
1: Bado changamoto kubwa ya Aussems ni kutofanya research ya kuwajua wapinzani wake. Prison ni aina ya timu inayohitaji kupigwa presha pembeni sio kufosi kupita katikati. Plan yake ndio kitu cha kwanza kilichoighairmu Simba kabla ya kutazama wachezaji.
2: Adolf Richard🙌 Fantastic approach 🙌 Haikushangaza leo Mkandala kutokea benchi. Ni mpango aliokua nao baada ya kujua madhaifu ya mpango wa Simba.
3: Mkandala🙌 What a player🙌 Ni miongoni kwa viungo watatu wanaonivutia msimu huu. Kama Manula angeamka vibaya leo, pengine mechi ingeamuliwa mguuni mwake.
4: Ni Aussems pekee anaejua kwanini Muzamir Yassin alikaa benchi na kwanini Miraj hakuwepo kabisa kwenye kikosi
5: Kama refa angekua makini, Kagere alistahili kadi nyekundu. Anafunga sawa, but Meddie ni miongoni mwa watu wasiokiwa na furaha uwanjani. Viungo wake wanampa wakati mgumu wa kucheza.
6: Yule Buha🙌 (Kiungo mkabali wa Prison) Anakaba hadi kivuli. Pressing yake iliwanyima uhuru kabisa Chama na Shiboub
7: Benjamin Asukile na Kimenya🙌 wachezaji wawili muhimu walioilewa vyema plan ya Adolph, kipindi cha kwanza. Wangekua makini pia, mechi ingeamuliwa kwao.
8: Bado Aussems ana changamoto ya kujua ni nani anastahili kua namba 10 wa Kagere. Kahata, Shiboub, Chama, Ajib wote wanaingia kwenye jukumu hilo na kushindwa kutoa Plan B kwa timu, inapokuwa
haina mpira.
9: Deo Kanda🤔 Ni kama alikwenda kumpaka poda mdoli. Hakua na impact yoyote zaidi ya kukimbia nje ya mpango wa timu.
10: Mkude 🤔 Ni mchezaji mzuri lakini hakustahili kurejea katika mechi ngumu kama hii. Muunganiko wa timu kutoka safu ya kiungo ya chini kwenda juu, ilikua tofauti na anapocheza Fraga au Muzamir
.
.
Nb: Muandalieni vipindi kabisa na Uchebe😃