
Pyramids.. Pyramids.. Pyramids! Wakiwa ugenini kule Congo Brazzaville, walipata bao kipindi cha kwanza. Mechi ikaisha 1-0. Wakashinda.
Wakiwa ugenini kule Algeria walipata bao dakika ya 11 kipindi cha pili. Mechi ikaisha 1-0. Wakashinda.
Kwa picha ya haraka haraka, kwa game hizo 2 zilizopita, hawa jamaa wana uwezo wa kutumia presha ya wenyeji kufunga mabao ya haraka, then ni wagumu kwenye safu yao ya ulinzi.
Nimetazama mechi zao 3 za Ligi.. Wanapenda kufunga mabao kipindi cha kwanza. Nini Yanga wafanye? Kuchunga sana presha yao ya uhitaji wa matokeo kwa pupa.
Wale Waalgeria walifungwa kwa krosi kutoka wingi ya kushoto. Wale Congo walifungwa kwa krosi kutoka wingi ya Kulia.
Unaona walivyo hatari kupitia pembeni. Wana uwezo wa kumiliki mpira lakini hutoka kwa kasi sana wanapovuka mstari wa kati
Ni mechi ambayo JUMA ABDUL na SONSO wanatakiwa kuwa katika viwango vyao bora zaidi.
Ni mechi ambayo ALLY ALLY anatakiwa kua bora sana kwenye mipira ya hewani.
Makame. Anahitahi kutuliza presha yake. Waarabu wanaweza kumtoa mchezoni kwa kutumia madhaifu yake ya kukosa utulivu
FeiToto, kama atapangwa, hii ni mechi ambayo anatakiwa kurejesha ubora wake kwa asilimia 100. Ile tabu aliyompa Makame kwa Zesco isiwepo leo.
Tshishimbi🙌 Game inafanana na yeye. Ana uwezo wa kuiamua hii mechi kama atacheza kwa utulivu mkubwa. Asiruhusu waarabu watulie na mpira katika eneo lao. Aongoze pressing.
Balama🙌 Yes.. Hii ni game yake ya kufunga na sio kuasist. Yeye pekee ndie atakaekua mchezaji huru eneo la mbele. Atumie faida ya nguvu/mikimbio ya Sadney kwenye kujitengenezea nafasi.
Sioni Sibomana akianza leo. Bado hajawa na ufiti wa asilimia 100. Mrisho Ngassa, kama atapewa game, basi akumbushwe mbali na kushambulia, jukumu lake la msingi leo ni kushuka kumsaidia Sonso.
Mechi ni ngumu sana kwa Yanga na Pyramids. Tension ni kubwa mno! Wasiwasi wangu uko kwa mabeki wa pembeni wa Yanga lakini Tshishimbi na Balama, kama watamka fresh, kimbinu hii ni game yao kuwabeba Wananchi.
Kila la kheri Yanga🙏
#kwako_mwalim_kashasha


















