
📅 TAREHE NA MWEZI KAMA WA LEO, MNAMO MWAKA 2013.. Ilipigwa Mechi ya Watani wa Jadi Nchini Simba SC dhidi ya Yanga SC, Game ambayo ni miongoni mwa mechi isiyosahaulika katika historia ya Miamba hawa.
.
– Ilikuwa ni Dakika ya 15 tu, Mrisho Ngassa aliyekuwa kipenzi cha Wananchi, anaifungia Yanga bao la kwanza baada ya kuiwahi krosi ya Mshambuliaji hatari wa Burundi 🇧🇮, Didier Kavumbagu…Yanga waliaanza mchezo kwa pasi za uhakika huku wakiwapa Simba taabu mno hasa eneo la kiungo likiongozwa nao Niyonzima, Domayo & Chuji.. Ilikuwa ni Dakika ya 36 ya mchezo, Mshambuliaji wa Uganda 🇺🇬, Hamis Kiiza “Diego” anaifungia Yanga SC bao la pili baada ya beki Wa Simba, Haruna Shamte “Terminator” kujichanganya mpira wa kurusha wa Mbuyu Twite ulioguswa na Didier Kavumbagu kwa kichwa.
.
– Mda mchache kabla ya Mapumziko Show game ilianza kwa Wananchi wakiamini game imeisha hii, Walikalia mpira na madoido kibao 😂😂, huku wale wa Simba wakianza kutoka uwanjani, MNAMO dakika ya 45, Yule yule Kiiza Diego anaifungia Yanga bao la tatu baada ya Kavumbagu kugongeana vizuri na kiungo wa Rwanda 🇷🇼, Haruna Niyonzima..
👉 HALF-TIME: Yanga SC 3-0 Simba SC
[Kiiza ⚽⚽, Ngassa ⚽].
.
– Simba wanaonekana kupoteana huku Yanga wakishambulia na kupoteza nafasi nyingi za Magoli… Ilikuwa dakika ya 53, Mshambuliaji, Betram Mwombeki anaipatia Simba SC bao la kwanza baada ya pasi ya Mshambuliaji wa Burundi 🇧🇮, Amis Tambwe…Simba wanaonekana kubadilika kipindi cha pili baada ya kuwatoa Humud na Haruna Chanongo kisha kuwaingiza chipukizi, William Gallas na Said Ndemla ambaye alikuja kuubonda mwingi Mno… Mnamo dakika ya 57, Simba wanafumania nyavu za Yanga kwa mara ya pili goli likifungwa nae Joseph Owino baada ya kuunganisha vizuri mpira wa kona wa Ramadhan Singano “Messi” wakati mabeki wa Yanga wakiwa wamezubaa.. Dakika ya 64, Ngassa anawatoka Mabeki Owino na Kaze, anabaki yeye na kipa, lakini anakosa goli la waziii baada ya kipa kuokoa…. Dakika ya 84, Beki wa Kimataifa wa Burundi 🇧🇮, Gilbert Kaze anawainua wana Simba waliokata tamaa kwa kufunga goli kwa Kichwa akiungamisha krosi ya faulo ya Nahodha, Masoud Nassor “Chollo”..
…
FULL-TIME 💓 3⃣ – 3⃣ 💛
#SimbaSC #YangaSC
@Harunlugoyah





