
Klabu ya FC Barcelona ilipitisha bajeti mpya ya msimu mnamo October 4, kwa msimu huu wanahitaji kiasi cha Euro millioni – lakini ili kufikia target waliyojiwekea wanahitaji kuuza wachezaji ambao wataweza kuzalisha kiasi cha 124m kabla ya June 30, 2020.
.
Klabu hiyo tayari imeshaanza kufanyia kazi mauzo ya baadhi ya wachezaji na mazungumzo yanaendelea.
Hawa ndio baadhi ya wachezaji wanaotajwa kuwekaa sokoni ili Barca ikamilishe bajeti yake. .
.
. β’Ivan Rakitic
Kiungo huyu wa Croatia yupo kwenye siku za mwisho za maisha yake ndani ya Camp Nou, alinusurika kuuzwa wakati wa dirisha la kiangazi baaada ya kupoteza nafasi kikosini, lakini sasa huenda dirisha la mwezi January likamuondoa Blaugrana.
Juventus walimhitaji na huenda wakarejea tena lakini pia kuna uwezekani akaenda aidha Inter au Manchester United wenye uhitaji wa kiungo kama Rakitic .
.
.
. β’ Arturo Vidal
Vidal hajawahi kuwa na nafasi ya kudumu katika kikosi cha Barca na sasa amepoteza zaidi nafasi na hili limezidisha timu zinazomhitaji kuzidi kumtolea macho – wakiongozwa na Inter Milan ambao kocha wao Antonio Conte anamhusudu sana Vidal.
Barcelona wanahitaji kumuuza sasa ili kupata pesa na kuondokan na hatari ya kumpoteza kwa uhamisho huru mwaka 2021. .
.
β’ Coutinho & Malcom π§π· .
Wabrazil hawa wawili ni biashara ambazo biashara ambazo zinahitaji ukamilifu tu.
Malcom aliuzwa kwenda Zenit Saint Petersburg kwa ada ya jumla ya 40m euros, lakini mpaka sasa imelipwa kiasi cha 8.2m euros, malipo mengine yataendelea kulingana na mkataba waliokubaliana.
Coutinho yupo kwa mkopo Allianz Arena, The Bavarians wanaweza kumsaini mchezaji huyo kwa ada ya uhamisho wa 120m euros – mpaka sasa ameanza vizuri msimu kiasi cha kuwashawishi vibopa wa Bayern kulipa fedha hizo ili kumsaini kiungo huyo wa Brazil. . .
. β’ Samuel Umtiti
Alikuwa na msimu bora sana wa 2017/18, lakini msimu uliopita majeruhi yaliharibu sana maendelea ya career yake ndani ya klabu. Barca bado wanamhitaji lakini huenda wakamuuza kutokana tu na majeruhi.
Wachezaji wengine ambao huenda wakauuzwa ni Carles Perez, Moussa Wague na Marc Cucurella.