Siumizwi ma.matokeo ya are asema. Aussems

Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema timu yake haikuwa ikiangalia matokeo zaidi kwenye michezo ya kirafiki waliyocheza jijini Dar es salaam na mkoani Kigoma

Simba ilianza kwa kuichapa Bandari Fc bao 1-0 jijini Dar es salaam kisha kuelekea mkoani Kigoma ambako ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mashujaa Fc kisha kulazimishwa suluhu ya bila kufungana na Aigle Noir

“Matokeo yalikuwa jambo la mwisho kwenye mechi zetu za kirafiki,” amesema

“Muhimu tulihitaji kuwapa wachezaji muda wa kucheza wakati huu ambao ligi imesimama”

Hata hivyo Aussems amekiri mazingira ya uwanja wa Lake Tangayika hayakuwa mazuri kwa timu yake kuweza kufanya vizuri

Jana baada ya mchezo dhidi ya Aigle Noir, beki Yusufu Mlipili alisema uwanja wa Lake Tanganyika uliwapa wakati mgumu kucheza kama walivyozoea

“Tulishindwa kabisa kucheza, uwanja lilikuwa tatizo. Lakini tunashukuru hatupoteza mchezo”

Simba inarejea jijini Dar es salaam kuendelea na maandalizi ya mchezo dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Oktoba 23

Alisson Becker arejea.kikosini livepool

Mlinda lango namba moja wa timu ya Liverpool, Alisson Becker, anatarajia kuwa kwenye kikosi cha timu hiyo kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Manchester United baada ya kuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili.

Kipa huyo raia wa nchini Brazil, alipata majeruhi kwenye mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa michuano ya Ligi Kuu England dhidi ya Norwich kwenye uwanja wa Old Trafford. Aliumia nyama za paja dakika ya 37.

Kocha wa timu ya Liverpool, Jurgen Klopp, ameweka wazi kwamba, alikuwa na nafasi ya kumchezesha kipa huyo kwenye mchezo dhidi ya Leicester City, ila alihofia hali yake, hivyo aliamua kumuacha afanye mazoezi kwa ajili ya mchezo wa mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Manchester United.

Kipa huyo alijiunga na Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 64.6, wakati wa uhamisho wa kiangazi 2018 akitokea klabu ya AS Roma. Tangu ajiunge na timu hiyo amekuwa na mchango mkubwa wa mafanikio ikiwa pamoja na kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Hata hivyo, Liverpool haijapoteza mchezo kwenye michuano ya Ligi Kuu England tangu kuanza kwa msimu huu japokuwa kipa huyo alikuwa nje ya uwanja huku nafasi yake ikichukuliwa na Adrian Castillo, raia wa nchini Hispania.

Kwenye msimamo wa Ligi, Liverpool wanaongoza wakiwa na jumla ya pointi 24 baada ya kucheza michezo nane, huku mabingwa watetezi Manchester City wakishika nafasi ya pili baada ya kuvuna pointi 16.

Mchezo huo ambao utapigwa Jumapili wiki hii, Manchester United watakuwa kwenye uwanja wa nyumbani Old Trafford, ambapo United wanatakiwa kushinda ili kulinda kibarua cha kocha wao Ole Gunnar Solskjaer. Kwa sasa Manchester United wanashika nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi baada ya kushinda michezo miwili na kutoka sare mitatu na kupoteza mitatu.

Wafungaji Bora kwenye mashindano ya kufuzu Euro 2020: ⚽ •

🇮🇱 Eran Zahavi – 11
🇷🇺 Artem Dzyuba – 9
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Raheem Sterling – 8
🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Harry Kane – 8
🇫🇮 Teemu Pukki – 7
🇵🇹 Cristiano Ronaldo – 7
🇷🇸 Aleksandar Mitrovic – 7

Eran Zahavi kinara wa mabao kwenye Euro Qualifiers, anacheza katika klabu ya Guangzhou RF na timu ya taifa ya Israel

Rekodi ya Eran Zahavi Mwaka 2019 (Guangzhou R&F na Israel):
👕 Mechi 30
⚽️ Mabao 37

Massimiliano Allegri aanza kujifunza Kiingereza kisa Man United.

Massimiliano Allegri: “Ninaongea Kiingereza vibaya sana kwa sasa, lakini bado ninajifunza.”

Kocha huyu wa zamani wa Juventus na bigwa mara 6 wa ligi ya Italia hafichi matamanio yake ya kufanya kazi kwenye Ligi ya EPL na anahusishwa kujiunga na Manchester United kuchukua nafasi ya Ole Gunnar Solskjer.

Klabu ya Anderlecht imepigwa faini ya £4,315 na shirikisho la soka la Ubelgiji

Klabu ya Anderlecht imepigwa faini ya £4,315 na shirikisho la soka la Ubelgiji kwa kumteua Vincent Kompany kama kocha mkuu wakati hana vigezo.

Beki huyo wa zamani wa Man City alipewa nafasi ya kuwa kocha mchezaji mwezi Mei lakini sasa uamuzi umerudi kuiburuta klabu yake ya Anderlecht baada ya kumpa majukumu kama kocha mkuu.

FA ya Ubelgiji inahitaji makocha wote wakuu kuwa na leseni ya UEFA Pro, na imebainika Kompany hana leseni hiyo.

Kompany amefanikiwa kupata ushindi mara mbili katika michezo kumi tangu alipochaguliwa kuwa kocha wa Anderlecht, huku ikishika nafasi ya 13 katika ligi anayocheza @samagoal77 (Belgium Pro League)

Zamalek wachezaji sasa hakuna kutumia mitandao ya kijamii

Raisi wa klabu ya Zamalek, Mortada Mansour ameongeza sheria mpya katika utawala wake, kwa kuwapiga marufuku wachezaji wa klabu hiyo kutumia mitandano ya kijamii.

Raisi huyo wa Zamalek ambaye pia ni mbobezi wa maswala ya sheria, amepiga marufuku ya mitandao ya kijamii kwa kuamini wachezaji wengine wamekua wakipoteza muda mwingi kwa matumizi ya simu.

Mchezaji yeyote wa Zamalek atakayebainika anamiliki akaunti ya kijamii atakatwa nusu ya mshahara wake, huku kukiwa na faini ya dola 18,00 za kimarekani kwa kila post itakayowekwa na mchezaji kwenye mtandao wa kijamii.

Mitandao ya kijamii inaonekana kuwa na athari kubwa kwa wachezaji kwani si Afrika pekee bali hata England, meneja wa Man City Pep Guardiola amekuwa mpingaji mkubwa wa matumizi ya simu kwa wachezaji na aliitambulisha sheria mpya (2018).

Guardiola 🗣”Ni marufuku kutumia simu katika eneo la Gym na sehemu ya kuchezea ya uwanja wa mazoezi (City Football Academy).”

Ghana yatwaa kombe la. Dunia.mbele.ya brazil

ON THIS DAY: Mnamo mwaka wa 2009, Timu ya taifa Ghana 🇬🇭 iliichalaza timu ya taifa ya Brazil kwa Mikwaju ya Penati 4⃣ – 3⃣ na kushinda Kombe la Dunia la Vijana walio chini ya umri wa miaka 20 huko nchini Misri.

– Ghana 🇬🇭 hawakupoteza game hata moja katika kundi lao D na Brazil 🇧🇷 hawakupoteza game yao yoyote katika Kundi E (WWD), Ghana walishinda mechi mbili (2-1 vs Uzbekistan 🇺🇿 & 4-0 vs England) na kutoka sare game moja (2-2 vs Uruguay)..
..
– Mtoano Ghana ilishinda 2-1 vs Afrika Kusini 🇿🇦, Robo fainali ikashinda 3-2 vs Korea Kusini 🇰🇷 na Nusu Fainali ikashinda tena 3-2 vs Hungary 🇭🇺 na kutinga fainal iliyomalizika kwa Suluhu dakika 120 kabla ya Penati kuamua Bingwa..
….
✍🏻 Hadi leo, Ghana 🇬🇭 ndio taifa la kwanza na la pekee kutoka Afrika kushinda mashindano hayo ya Dunia… Wapo wapi wachezaji waliotwaa Ubingwa huo?! 🇬🇭
#Ghana #U20WC #FIFAU20WC
@Harunlugoyah

Paul Pogba na David de Gea kuikosa livepool.

✍🏻 Ole Gunnar Solskjaer amethibitisha kwamba kiungo, Paul Pogba na mlinda lango, David de Gea watakosa kuitumikia klabu yao ya Manchester United katika mechi yao dhidi ya Liverpool siku Jumapili katika Muendelezo wa Premier League.

✍🏻 De Gea alitolewa baada ya kupata majeraha wakati Akiitumikia timu yake ya taifa ya Hispania katika mechi ya kuwania kufuzu EURO 2020 dhidi ya Sweden jana Jumanne, Wakati huo huo, Pogba, amekosa mechi tano zilizopita za United kutokana na jeraha la kifundo cha Mguu “Ankle”… Kwasasa Mfaransa huyo yupo Dubai akiendelea kupona “Mdogo mdogo”.
#PremierLeague #ManUtd
@Harunlugoyah

Paul Pogba na David de Gea kuikosa livepool.

✍🏻 Ole Gunnar Solskjaer amethibitisha kwamba kiungo, Paul Pogba na mlinda lango, David de Gea watakosa kuitumikia klabu yao ya Manchester United katika mechi yao dhidi ya Liverpool siku Jumapili katika Muendelezo wa Premier League.

✍🏻 De Gea alitolewa baada ya kupata majeraha wakati Akiitumikia timu yake ya taifa ya Hispania katika mechi ya kuwania kufuzu EURO 2020 dhidi ya Sweden jana Jumanne, Wakati huo huo, Pogba, amekosa mechi tano zilizopita za United kutokana na jeraha la kifundo cha Mguu “Ankle”… Kwasasa Mfaransa huyo yupo Dubai akiendelea kupona “Mdogo mdogo”.
#PremierLeague #ManUtd
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started