
Yale tuliyoyashuhudia kwa Yanga kupitisha bakuli kwa mashabiki wa klabu hiyo ili kupata fedha za kujiendesha – yamejitokeza kwa namna nyingine nchini Tunisia.
.
.
Mashabiki kindakindaki wa Club Africain wachangia $450,000 za Kimarekani kwa siku moja (zaidi ya bilioni 1) ili kusaidia kulipa deni la klabu hiyo
:
Mashabiki wa klabu kongwe ya Tunisia ikiwa ni pamoja na shabiki mmoja mwenye ulamavu wa macho ambaye alichagua kutoa fedha ya gharama za dawa anayotumia ili kusaidia timu yake pendwa, kwa ujumla wametoa zaidi ya Dola $450,000 (Pauni 350,000) kwa siku moja wakati wanapambana kuokoa klabu kutoka katika ukata wa kifedha
Club Africain, ambayo ni klabu ya pili kongwe Tunisia na moja ya klabu zinazojulikana barani Afrika, imekatwa pointi sita na kupigwa faini ya kifedha ($6m) kwa sababu ya kutolipa mishahara kwa wachezaji wake wa zamani.
Ili kusaidia klabu ambayo ilianzishwa mwaka 1920, Shirikisho la Soka la Tunisia (FTF) liliunda kamati ya usimamizi wa mgogoro huo ili kuokoa timu kutopata na vikwazo zaidi.
Ilikuwa mwezi Oktoba, FTF ilianzisha akaunti ya benki kwa mashabiki kutoa pesa kusaidia kuondoa deni ambalo linaikabili Club Africain na hadi sasa dola za Kimarekani 600,000 zimekusanywa.
Katika kampeni ya masaa 24 iliyofanyika Junanne, mashabiki wa Club Africain wameonyesha kina cha kujitolea kwao kwa kilabu, ikiwa ni pamoja na mashabiki wazee na watoto ambao walifika na benki listi za malipo ya benki kwenye makao makuu ya klabu hiyo uku wakiwa na shabiki ambaye ni mlemavu wa macho aliyekabidhi akiba yake na klabu ilionyesha heshima kwa kumkabidhi jezi iliyosainiwa na wachezaji wote wa Club Africain.
Hiyo jumla pamoja na michango ya Jumanne inamaanisha klabu ya Africain imefikisha zaidi ya $ 1m kwa deni lote ambalo shirikisho limeweka ikiwa ni $ 6m (bilioni 13.8)




Jina lake halisi ni Oluwafikayomi Oluwadamilola Tomori na alizaliwa Desemba 19, 1997 katika Mji wa Calgary, Alberta, Canada. Wazazi walikuwa Wanigeria lakini ambao walihamia jijini London, England.


Kuna muda macho yetu huhukumu lakini kuna nyakati uhalisia ubaki kuwa kwenye uhalisia wake!!!
#VodacomPrimierLeague









