Vita ya kuwania kiatu cha ufungaji bora Vpl 2019/20 ni ya 4G. .

Vita ya kuwania ufungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara imezidi kupamba kushika kasi ya 4G baada ya washambuliaji wawili wa Lipuli, Daruweshi Saliboko na Paul Nonga kufikisha mabao sita wakiwa nyuma kwa mabao mawili kwa kinara Meddie Kagere wa Simba.
.
Kagere anaongoza msimamo wa wafungaji bora akiwa amefunga mabao nane wakati Saliboko na Nonga wote wamefikisha mabao sita kila mmoja. Mabao matatu aliyofunga Saliboko na mawili ya Nonga katika mchezo dhidi ya Singida Utd jumatano ya wiki hii yametosha kuwapaisha wachezaji hao hadi katika nafasi ya pili katika msimamo wa wafungaji na kumkaribia Kagere.
.
Wachezaji wengine wanaofuatia katika chati ya wafungaji ni Athuman Miraj wa Simba, Peter Mapunda (Mbeya City), Yusuf Mhilu (Kagera Sugar) na Gerald Mathias Mdamu wa Mwadui wenye mabao manne kila mmoja.
.

C

omment fupi fupi chapu tupite. Unaionaje kasi hii..??
#bakinasisi__
#TupoNawePaleUlipo
#NjooKwetu

SAMATTA AWANIWA NA NEWCASTLE NA WEST HAM

Vilabu viwili vya ligi kuu ya England Newcastle United na West Ham United vimeonyesha nia ya kumsajili nahodha wa Taifa Stars na mshambuliaji wa Genk ya Ubelgiji Mbwana Samatta katika dirisha dogo la usajili la mwezi January.

Samatta mfungaji pekee wa bao la Genk katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Liverpool wakati Genk walipofungwa bao 2-1 anatajwa kuwa na thamani ya paundi milioni 10.

#wapendasokaupdates

NDANDA: YANGA ITAKUJA NA HASIRA NANGWANDA LAKINI TUTAWATULIZA

Uongozi wa klabu ya Ndanda FC ya Mtwara umesema unafahamu Yanga itaingia kwa hasira katika mchezo wao wa leo wa ligi kuu ya Vodacom kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona dhidi yao ili kupata ushindi baada ya kulifuta benchi zima la ufundi.

Yanga ililiondoa benchi zima la ufundi la klabu hiyo lililokuwa chini ya Mwinyi Zahera na msaidizi wake Noel Mwandila juzi Jumanne kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa timu.

Katibu mkuu wa Ndanda, Seleman Kachele amesema wanatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Yanga ambao hawatapenda kupoteza mechi baada ya kufukuza benchi la ufundi lakini wamefanya mazoezi ya kutosha kuhakikisha wanabaki na alama zote tatu nyumbani. “Yanga ni timu kubwa na ina wachezaji wazuri, wametoka kuliondoa benchi la ufundi kwahiyo watakuwa na hasira kusaka pointi tatu na sisi tutatumia hasira zao kuwamaliza,” alisema Kachele.

Baada ya kumfuta kazi Zahera na benchi lake zima la ufundi sasa Yanga ipo chini ya kocha wa muda Charles Mkwasa akisaidiwa na winga wazamani wa timu hiyo Said Maulidi ‘SMG’. #wapendasokaupdates

SURA YAKE INATIA HURUMA,MWILI UNAMHUKUMU

:
Prepared @octa_ayubu_jr
:
Kila kazi unayotaka kuifanya lazima uangalie na uwezo wa mwili wako unaweza kumudu mahitaji ya kazi husika.Kuna wakati unatamani Kama ungefanya kitu na unaamini unaweza lakini mwili na akili yako vinakosa ushirikiano
:
Bado nitaendelea kumkumbuka Ibrahimu rajabu “Jeba”(marehemu) Alionekana ana uwezo mkubwa kisoka lakini Kila alipotaka kujaribu kutuonyesha kile alichojaliwa miguuni mwake kwa dakika zaidi ya 60 basi mwili wake ulimkataa.Na Kama angeamua kulazimisha basi kwa wale wanaosubili wafunguliwe geti dakika 10 za mwisho Basi wangeingia na kusema hakuna mchezaji hapo,Kumbe mwili wake ulikuwa unainyima akili yake ushirikiano
:
Inaumiza,inasikitisha na inahuzunisha kila ninapoitazama sura ya Shomary Salum Kapombe akiwa uwanjani.As canes hawakuwa wajinga kumsafirisha Kapombe mpaka ufaransa,Kuna kitu walikiona.Tuna mabeki zaidi ya 30 wa kulia ndani ya Timu zetu 20 za VPL lakini tuna Kapombe mmoja tu
:
Sina maana wengine hawakabi na kupandisha mashabulizi,lakini Kapombe anafiti kwenye mfumo wowote ambao kocha amepanga kumtumia.Lakini kwasasa muda mwingi anautumia zaidi kitandani kuliko uwanjani na Kuna vitu vingi vimepungua kwake
:
Mpira ndio kazi inayoendesha maisha ya Kapombe,bahati mbaya wachezaji wetu wengi wakianza kufanikiwa kisoka Elimu kwao unageuka msamiati.kiufupi Kapombe Hana kazi mbadala nje ya soka vinginevyo Kama Kuna miradi ameijenga kwa Sasa kupitia soka
:
Majeruhi ya mara kwa mara yamemfanya Kapombe apoteze kujiamini,Kuna wakati hatamani akabane na mpinzani kwasababu anahofia majeruhi.Kila akichezewa faulo ukimtaza sura yake Inatia huruma mno,Kuna wakati Kapombe viwanja vya mikoani ataomba asicheze kwa kuhofia vichuguu, Kwasababu mwili wake umekosa utimilifu na hivyo kupelekea hofu ya kupoteza ajira yake kwasababu ya majeruhi.
:
Wiki chache zilizopitwa Kuna ujumbe ulizagaa mitandaoni,Kwa masikitiko makubwa Kapombe akatangaza kustaafu kuichezea Timu ya taifa akiwa na miaka 27 tu. Inasikitisha Sana umri ambao jemmy vard alikuwa hafahamiki Wala kufikiria kuitwa national team lakini majeruhi yanamstaafisha Kapombe katika umri mdogo mno
:
Inaendelea

YALIYOJIRI GAME YA SIMBA VS PRISONS!

:
1. Prisons ni timu iliyo bora sana kuanzia eneo la ulinzi mpaka kiungo wanacheza kwa nidhamu sana na wanacheza kitimu sana shida ipo kwenye final third yao wanapoenda kushambulia hawana wachezaji wenye uchu wa kupata magoli!!
:
2. Adolf Rishard, watu wanalalamika Simba kutoshinda ila kwanza wanatakiwa wampongeze Adolf Rishard kwa kutengeneza timu ya ushindani, ngumu kufungika na yenye nidhamu ya mchezo!!
:
3. Pengo la Bocco linamtesa sana Aussems anakosa options baada ya kukosa aina ya wachezaji kama Bocco mwenye uwezo wa kushambulia kutokea pembeni na kupambana na mabeki wagumu kuwafanya mabeki kuwa na kazi nyepesi ya kumkaba Kagere peke ake!!
:
5. Watu wanampa sifa sana Salum Kimenya ila Ismail Michael ni mchezaji hatari sana na naona kama anaweza kututatulia tatizo la beki namba mbili kama atapata nafasi ya kucheza mechi nyingi za ushindani!!
:
6. Prisons walistahili kupata zaidi ya walichokipata ila bahati haikuwa upande wao na pia ubora wa Manula umewanyima nafasi ya kuondoka na pointi 3 na Simba kupata pointi 1 kwa game ya jana ilikuwa BONUS!!
:
7. Natamani kila weekend tushuhudie game kama hizi ili tutengeneze wachezaji wenye ushindani na kupunguza lawama kwa makocha wa timu ya taifa pindi wanapoita wachezaji!!!
:
Prepared @karimkondo
Powered by @bikotanzania

MATOKEO YA SOKA JANA +RATIBA YA SOKA LEO

:
#VodacomPrimierLeague
FT Simba Sc 0-0 Tanzania Prisons
:
#UefaEuropaLeague
FT APOEL Nicosia 2 – 1 Qarabag FK FT F91 Dudelange 2 – 5 Sevilla
FT FC Koebenhavn 1 – 1 Dynamo Kyiv
FT Lugano 0 – 0 Malmoe FF
FT Basel 2 – 1 Getafe
FT FC Krasnodar 3 – 1 Trabzonspor
FT LASK 4 – 1 PSV Eindhoven
FT Rosenborg 0 – 2 Sporting CP
FT CFR Cluj 1 – 0 Rennes
FT Lazio 1 – 2 Celtic
FT Standard Liege 2 – 1 Eintracht Frankfurt
FT Feyenoord 1 – 1 Young Boys
FT Rangers 2 – 0 FC Porto
FT RCD Espanyol 6 – 0 Ludogorets Razgrad
FT Ferencvaros 0 – 0 CSKA Moscow
FT Oleksandriya 2 – 2 Saint-Etienne
FT Wolfsburg 1 – 3 Gent
FT Borussia Mönchengladbach 2 – 1 Roma
FT Wolfsberger AC 0 – 3 Istanbul Basaksehir
FT SC Braga 3 – 1 Besiktas
FT Wolverhampton Wanderers 1 – 0 Slovan Bratislava
FT FC Astana 0 – 5 AZ Alkmaar
FT Manchester United 3 – 0 Partizan Beograd
:
#WorldCup U-17 – Play-off
FT Ecuador 0 – 1 Italy
FT Paraguay 3 – 2 Argentina
:
KAMATA RATIBA YA SOKA LEO
:
#VodacomPrimierLeague
16:00 Ndanda SC vs Yanga SC
19:00 Azam Fc Vs Biashara Mara
16:00 KMC vs Kagera Sugar
:
#EnglandPremierLeague
23:00 Norwich City vs Watford
:
#SpainLaLigaSantander
23:00 Real Sociedad vs Leganes
:
#ItalySerie A
22:45 Sassuolo vs Bologna
:
#GermanyBundesliga
22:30 1. FC Köln vs Hoffenheim
:
#FranceLigue 1
22:45 Nice vs Bordeaux
:
#BelgiumFirstDivision A
22:30 Zulte Waregem vs Anderlecht
:
#SouthAfricaPremierLeague
21:00 Bidvest Wits vs SuperSport United
21:00 Maritzburg United vs Bloemfontein Celtic

Prepared by @officialchristz
Powered by @bikotanzania

Design a site like this with WordPress.com
Get started