Aussems-mchezo wetu na azam si rahisi

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems amesema mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC hautakuwa rahisi, anaamini Azam ni moja ya timu bora Tanzania.

Simba na Azam Fc zitacheza Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwa ni mara ya pili msimu huu baada ya kukutana kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii na Simba kushinda 4-2.

Aussems amesema anawaheshimu Azam Fc kwani wana timu nzuri kwa sasa lakini malengo ya kikosi chake ni kushinda mchezo huo

“Niliwaona Azam FC tangu msimu uliopita ni miongoni mwa timu nzuri za Tanzania, katika mpira hakuna mchezo rahisi, lakini tunajiandaa kupata matokeo mazuri tukijua ni wapinzani wa aina gani”

Simba ilitumia vyema mapumziko wa kalenda ya Fifa katika kujiimarisha kwa michezo mitatu ya kirafiki ambapo walishinda miwili na kupata sare moja.

Manchester City yarejea kwa kishindo EPL

Manchester City imerejea kibabe kutoka mapumziko ya michezo ya Kimataifa baada ya kuifumua timu ngumu ya Crystal Palace mabao 2-0

Mabao ya Gabriel Jesus na David Silva yalitosha kuihakikishia City ushindi muhimu ambao umeopunguza tofauti ya pointi baina yao na vinara Liverpool kuwa tano

Liverpool itashuka dimba la Old Trafford kuikabili Manchester United leo katika mchezo ambao Liverpool inapewa nafasi ya kuendeleza wimbi la ushindi kwenye ligi hiyo

Manchester City jana ilicheza bila mlinzi wa kati asili ikiwatumia viungo Rodri na Fernadihno kama walinzi wa kati kutokana na kukabiliwa na wimbi la majeruhi

Aidha Nicholas Otamendi alichelewa kurejea kutoka Argentina alikokwenda kutimiza majukumu ya timu ya Taifa

Raheem Sterling. Kupata shavu.manchester city

Klabu ya Manchester City ipo kwenye mipango ya kumuongezea mkataba mpya wenye ofa nono nyota wake Raheem Sterling ili kumzuia asitimkie kwenye vilabu vya Real Madrid pamoja na Barcelona ambavyo vimeonyesha nia ya kumhitaji
. .
Kwa mujibu wa Daily Express Inasemekana Man City inataka kumfanya Sterling awe mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi kuliko mchezaji yeyote katika Premier League.
.
.
Powered by @mcheza_tz @bussi_ntua @tshombee1 #sokaonlineupdates

Kiungo wa Real Madrid kukutana na Perez

Kiungo wa Real Madrid Dani Ceballos ambaye anakipiga Arsenal kwa mkopo atarajia kukutana na Rais wa Madrid Florentino Perez ili kujadiliana kuhusiana na mustakabali wake ndani ya klabu hiyo
. .
Kwa mujibu wa DAILY STAR ON SUNDAY Ceballos hayupo tayari kurejea Real Madrid hivyo anataka auzwe moja kwa moja kwa washika bunduki hao wa London
. .
Powered by @mcheza_tz @bussi_ntua @tshombee1 #sokaonlineupdates

Ni Wachezaji wawili tu ambao wapo mpaka Sasa ndani ya Kikosi Chelsea

👉 Ni Wachezaji wawili tu ambao wapo mpaka Sasa ndani ya Kikosi Chelsea, wamefunga Magoli mengi zaidi ya Premier League kumzidi Marcos Alonso tangu kuanza kwa msimu wa 2016/17:
🇪🇸 Pedro (21)
🇧🇷 Willian (18)
🇪🇸 Marcos Alonso (16)

😳 Alonso ni Beki 🙌🙄
#chelseafc #PremierLeague

Ronaldo aendeleza kasi ya ufungaji

– Cristiano Ronaldo sasa kafunga katika mechi zake Sita kati ya Saba alizocheza kwa Klabu yake ya @juventus 🇮🇹 na timu yake ya taifa ya @portugal 🇵🇹:
….
⚽️ vs. Hellas Verona
⚽️ vs. SPAL
⚽️ vs. Bayer Leverkusen
❌ vs. Inter Milan
⚽️ vs. Luxembourg
⚽️ vs. Ukraine
⚽️ vs. Bologna

701 goals and counting. 💫
#CristianoRonaldo #Juventus #Portugal
@Harunlugoyah

Madrid yaendelea.kula.vipigo

jana usiku Real Madrid ilishindwa kutamba mbele na Mallorca baada ya kuchapwa bao 1-0

Hicho ni kipigo cha kwanza kwa Real Madrid msimu huu awali ikiwa imecheza mechi nane bila ya kupotea mchezo

Lago Junior alifunga bao pekee la Mallorca kwenye mchezo huo

Mapema Fc Barcelona iliichapa Eibar mabao 3-0 na kukwea kileleni mwa msimamo wa ligi kwa mara ya kwanza msimu huu

Mabao ya Antoine Griezmann, Luis Suarez na Lionel Messi yaliihakikishia Barca ushindi huo muhimu

Atletico Madrid na Valencia zilitoshana nguvu baada ya kutoka sare ya bao 1-1

VAR yainusuru spurs kipigo

Pepo mbaya ameendelea kuzengea kibarua cha Mkufunzi wa Tottenham Hotspurs Mauricio Pochettino baada ya timu yake jana kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Watford

Spurs nusura ipoteze mchezo wa tatu mfululizo kwenye uwanja wake wa nyumbani kama bao la Delle Alli lingekataliwa

Kiungo huyo alifunga bao kwenye dakika ya 86, hata hivyo mwamuzi alilazimika kutumia usaidizi wa VAR baada ya Delle kuonekana kama kautuliza mpira na sehemu ya mkono wake kabla ya kufunga

Pamoja na bao hilo kukubaliwa, ‘screen’ ya VAR ilionyesha bao hilo limekataliwa tukio lililoibua sintofahamu kwa muda mfupi

Kampuni ya Hawk-Eye iliyotoa vifaa vya VAR iliomba radhi kutokana na mkanganyiko huo

Baada ya kufungwa mabao 7-1 na Bayern Munich kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa, upepo wa ‘kisulisuli’ unaonekana kuipitia Spurs kwani bado inaonekana kuweweseka kutokana na kipigo hicho

Kwani tangu wakati huo haijaweza kushinda ikiambulia sare hiyo jana

Kumekuwa na tetesi kuwa Pochettino anaweza kuondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Jose Mourinho

Design a site like this with WordPress.com
Get started