Mijadala.yaibuka nini maana ya CLEAN SHEET,

KUNA, mijadala bado inaendelea kwenye mitandao ya Kijamii, kuhusu Neno CLEAN SHEET, kwenye mchezo wa soka linatumikaje.
.
.
CLEAN SHEET, ni kitendo cha timu nzima kucheza bila ya wavu wao kuguswa , hii mara nyingi wana michezo huwa tunaangalia eneo la safu ya ulinzi. Na ukisema safu ya ulinzi inaanzia goal kipa mabeki wake wa kati wapembeni na kiungo namba cha ulinzi hao wote ni safu ya ulinzi ndo huwa mara nyingi wanahusika sana kwenye clean sheet.
.
.
Kwa sababu wao ndo muda mwingi wanafanya majukumu ya ulinzi kwenye eneo la nyuma kama huna safu bora ya ulinzi maana yake kuna asilimia 70 za kuwa kila mechi unaruhusu mabao zipo timu kibao kupata CLEAN SHEET, kwao ni ngumu sana.Leo nimekumbuka maneno ya kocha Jose Mourinho, aliwahi kusema hivi wakati akiwa kocha wa Inter Milan, kuwa ukiwa na safu bora ya ulinzi utatwaa Ubingwa na alikuwa akimaanisha kitu akafanikiwa kutwaa Ubingwa wa Ulaya mwaka 2010.
.
.
CLEAN SHEET, pia inatumika kwenye kuwafananisha wachezaji kila msimu mfano mzuri labda Virgil Van Djick , amecheza michezo 50 ameruhusu wavu kuguswa mara 7 na amepata CLEAN SHEET, 6 na Puyol, amecheza michezo 50 wavu wake umeguswa mara 9 na amepata CLEAN SHEET, mara 4 je nani bora hapo ni Virgil Van Djick, namba zinambeba 🙌🙌.
.
.

Kaka yangu @alikamwe, anasema hivi CLEAN SHEET, ni ya kipa tu sawa je? Kipa anacheza peke yake ndani?jibu ni hapana. Na pia kusema kiungo hasifiwi CLEAN SHEET, je ukitaka kumfaninisha na Kiungo wa timu pinzani ni lazima utimie kigezo cha CLEAN SHEET, amecheza michezo mangapi safu yake ya ulinzi imeruhusu mabao mangapi na vingine.
.
.
Kipa ndo mchezaji anayepata ile Golden glove, kwa sababu kwa upande wa asimilia 80 anaokoa michomo hatari pale timu yake mabeki wanavo kuwa hawachezi vizuri mfano mzuri mchezo wa Jana wa ligi kuu England kati ya Tottenham dhidi ya Liverpool, kipa wa Paul Diano Tottenham, aliokoa michomo 7 kipindi cha kwanza 🙌.
.
.
✍🏻@azizi_mtambo_15 wa @sokaplace_
Powered by @bikotanzania

Pogba nje ya dimba hadi.mwezi disemba

Ole Gunner Solskjaer: 🗣 “Sidhani kama tutamuona Paul kabla ya mwezi wa 12. Hatutakuwa naye kwa muda. Anahitaji muda wa kutosha ili kupona kabisa, kwa hivyo sidhani kama atarudi kwasasa.” Paul Pogba nje ya uwanja hadi mwezi Desemba mwaka huu kutokana na Majeraha ya enka.

Mfaransa huyu mwenye miaka 26, hajacheza mechi yoyote tangu mwezi wa 9 mwaka huu baada ya kupata majeraha ya ankle kwenye mchezo dhidi ya Arsenal

Biashara fc yapata mkombozi safu.ya ulinzi

Kiungo Novatus Dismas mwenye umri wa miaka 17 ameibuka kuwa lulu kwenye kikosi cha Biashara UTD cha mjini Musoma mkoani Mara,kiungo huyo anacheza pia timu ya taifa ya vijana U 20 ( Ngorongoro Heroes ) amejizolea sifa kutokana na kuiongoza timu yake kutokuruhusu nyavu kuguswa kwenye michezo yao 3 iliyopita ya VPL,
Hapo jana aliiongoza timu yake kupata ushindi wa bao 1-0 mbele ya Namungo FC.
Hongera sana kijana @novadismac_40 Michezo = 3
Ushindi = 2
Sare = 1
Dakika alizocheza = 270
Clean sheet = 3

YANGA YALALA MBELE YA WAARABU KIRUMBA

Matumaini ya kuingia hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Afrika kwa timu ya Yanga yamefifia baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 katika mchezo uliofanyika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mchezo huo ulianza kwa kasi huku timu hizo sikisomana lakini Pyramids walifanya mashambulizi ya hatari zaidi langoni mwa Yanga.
Pyramids walipata bao la kwanza dakika ya 42 kupitia kwa Traory Erick baada ya kutengewa pasi na Mohammed El Qaras akiwa ndani ya 18 na kupiga shuti la chini chini lililomshinda mlinda mlango Farouk Shikalo.

Pyramids waliongeza bao la pili dakika ya 62 baada ya Traory kutoka na mpira nyuma kwenye lango lao huku wachezaji wa Yanga wakidhani mpira ulikuwa umetoka na kupiga pasi iliyomkuta Abdallah Sayed nakuuweka kimiani.

Nahodha wa Yanga, Papy Tshishimbi aliwafungia vijana hao wa Jangwani bao la kufutia machozi dakika ya 88 akimalizia pasi ya Patrick Sibomana akiwa ndani ya 18.

Yanga ilimaliza mechi hiyo wakiwa pungufu baada ya mlinzi Kelvin Yondani kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 90 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.

Mchezo wa pili wa marudiano utapigwa nchini Misri Novemba 3 ambapo Yanga itahitaji kupata ushindi wa bao mbili ili kufuzu hatua ya makundi.

#wapendasokaupdates
#CAFCC

Mocha wa zamani.taifa stars …kujiunga na yanga

“Niko Denmark naendelea na project mbalimbali za FIFA. Sina mkataba na timu yoyote ile kwa sasa. Nimepokea simu nyingi kutoka Tanzania leo. Yanga ni timu kubwa sana Tanzania na nafikiri itanipa pia fursa ya kusaidia maendeleo ya soka la Afrika kama nitakwenda kufanya nao kazi.”
.
.
Kim Poulsen, akijibu tetesi za kutafutwa na Uongozi wa Klabu ya Yanga.

Cc @alikamwe

Mchezo.kombe la.shilikisho wahairishwa kisa mvua

– Mchezo wa jana wa Play-off ya Kombe la Shirikisho, kati ya Asante Kotoko dhidi ya FC San-Pedro umeshindwa kuendelea Kipindi cha Pili kufuatia Maamuzi ya mwamuzi kuahirisha kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha huko Kumasi, Ghana 🇬🇭.

– Mechi hiyo ambayo Asante Kotoko ndio wenyeji wa San Pedro itachezwa tena leo kuanzia mwanzo tu wa kipindi cha pili (Dakika 45) Matokeo Mpaka Mapumziko yalikuwa ni 0-0.
#CAFCC #TotalCAFCC
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started