa – kuanzia kwenye uongozi wa juu mpaka kwenye benchi la ufundi – lakini ‘Klopp Man Manmanagement’ ni sababu kuu katika kuunda ngome ngumu ya Liverpool.
Msimu ambao Klopp alichukua mikoba ya Rogers, Liverpool walimaliza kwenye ligi katika nafasi ya 8, nyuma ya timu kama Soton na West Ham, timu ambazo hivi sasa zikisikia inakuja mechi na Liverpool zinajua vipigo vinakuja.
Kumekuwepo na matokeo ya kuwarudisha nyuma kama Fainali ya Europe League 2016, kuondokewa na baadhi ya wachezaji muhimu kama Coutinho – lakini chini ya uongozi wa Klopp, Liverpool imeendelea kuimarika.
•••••••••INAENDELEA••••