Kambi ya timu ya 🇰🇪 kwa Wanawake imevunjwa ukata wa pesa wazidi

✍🏻 Kambi ya timu ya Kenya 🇰🇪 kwa Wanawake imevunjwa rasmi hii leo, Shirikisho la Soka Nchini humo limethibitisha kuwa Sababu ni Ukata wa Fedha.. Kwamba Serikali haijaziunga Mkono timu zao za Taifa..

✍🏻 Wakina Dada hao walikuwa wanajiandaa na mchezo wao wa Raundi ya Nne kuwania Kufuzu Michuano ya Olimpiki 2020 dhidi ya Zambia ambapo game ya kwanza imepangwa kufanyika Novemba 04 na siku Nne Baadaye watarudiana huko Lusaka.

✍🏻 Hali Ikiendelea hivi, inaweza kutokea mpaka katika timu ya taifa ya Wanaume “Harambee Stars”, ikiwa Serikali ya Kenya itaendelea kushindwa kuzipa huduma timu zao za Taifa, Basi huenda Kikosi cha Harambee Stars kikashindwa kusafiri kwenda Misri kucheza mechi yao ya kuwania Kufuzu Fainali za AFCON 2021 dhidi ya Mafarao hao siku ya Novemba 14.
#Olympic #AFCONQualifier
@Harunlugoyah

No.salad aitwa kikosini misri kujifua AFCON

🇨🇩 Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Misri, Hossam El Badry Amemuita mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah katika kikosi chake kuelekea kwenye mechi za kuwania Kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi ujao Novemba… El Badry alikubali kumpumzisha Salah kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Botswana mapema mwezi huu katika mechi ya Kirafiki.
..
✍🏻 Mafarao wataanza kampeni yao ya kuwania Kufuzu Kombe la Mataifa Afrika 2021 dhidi ya Kenya 🇰🇪 mnamo 14 Novemba nyumbani kisha kusafiri kwenda Comoros 🇰🇲 siku nne baadaye.

✍🏻 Katika Kikosi hicho, Kuna ongezeko la Mahmoud Abdul Monem ‘Kahraba’ kwa mara ya kwanza tangu Kombe la Dunia la 2018 nchini Urusi…Kahraba hivi sasa yuko Ureno akiichezea Aves na amefanikiwa kufunga bao moja katika mechi nne msimu huu… Kocha huyo pia kawaita kwa mara ya kwanza Wachezaji kutoka Ligi ya Ndani, Ahmad Mahmoud Wahed wa Al Ahly, Marwan Hamdi wa Wadi Degla, Mohamed Farouk wa Pyramids na Ahmed “Zizo” Sayed, ambaye anachezea Zamalek.
#Egypt #Pharaohs #TotalAFCON2021 #AFCONQualifier
@Harunlugoyah

Makocha watatu kutua jangwani nani.kumrithi zahera

👉 Chini Chini ya Kapeti ni Kwamba mmoja kati ya Hawa Makocha Wazoefu anaweza kuja kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Yanga SC ambayo kwasasa ipo chini ya Mwinyi Zahera 🇨🇩… Kazi kwenu Wananchi katika Kutafuta Kocha mpya au kuendelea kumuamini na kumuunga Mkono Papaa Zahera 🙌..
:
✍🏻 Kim Poulsen 🇩🇰 kwa mara ya kwanza alitua Nchini Tanzania April 2011 na kuanza kuinoa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania chini ya Umri wa Miaka 21 hadi Mei mwaka 2012 na kuchukua mikoba mwenzake, Jan Børge Poulsen kwenye kikosi cha Taifa Stars… Alitimuliwa japo wengi hawakupenda kuondoka kwake..

✍🏻 Raoul Jean-Pierre Shungu 🇨🇩 kwa mara ya kwanza alitua nchini mwaka 1998 kuja kuwa kocha Mkuu wa Yanga SC, Lakini alitimuliwa mwaka 2000…Katika kipindi chake cha kufanya kazi kwake Yanga, Shungu aliipa Yanga Kombe la Afrika Mashariki na Kati, mwaka 1999 katika fainali zilizofanyika Kampala, Uganda 🇺🇬 na mataji kadhaa ya nyumbani, likiwemo Kombe la FA, Nyerere, Muungano na ubingwa wa Bara.. Aliondoka Yanga baada ya kutofautiana na Mwenyekiti wa klabu hiyo wakati huo, Tarimba Abbas baada ya kusema amekwenda Ufaransa kusoma kozi fupi ya FIFA, lakini aliporudi akaambiwa aonyeshe pasipoti yake kama viza ya nchini humo, akawa anapiga chenga, hivyo akaonekana muongo.. Kilichofuatia, aliyekuwa kocha wa African Sports ya Tanga wakati huo, Charles Boniface Mkwasa akaajiriwa kama Meneja wa timu na Shungu akaondolewa.. Kwa Sasa Shungu bado Ni Kocha Msaidizi wa kwanza wa The Dolphins 🐬 “AS Vita Club” 🇨🇩.

✍🏻 Hans Van Der Pluijm 🇳🇱 Kwa mara ya kwanza alitua Nchini Tanzania mwaka 2014 kuja kuwa kocha Mkuu wa Yanga SC, Alipata mafanikio makubwa Mno na timu hiyo ya Wananchi na hilo lipo wazi, Aliiongoza Yanga mpaka 2017 akitwaa Ubingwa wa FA, Mataji ya Ligi Kuu na kuifikisha timu katika hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kisha kuwa Mkurugenzi wa Ufundi kwa muda mfupi kisha kutimka, akatua Singida Kisha kumaliza Career yake Nchini akiwa na Azam FC..
#TransfersNews #VPLUpdates #CAFCC

✍🏻 @Harunlugoyah

Kocha wa @BafanaBafana ataja kikosi

Kocha wa @BafanaBafana ya Afrika Kusini Molefi Ntseki ametaja
Kikosi kilichoitwa kwa ajili ya Maandalizi ya Mchezo wa kufuzu Afcon dhidi ya Ghana November 14 Mwaka huu
:
1. Darren KEET OH Leuven FC (Belgium)
2. Ronwen WILLIAM Supersport United FC (SA)
3. Ricardo GOSS Bidvest Wits FC (SA)
DEFENDERS:
4. Erick MATHOHO Kaizer Chiefs FC (SA)
5. S’fiso HLANTI Bidvest Wits (SA)
6. Buhle MKHWANAZI Bidvest Wits FC (SA)
7. Thulani HLATSHWAYO (C) Bidvest Wits FC (SA)
8. Thapelo MORENA Mamelodi Sundowns FC (SA)
9. Thamsanqa MKHIZE Cape Town City FC (SA)
10. Innocent MAELA Orlando Pirates FC (SA)
11. MOSA LEBUSA Mamelodi Sundowns (SA)
:
MIDFIELDERS:
12. Kamohelo MOKOTJO Brentfort FC (England)
13. Bongani ZUNGU Amiens FC (France)
14. Thato MOKEKE Cape Town City FC (SA)
15. Dean FURMAN Supersport United FC (SA)
16. Lebohang PHIRI Guingamp FC (France)
17. Mothobi MVALA Highlands Park FC (SA)
18. Themba ZWANE Mamelodi Sundowns FC (SA)
19. Thembinkosi LORCH Orlando Pirates FC (SA)
20. Percy TAU Club Brugge FC (Belgium)
21. Thulani SERERO Al Jazira FC (Abu Dhabi)
22. AUBREY MODIBA Supersport United FC (SA) :
FORWARDS
23. Lebo MOTHIBA Strasbourg FC (France)
24. Bradley GROBLER Supersport United FC (SA)
25. Kermit ERASMUS

Powered by @bikotanzania

TARIMBA AMKINGIA KIFUA ZAHERA YANGA

Mkurugenzi wa Udhibiti na Uendeshaji wa SportPesa ambaye pia ni mwanachama wa klabu ya Yanga, Tarimba Abbas amesema kocha wa timu hiyo, Mwinyi Zahera hapaswi kulaumiwa juu cha kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Pyramids ya Misri walichopata jana.

Tarimba amesema kipigo cha jana katika uwanja wa CCM Kirumba kimetokana na uzembe wa moja kwa moja kutoka kwa wachezaji wa Yanga na sio kosa la kocha Zahera.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa bao la pili walilofungwa lilitokana Mrisho Ngasa kuacha kukaba akidhani mpira ulikuwa umetoka wakati mwamuzi hakupiga filimbi huku lile la kwanza likitokana na uzembe wa Papy Tshishimbi. “Sijaona kosa la kocha Zahera, wachezaji wenyewe walifanya makosa ya kizembe ambayo wenzetu waliyatumia na kupata matokeo ugenini,” alisema Tarimba.

Tarimba amekiri kuwa Pyramids wanafungika kama Yanga itajipanga vizuri itaweza kupindua meza kibabe ugenini nchini Misri, Novemba 3.

#wapendasokaupdates

TARIMBA AMKINGIA KIFUA ZAHERA YANGA

Mkurugenzi wa Udhibiti na Uendeshaji wa SportPesa ambaye pia ni mwanachama wa klabu ya Yanga, Tarimba Abbas amesema kocha wa timu hiyo, Mwinyi Zahera hapaswi kulaumiwa juu cha kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Pyramids ya Misri walichopata jana.

Tarimba amesema kipigo cha jana katika uwanja wa CCM Kirumba kimetokana na uzembe wa moja kwa moja kutoka kwa wachezaji wa Yanga na sio kosa la kocha Zahera.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa bao la pili walilofungwa lilitokana Mrisho Ngasa kuacha kukaba akidhani mpira ulikuwa umetoka wakati mwamuzi hakupiga filimbi huku lile la kwanza likitokana na uzembe wa Papy Tshishimbi. “Sijaona kosa la kocha Zahera, wachezaji wenyewe walifanya makosa ya kizembe ambayo wenzetu waliyatumia na kupata matokeo ugenini,” alisema Tarimba.

Tarimba amekiri kuwa Pyramids wanafungika kama Yanga itajipanga vizuri itaweza kupindua meza kibabe ugenini nchini Misri, Novemba 3.

#wapendasokaupdates

Kivumbi kombe la dunia vijana USA 1-4 SENEGAL

– Michuano ya Kombe la Dunia kwa Vijana walio chini ya Umri wa Miaka 17, imeendelea kutimua vumbi jana huko Nchini Brazil kwa kupigwa mechi za Kundi C na Kundi D… Baada Wawakilishi kutoka Barani Afrika, Angola 🇦🇴 na Nigeria 🇳🇬 kuanza na Ushindi Juzi, Hatimae na jana Wawakilishi wengine, Senegal 🇸🇳 wameanza kwa kupata Ushindi.
….
KUNDI C
FT: Ufaransa 🇫🇷 2️⃣ – 0️⃣ 🇨🇱 Chile
FT: Korea Republic 🇰🇷 2️⃣ – 1️⃣ 🇭🇹 Haiti
:
Kundi D
FT: Marekani 🇺🇸 1️⃣ – 4⃣ 🇸🇳 Senegal
FT: Japan 🇯🇵 3⃣ – 0️⃣ 🇳🇱 Uholanzi
….
– Leo tena Michuano hii inaendelea kwa kuchezwa game nyingine za Kundi E na Kundi F… Kila Lakheri Cameroon 🇨🇲 ✊.
KUNDI E.
23:00 Hispania 🇪🇸 🆚 🇦🇷 Argentina
02:00 Tajikistan 🇹🇯 🆚 🇨🇲 Cameroon
:
KUNDI F.
23:00 Solomon Islands 🇸🇧 🆚 🇮🇹 Italia
02:00 Paraguay 🇵🇾 🆚 🇲🇽 Mexico
#U17FIFAWC #FIFAU17WorldCup
@Harunlugoyah

Design a site like this with WordPress.com
Get started