FRAGA NA KAKOLANYA WAZUNGUMZIA MECHI DHIDI YA AZAM

Kiungo mkata umeme Gerson Fraga amesema anatambua Azam Fc ni moja ya timu bora kwenye ligi msimu lakini wao hesabu zao ni kuhakikisha wanashinda Jumatano

Simba na Azam Fc zitakutana Jumatano kwenye mchezo wa ligi kuu ambao utapigwa uwanja wa Taifa

Akizungumza jana jioni baada ya mazoezi ya Simba yaliyofanyika uwanja wa Uhuru, Fraga alisema anawasubiri Azam Fc kwa hamu

“Azam Fc wana timu nzuri sana tunafahamu, lakini tunafanya maandalizi kabambe ili kuhakikisha tunshinda mchezo huo”

“Tumeusubiri sana mchezo huu ili tuendelee kuwapa furaha mashabiki wetu,” amesema

Nae mlinda lango Beno Kakolanya ambaye alidaka katika mchezo wa Ngao ya Jamii amesema pamoja na Simba kuibuka na udhindi kwenye mchezo huo, Azam Fc walitoa upinzani mkali hivyo wanapaswa kujiandaa kikamilifu ili kuhakikisha wanashinda tena Jumatano

STARS YATIBUA ULAJI KOCHA SUDAN

ZDRAVKO Logarusic raia wa Crotia
ambaye ni Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Sudan hali ni tete kwenye benchi la ufundi kutokana na kushindwa kutimiza lengo la kwenye mkataba la kuhakikisha anafuzu fainali za Chan.

Stars imeongeza ugumu kwa bosi huyo kuitwa mezani tena kutokana na kupindua meza kibabe kwa ushindi wa mabao 2-1
na kufanya idadi ya mabao kuwa 2-2 na Stars kufuzu kwa faida ya bao la ugenini. Logarusic aliyejiunga na Sudan Desemba
2017, mkataba wake umefika ukingoni na inaelezwa kuwa mabosi walikuwa wanamsikilizia afuzu michuano ya Chan
ambayo inawahusisha wachezaji wa ndani kwa kuwa amechemsha basi kuna hatihati atapigwa chini mazima.
Logarusic muda mchache kabla ya
mchezo alisema kuwa ushindi wake mbele ya Tanzania ulikuwa umeshikilia mkataba wake mpya.

“Nimekaa na timu kwa muda mrefu na mkataba wangu kwa sasa upo ukingoni na hakuna dalili zozote ambazo mabosi
zangu wamezionyesha hivyo baada ya
mchezo dhidi ya Tanzania hatma yangu
itajulikana.
“Mpango wa kubaki huku sina uhakika kwa kuwa mimi ninaujua uwezo wangu na
ninatambua mbinu nyingi, sina mashaka endapo sitaongezewa mkataba ndani ya
timu ninayosimamia kwa sasa,” alisema Logarusic ambaye aliwahi kuikochi Simba.

#LikePageNewsUpdates

Rekodi zaiweka simba pazuri dhidi ya Azam

Katika misimu miwili iliyopita, Simba imeweka rekodi bora ya kufanya vizuri dhidi ya Azam Fc katika michezo iliyozikutanisha timu hizo kwenye ligi

Msimu uliopita Azam Fc iliambulia alama moja tu katika mchezo wa ligi kuu mzunguuko wa pili

Kwenye mchezo wa mzunguuko wa kwanza Azam Fc ilipokea kichapo cha mabao 3-1, mabao ya Meddie Kagere (2) na nahodha John Bocco huku lile la Azam likifungwa na Frank Domayo

Ushindi pekee iliyopata Azam dhidi ya Simba ni michuano ya Kagame na kombe la Mapinduzi ambayo Simba haikuwa imeipa kipaumbele

Msimu huu tayari Azam Fc wameshachezea kichapo cha mabao 4-2 kwenye mchezo wa ufunguzi wa msimu maarufu kama Ngao ya Jamii

Rekodi hizo zinaifanya Simba iingie kifua mbele kwenye mchezo wa kesho ambao utapigwa saa 11 jioni uwanja wa Taifa

Nahodha John Bocco amesema wamejipanga kuendeleza ubabe kwa Azam, wakiweka mikakati ya ushindi

“Mimi sitacheza mechi kwa sababu bado sijawa fiti, lakini nazungumza kama nahodha, tumejipanga vizuri, wachezaji wenzangu naamini watafanya kile walichoelekezwa na mwalimu,” alisema Bocco.

Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikikusanya alama 12 baada ya kushinda michezo yote minne iliyocheza

Azam Fc ina alama tisa ikiwa nayo imeshinda mechi zote tatu walizocheza

Hivyo ni mchezo utakaokutanisha timu zote zenye rekodi ya ushindi wa asilimia 100 kwenye ligi msimu huu

Senzo atembelea TFF

Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba Senzo Mazingiza leo alipata nafasi ya kutembelea Ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) zilizoko Ilala jijini Dar es salaam

Ziara hiyo ya kwanza tangu akabidhiwe majukumu ya klabu ya Simba, ilikuwa maalum kwa ajili ya kujitambulisha na kubadilishana mawazo na viongozi wa TFF

Senzo ameanza majukumu yake vyema kunako klabu ya Simba, akishiriki kikamilifu katika matukio mbalimbali

Simba yaahidi kuendeleza ushindi VPL

Katika misimu miwili iliyopita, Simba imeweka rekodi bora ya kufanya vizuri dhidi ya Azam Fc katika michezo iliyozikutanisha timu hizo kwenye ligi

Msimu uliopita Azam Fc iliambulia alama moja tu katika mchezo wa ligi kuu mzunguuko wa pili

Kwenye mchezo wa mzunguuko wa kwanza Azam Fc ilipokea kichapo cha mabao 3-1, mabao ya Meddie Kagere (2) na nahodha John Bocco huku lile la Azam likifungwa na Frank Domayo

Ushindi pekee iliyopata Azam dhidi ya Simba ni michuano ya Kagame na kombe la Mapinduzi ambayo Simba haikuwa imeipa umuhimu

Msimu huu tayari Azam Fc wameshachezea kichapo cha mabao 4-2 kwenye mchezo wa ufunguzi wa msimu maarufu kama Ngao ya Jamii

Rekodi hizo zinaifanya Simba iingie kifua mbele kwenye mchezo wa kesho ambao utapigwa saa 11 jioni uwanja wa Taifa

Nahodha John Bocco amesema wamejipanga kuendeleza ubabe kwa Azam, wakiweka mikakati ya ushindi

“Mimi sitacheza mechi kwa sababu bado sijawa fiti, lakini nazungumza kama nahodha, tumejipanga vizuri, wachezaji wenzangu naamini watafanya kile walichoelekezwa na mwalimu,” alisema Bocco.

Simba iko kileleni mwa msimamo wa ligi ikikusanya alama 12 baada ya kushinda michezo yote minne iliyocheza

Azam Fc ina alama tisa ikiwa nayo imeshinda mechi zote tatu walizocheza

Hivyo ni mchezo utakaokutanisha timu zote zenye rekodi ya ushindi wa asilimia 100 kwenye ligi msimu huu

Yanga sc yapania kuichakaza mbao fc

Kikosi cha Yanga kiko mkoani Mwanza ambapo leo jioni watashuka kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuikabili Mbao Fc ukiwa ni mchezo wa ligi kuu ya Vodacom

Yanga mabingwa mara 27 ligi kuu ya Tanzania Bara watakuwa na kazi moja tu ya kuhakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mchezo huo

Hata hivyo Mbao Fc imekuwa na kawaida ya kuwapa wakati mgumu vijana hao wa Jangwani hasa wanapokutana dimba la CCM Kirumba

Msimu uliopita kwa mara ya kwanza Yanga iliweza kupata ushindi dhidi ya Mbao hapo Kirumba baada ya kupoteza michezo mitatu kabla

Morali ya wachezaji wa Yanga iko juu hasa ikizingatiwa wanakabiliwa na mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Pyramids Fc Jumapili ya Oktoba 27

Matokeo ya ushindi yatawaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na wakazi wa jiji la Mwanza na mikoa ya jirani

Jana jioni Yanga ilifanya maandalizi yake ya mwisho kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuelekea mchezo huo

Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera alisema vijana wake wako tayari kwa mchezo huo

“Kwa kawaida naiandaa timu kwa ajili ya mchezo uliokuwa mbele yangu, hadi sasa timu iko vizuri na tayari kwa mchezo dhidi ya Mbao FC”

“Tunawaheshimu Mbao ni timu nzuri, lakini na sisi ni wazuri pia na tumejiandaa kwa ushindi,” alisema

Virgil van Dijk ni mmoja wa wachezaji saba wa Liverpool waliotajwa Ballon d’Or

Virgil van Dijk ni mmoja wa wachezaji saba wa Liverpool waliotajwa kuwa miongoni mwa Wachezaji 30 wanaowania tuzo ya Ballon d’Or mwaka huu 2019, Mohamed Salah, Sadio Mane, Roberto Firmino, Trent Alexander-Arnold, Georginio Wijnaldum na Alisson pia walichaguliwa kutoka katika Kikosi hicho cha Mabingwa wa Ulaya..

– Liverpool ikiwa ndio Klabu ambayo imetoa Wachezaji wengi zaidi, inafuatiwa na Wachezaji watano wa Manchester City – Raheem Sterling, Riyad Mahrez, Kevin Bruyne, Bernardo Silva na Sergio Aguero – wapo kwenye orodha… Kutoka Premier League, Hugo Lloris na Son Heung-min kutoka Tottenham wamejumuishwa pia.

– Cristiano Ronaldo na Lionel Messi, ambao wameshinda taji mara 10 kati yao, wako tena kati ya wagombea…Barcelona ina wachezaji wanne; Messi, Frenkie de Jong, Marc-Andre ter Stegen na Antoine Griezmann wako kwenye orodha hiyo…Mshambuliaji wa Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang amejumuishwa, na pia mchezaji wa zamani wa Chelsea na Sasa Real Real Madrid, Eden Hazard yupo katika Orodha hiyo pamoja na mwenzake, Karim Benzema… Wengine ni Roberto Lewandowski kutoka Bayern Munich, Joao Felix zamani Benfica na Sasa Atletico Madrid, Kylian Mbappe & Marquinhos kutoka PSG, Kalidou Koulibaly kutoka Napoli, Don Van De Beek & Dusan Tadic kutoka Ajax na Matthijs de Ligt zamani Ajax na Sasa Juventus… Mshindi kutangazwa huko Paris nchini Ufaransa siku ya Disemba 02, 2019.
#BallonDor
@Harunlugoyah

Tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia U21 kutolewa

– Tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia chini ya umri wa miaka 21, kwa mara ya Pili inatolewa mwaka huu tuzo hii inayojulikana Kama “Kopa Trophy” ikipewa jina baada ya Mchezaji wa zamani wa Ufaransa Aliyefariki Dunia Miaka Miwili iliyopita, Raymond Kopa… kwa mara ya kwanza ilitolewa mwaka jana 2018, mshambuliaji wa Paris St-Germain na Mshindi wa Kombe la Dunia kwa Ufaransa, Kylian Mbappe aliiibuka mshindi, akiwabwaga, Christian Pulisic na Justin Kluivert.

– Wagombeaji wa tuzo wa mwaka huu ni Kinda wa Borussia Dortmund na England, Jadon Sancho “19”, Mshambuliaji wa Everton na Italia, Moise Kean, 19, na kiungo wa kati wa Ufaransa Matteo Guendouzi, Umri wa miaka 20 akikipiga pale Arsenal.
….
– Wengine ni Beki wa Juventus na Uholanzi, Matthijs de Ligt, 20, mshambuliaji wa Brazil na Real Madrid Vinicius Junior, 19, mlinda lango wa Real Valladolid na Ukraine, Andriy Lunin, 20, kiungo wa Bayer Leverkusen na Ujerumani, Kai Havertz, 20, Mshambuliaji wa Atletico Madrid na Ureno, Joao Felix 19, Samuel Chukwueze akiwa na miaka 20 kutoka nchini Nigeria na Klabu ya Villarreal, na vile vile Lee Kang-in wa umri wa miaka 18 akikipiga pale Valencia na kutoka nchini Korea Kusini..
#KopaTrophy #Updates
@Harunlugoyah

TFF KUMTANGAZA NDAYIRAGIJE WIKI HII

Rais wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Wallace Karia amesema ndani ya wiki hii itamtangaza rasmi kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’. Karia hajaweka wazi kama Ettiene Ndayiragije ambaye alikuwa kaimu kocha mkuu kuwa ndiye atakaye tangazwa ingawa mwenyewe amethibitisha kuwa atakinoa kikosi hicho kinachojianda na michuano mbalimbali.

Rais huyo ambaye ametimiza miaka miwili madarakani amesema wanasubiri ripoti ya kocha huyo kabla ya kutangaza kocha mpya ndani ya wiki hii. “Tumepokea maombi kwa makocha wengi wakitaka kuifundisha Taifa Stars lakini tunapitia CV zao na ndani ya wiki hii tumtangaza kocha mpya,” alisema Karia.

Kwa upande wa Ndayiragije ameishukuru klabu yake ya Azam FC kwa kumruhusu kuondoka bila kipingamizi huku akiwatakia kila la kheri.

@tanfootball @taifastars_ @wallacekaria @wilfredkidao
#wapendasokaupdates

Design a site like this with WordPress.com
Get started